Elections 2010 Madhara ya kutokumtambua Rais

WanaJF wakereketwa wa CDM, HAKUNA madhara!!!!!!!!!!!!!! Anaye-advocate kwamba kuna madhara hatutakii mema!!!!! Ukombozi ni vita !!!!!!!!!!!!! CDM ina wasomi kupindukia na wanaelewa vyema kabisa wanachofanya!!!!!!!!!!!! Hapa ni vita ya kung'oa mizizi ya ufisadi/ushirikina/uchawi/ujinga/maradhi na mengine yota yatokanayo!!!!!!!!!!! Pipoos Pawaaaaaaaaaaaaaaaaa! Tumieni vyema fimbo ya Serekali Kivuli bungeni kupindua kila jiwe!!!!!!!!!!!!! Nguvu ya Umma iko nyuma yenu!!!!!!!!! Mkisahau kumbuka ile nguvu iliyoonekana Nyamagana, MBY,ARU, MSM, IRA, MSH,UBNGO, KAWE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Uamuzi wa CHADEMA kwamba wabunge wao watasikiliza hotuba ya rais wakati wanasema hawamtumbui unachanganya mambo. Kama rais hawamtambui hawana haja ya kumsikiliza bungeni. Sasa wakichangia hiyo hotuba watakuwa wanamnukuu kama nani?
 
Uamuzi wa CHADEMA kwamba wabunge wao watasikiliza hotuba ya rais wakati wanasema hawamtumbui unachanganya mambo. Kama rais hawamtambui hawana haja ya kumsikiliza bungeni. Sasa wakichangia hiyo hotuba watakuwa wanamnukuu kama nani?

Kwani hivi sasa wanapoongea habari zake wanamtaja kama nani? kama hawamtambui kwa wadhifa wa urais lakini wanamtambua kwa jina lake la Jakaya Kikwete.
 
Madhara yapo sana hasa kwa JK mwenyewe ndo maana hata wabunge wa CHADEMA walioko Dodoma wanatakiwa kutoka nje ya ukumbi wa bunge mara JK atakapoanza kuhutubia..tena ikiwezekana wachukue draft na karata wawe wanacheza kabisa muda wote wa hotuba yake..akimaliza basi warudi ndani au waende zao chako ni chako kula kuku..Hiyo itatuma salamu very clear kuwa JK hupendwi na umeiba kura kuwa rais

lakini si wamekula kiapo kushirikiana naye?
 
Mimi siamini kabisa katika huo mpango wa kumkimbia mdhulumu wao. kutoka nje maanake umkwepa m babe wako. kutoka nje ni ishara ya woga. JK atatanga baraza lake la mawaziri kuunda serikali, inamaana serikali dhalimu ikiwa bungeni basi wasusie bunge kwa ujumla wake? Physchological battle haiendi hivyo. CHADEMA wanatakiwa wafanye kile walichomfanyia PINDA, wakati wao wanashangilia CHADEMA piga kimya, kwenye kura mnamkataa. ile kitu imemuuma sana Pinda. maana anaelewa kwanini imekuwa hivyo. hawakumkataa Pinda kama Pinda bali wamkataa kama ishara ya kuikataa serikali dhalimu.

Hakuna kususia vikao vya bunge hata akija nani bungeni. cha kukataa ni kile atakachokileta huyo asiekubalika.

CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani wanatakiwa kuisikiliza kwa makini hiyo hotuba ya JK ana kutumia fursa ya wakati wa kuijibu fungua madukuduku yao yaliowakaa moyoni kuhusu uhalali wa JK na NEC yake.

CHADEMA lazima watumie vizuri zana chache walizo nao. hivi sasa wana zana kuu tatu:
1. Uongozi wa upinzani Bungeni. 2. Wabunge imara 3. Wananchi.

Iwapo watatumia hizo zana tatu kwa ustaha hakika watawafanya baya CCM A na B pamoja na serikali yao.

CHADEMA Mungu kawajalieni top management team zaidi 90% yote ipo bungeni tutawashangaa kama mkituangusha

Naona wewe ni chief whip wa ccm unabembeleza

1. Watapewa hotuba hiyo kabla ya kikao so wanaweza kuisoma popote walipo na kuielewa
2.uimara hauletwi na kumsikiliza mwizi wa kura
3.wananchi walimkataa ndio maana wako nyuma ya wabunge watakaotoka nje ya ukumbi wa bunge
 
Wana jf naombeni mnisaidie katika hili, hivi Tamko la Dk slaa kwamba Chadema haimtambui JK kama rais wa Nchi lina madhara yeyote kwa CCM au serikali iliyopo madarakani? na mimi kama mwana-CHADEMA nifanye nini ili kuonyesha kwamba simtambui Rais?. Maana majuzi nilitaka nikatae kumpisha barabarani kwasababu na mimi simtambui kama ni rais wa Tanzania lakini roho yangu ilisita kidogo.

Bora ulitumia mawazo yako mwenyewe,ungepata kichapo mjomba.
 
