darcity
JF-Expert Member
- Jul 20, 2009
- 8,719
- 16,932
Kwanza nimefurahishwa na uamuzi wa Rais Kikwete kuhusu uamuzi wake wa kuhakikisha kwamba tunakuwa na katiba mpya.Hii inajenga msingi imara wa maendeleo ya demokrasia pamoja nauwajibikaji wa serikali na wananchi wa Tanzania kwa ujumla.
Kama Mtanzania mwenye uchungu wa nchi yake, nachukua nafasi hii kutoa maoni yangu na ningependa Watanzania wenzangu mniunge mkono katika suala hili kwa manufaa ya taifa letu kwa siku zinazokuja.Ningependa maoni haya yasiishie kwenye mjadala huu tu wa kwenye website hii ya tume ya kukusanya maoni ya katiba, bali pia wakati wajumbe wanaokusanya katiba wakipita maeneo mbali mbali hapa nchini wayasikie midomoni mwenu. Ndiyo sauti ya wengi siku zote hushinda! kama wahenga wetu walivyopata kusema, ''wengi wape''
Sekta ya madini hivi sasa inakuwa kwa kasi. Kwa watu makini hili ni ashirio zuri kwa taifa na hasa uchumi wa taifa. Lakini bado haimaanishi kwamba kukua huku kwa kasi kunaambatana n aukuaji wa kasi wa usalama wa taifa letu kiuchumi na kijamii.Tanzania ina hifadhi ya mamilioni ya tani za dhahabu,almasi,shaba,makaa ya mawe,chuma cha pua,gesi carat,nikel n.k lakini bado umaskini ni wa kutupwa kwa raia wake.Pitia mitandao mbali mbali uone tunavyosanifiwa kwa umaskini wa watu wetu na utajiri wa taifa letu. Pengine hili ndilo linalonifanya niandike maoni haya.
Ili kuhakikisha usalama wa kiuchumi wa taifa letu inabidi sasa katiba mpya ibainishe wazi kwamba sekta ya madini ni miongoni mwa vipaumbele vya usalama wa taifa. Usalama wa taifa sio tu kuwa na amani ya kisiasa na amani ya mpakani bali pia amani ya kiuchumi, hii muhimu kwa taifa na hata mwananchi wa kawaida anayekabiliwa na umaskini wa kutupwa. Tumezoea kuambiwa kwamba tanzania ni nchi yenye amani,lakini ukweli ni kwamba amani hiyo haipo kwani mamilioni ya wananchi wake wako katika dhiki kubwa huku nafsi zao zikiwa na hofu ya kuamka kesho na kupata riziki zao.
Wakati tunatumia jitihada nyingi kulinda mipaka yetu na maadui wa ndani,tumesahau kwamba hivi sasa kumeibuka wimbi la maadui wapya wa ndani, hawa ni wafujaji wa mali za umma,wala rushwa na wakwapuaji wa fedha za umma. Ndio, hawa ndio maadui wakubwa wa usalama wa taifa letu kwa hivi sasa wakiendeshwa na tamaa na ubinafsi wa kupindukia kupitia mamlaka waliyopewa kisheria kuingia mikataba mibovu isiyo na tija kwa taifa. Ni wakati muafaka sasa kupambana nao kupitia sauti zetu.Ni wakati wa kupigania madini na rasilimali zetu dhidi ya watu wachache wasio na uzalendo wala uchungu wa taifa lao.Ni wakati ambao tunapaswa kuiga taifa la Marekani ambalo baada ya kuona linatishiwa kunyimwa mafuta na mataifa ya kiarabu katika miaka ya sabini ikaamua kuweka mafuta kuwa miongono mwa vipaumbele vya usalama wa taifa lao! inakuwaje sisi wenye wingi wa rasilimali na madini tusifanye hivo?
MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU IBARIKI AFRIKA
Mtoa maoini- darcity8@gmail.com
Shirikiri kwenye mjadala katika tovuti ya tume ya katiba mpya,
MADINI YAWE SEHEM YA USALAMA WA TAIFA
Kama Mtanzania mwenye uchungu wa nchi yake, nachukua nafasi hii kutoa maoni yangu na ningependa Watanzania wenzangu mniunge mkono katika suala hili kwa manufaa ya taifa letu kwa siku zinazokuja.Ningependa maoni haya yasiishie kwenye mjadala huu tu wa kwenye website hii ya tume ya kukusanya maoni ya katiba, bali pia wakati wajumbe wanaokusanya katiba wakipita maeneo mbali mbali hapa nchini wayasikie midomoni mwenu. Ndiyo sauti ya wengi siku zote hushinda! kama wahenga wetu walivyopata kusema, ''wengi wape''
Sekta ya madini hivi sasa inakuwa kwa kasi. Kwa watu makini hili ni ashirio zuri kwa taifa na hasa uchumi wa taifa. Lakini bado haimaanishi kwamba kukua huku kwa kasi kunaambatana n aukuaji wa kasi wa usalama wa taifa letu kiuchumi na kijamii.Tanzania ina hifadhi ya mamilioni ya tani za dhahabu,almasi,shaba,makaa ya mawe,chuma cha pua,gesi carat,nikel n.k lakini bado umaskini ni wa kutupwa kwa raia wake.Pitia mitandao mbali mbali uone tunavyosanifiwa kwa umaskini wa watu wetu na utajiri wa taifa letu. Pengine hili ndilo linalonifanya niandike maoni haya.
Ili kuhakikisha usalama wa kiuchumi wa taifa letu inabidi sasa katiba mpya ibainishe wazi kwamba sekta ya madini ni miongoni mwa vipaumbele vya usalama wa taifa. Usalama wa taifa sio tu kuwa na amani ya kisiasa na amani ya mpakani bali pia amani ya kiuchumi, hii muhimu kwa taifa na hata mwananchi wa kawaida anayekabiliwa na umaskini wa kutupwa. Tumezoea kuambiwa kwamba tanzania ni nchi yenye amani,lakini ukweli ni kwamba amani hiyo haipo kwani mamilioni ya wananchi wake wako katika dhiki kubwa huku nafsi zao zikiwa na hofu ya kuamka kesho na kupata riziki zao.
Wakati tunatumia jitihada nyingi kulinda mipaka yetu na maadui wa ndani,tumesahau kwamba hivi sasa kumeibuka wimbi la maadui wapya wa ndani, hawa ni wafujaji wa mali za umma,wala rushwa na wakwapuaji wa fedha za umma. Ndio, hawa ndio maadui wakubwa wa usalama wa taifa letu kwa hivi sasa wakiendeshwa na tamaa na ubinafsi wa kupindukia kupitia mamlaka waliyopewa kisheria kuingia mikataba mibovu isiyo na tija kwa taifa. Ni wakati muafaka sasa kupambana nao kupitia sauti zetu.Ni wakati wa kupigania madini na rasilimali zetu dhidi ya watu wachache wasio na uzalendo wala uchungu wa taifa lao.Ni wakati ambao tunapaswa kuiga taifa la Marekani ambalo baada ya kuona linatishiwa kunyimwa mafuta na mataifa ya kiarabu katika miaka ya sabini ikaamua kuweka mafuta kuwa miongono mwa vipaumbele vya usalama wa taifa lao! inakuwaje sisi wenye wingi wa rasilimali na madini tusifanye hivo?
MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU IBARIKI AFRIKA
Mtoa maoini- darcity8@gmail.com
Shirikiri kwenye mjadala katika tovuti ya tume ya katiba mpya,
MADINI YAWE SEHEM YA USALAMA WA TAIFA