Boney E.M.
JF-Expert Member
- Jan 22, 2007
- 425
- 35
Tanzania tunazo nguzo nyingi za simu zilizojengwa na makampuni ya simu lakini suala na madhara yake halijawekwa bayana wakati tunavyo vyombo husika kama TCRA. Inashangaza na kuona kwamba wananchi wako katika hatari kubwa ya madhara ya kiafya bila hatua za haraka kuchukuliwa. Imebainika katika utafiti uliofanywa huko Botswana na katika maeneo mengi kama nane yaliofanyiwa utafiti duniani, watu wanaokaa karibu na nguzo za simu wanapata madhara ya kiafya kama kuumwa sana na kichwa, uchovu mwingi, kutopata usingizi mzuri, matatizo ya tumbo, shinikizo la damu, mapigo ya moyo kutokuwa sawa, kiungulia, matatizo ya ngozi, kupoteza kumbukumbu, upungufu wa kinga mwilini, maungo kuuma, kizunguzungu, kansa, kifafa n.k.
Tanzania ina tabia ya kudharau tafiti kama hizi na pindi zinapoongelewa kama Bungeni utaona mazungumzo yanapotoshwa na wahusika wakati wananchi wanaendelea kudhurika. Kuna haja ya taarifa kamili kutolewa na TCRA pamoja na serikali kuhusu madhara ya nguzo za umeme karibu na makazi ya watu.
Kwa kuwa tafiti zilifanywa huko Afrika Kusini, Ujerumani, Austria na Israel zimeonyesha matokeo yanayofanana hususan magonjwa hayo serikali ionyeshe nia ya wazi ya kuwakinga wananchi wake.
Nukuu: The Guradian, 20 October 2009, page (iii)
Tanzania ina tabia ya kudharau tafiti kama hizi na pindi zinapoongelewa kama Bungeni utaona mazungumzo yanapotoshwa na wahusika wakati wananchi wanaendelea kudhurika. Kuna haja ya taarifa kamili kutolewa na TCRA pamoja na serikali kuhusu madhara ya nguzo za umeme karibu na makazi ya watu.
Kwa kuwa tafiti zilifanywa huko Afrika Kusini, Ujerumani, Austria na Israel zimeonyesha matokeo yanayofanana hususan magonjwa hayo serikali ionyeshe nia ya wazi ya kuwakinga wananchi wake.
Nukuu: The Guradian, 20 October 2009, page (iii)