Wana jf naombeni mnisaidie katika hili, hivi Tamko la Dk slaa kwamba Chadema haimtambui JK kama rais wa Nchi lina madhara yeyote kwa CCM au serikali iliyopo madarakani? na mimi kama mwana-CHADEMA nifanye nini ili kuonyesha kwamba simtambui Rais?. Maana majuzi nilitaka nikatae kumpisha barabarani kwasababu na mimi simtambui kama ni rais wa Tanzania lakini roho yangu ilisita kidogo.

Usije tia ngumu mbele ya msafara wa mwenye mamlaka ya Uprez.
hata kuua yeye ila wapambe wake
Hata Ibilisi huko kuzimu ana nguvu zake nyingi tu ukitaka kumseta ni lazima umbane kiroho. Physically atakumaliza.

prez anapata nguvu pale watu wanao nyanyaswa na uwepo wake wasimamapo kidete kumtetea kwa mazoea na bila kuwa na hoja ya maana.

Kuongea na marafiki majirani na wasafiri wenzako juu ya negatives za system nzima na kuhitimisha na kuunga mkono tamko la Dr Slaa ni msimamo tosha uletao tija katika zoezi zima la kugomea matokeo.
 
nitashukuru sana kama msimamo huu wa chadema utapata nguvu ya kisheria. vinginevyo, tutanuna kwa miaka yote mitano ijayo na kupunguza concentration yetu ya kilichotupeleka mjengoni. lakini nawapa big up my good people of tanzania kwa mshikamano wa dhati kipindi chote cha uchaguzi, utangazwaji wa matokeo hadi leo.
 
kinachotakiwa ni kuuonyesha ulimwengu kuwa wamedhurumiwa. Na ungwana ndio huo kutomsikiliza... watanzania hatutapigana kama majirani zetu
 
wana jf naombeni mnisaidie katika hili, hivi tamko la dk slaa kwamba chadema haimtambui jk kama rais wa nchi lina madhara yeyote kwa ccm au serikali iliyopo madarakani? Na mimi kama mwana-chadema nifanye nini ili kuonyesha kwamba simtambui rais?. Maana majuzi nilitaka nikatae kumpisha barabarani kwasababu na mimi simtambui kama ni rais wa tanzania lakini roho yangu ilisita kidogo.

yaani ungefanya hivyo ndio ungekijua kilichomnyoa kanga manyoya. Ungeozea segerea. Yupo mzungu aliwahi kuingilai mafara wa jk aliozea segera na alipotoka akajiua.

Ni lazima tutofautishe shughuli za kisiasa na kisheria. Chadema wanasema hawamtambui rais kisiasa lakini
wanalazimika kumtambua kisheria kutokana na katiba na sheria vyetu kuwa vibaya. Tupende tusipende chadema watalazimika kushirikiana na kumtii rais katika shughuli za kisheria na sio za kisiasa tu. Hivyo na sisi raia wafuasi wa chadema tunatakiwa kutomtambua na kumtii jk katika shughuli za kisiasa tuu kama vile kutohudhuria mikutano yake na kusikiliza hotuba zake kama tulivyokuwa tukifanya zamani; lakini tutalazimika kumtii kisheria ama sivyo tutakuwa tunavunja sheria na kutenda makosa ya jinai.

Japo mtu/watu wanaweza kudai kuwa kutomtambua rais kisias haitaithiri chochote, si kweli kutokana na jk kujua kuwa sehemu kubwa ya jamii anayoiongoza haimtambui kisiasa hatakuwa na amani kama aliyokuwa nayo katika kipindi cha miaka kmitano ya uongozi wake. Ni wazi kuwa tutakuwa tunamuathiri kisaikolojia yeye na ccm yake. Kwa kuwa siasa za tanzania zinaendeshwa kwa umungu utu, wa wanasiasa wa ccm kutaka kuonekana wanakubalika na watu wote hio litakuwa ni pigo kubwa sana kwao.
 
Wana jf naombeni mnisaidie katika hili, hivi Tamko la Dk slaa kwamba Chadema haimtambui JK kama rais wa Nchi lina madhara yeyote kwa CCM au serikali iliyopo madarakani? na mimi kama mwana-CHADEMA nifanye nini ili kuonyesha kwamba simtambui Rais?. Maana majuzi nilitaka nikatae kumpisha barabarani kwasababu na mimi simtambui kama ni rais wa Tanzania lakini roho yangu ilisita kidogo.

Hakuna athari yoyote kwa tamko hilo, kwani ni Rais anawekwa kwa mujibu wa katiba ambayo ndiyo hiyo hiyo imewaweka wabunge wa CHADEMA hapo walipo. Na isitoshe kutomtambua Rais hiyo ni nadharia zaidi kuliko kivitendo, kwani hata km humtambui kodi atakusanya, na huwezi kusema usilipe kodi, nk. Kwa ujumla halina athari , na hata mataifa ya nje yameisha toa tamko kuwa wapo tayari kufanya kazi na JK, ambapo CHADEMA ndio wanategemea wapeleke malalamiko yao ili nchi inyimwe misaada, THINKTWICE !
 
Back
Top Bottom