Black Rose
JF-Expert Member
- Nov 21, 2011
- 243
- 171
Suala la Wabunge na posho ya 330,000/= kwa siku kupitishwa na Rais, na huku Waziri Mkuu akiwaamuru madaktari warudi kazini mara moja akiwatishia kuwafukuza kazi wakikaidi ni kwa hasara ya SERIKALI!
Unaposhindwa kufikia muafaka kwenye mambo ya msingi, unajitafutia tatizo kubwa zaidi.MUAFAKA haufikiwi kwa kuwa na double standards.Hakuna mahali popoye duniani, amani na mafanikio vimetawala kwa vile nguvu na upendeleo vilitumika.
Madaktari siyo kama makarani useme wakilazimishwa kurudi kazini, utawalazimisha kuandika na kupeleka makabrasha unapotaka wewe mwajiri.Pia siyo kama wafanyakazi wengine useme hata wakivuta miguu hakuna madhara.Hawa wameshikilia roho za watu tena wengi ni maskini, mikononi mwao.
Serikali hamlioni hili?
Na nyie wabunge kwanini mnatafuta kutuletea balaa sisi wapiga kura tuliowachagua?
Unaposhindwa kufikia muafaka kwenye mambo ya msingi, unajitafutia tatizo kubwa zaidi.MUAFAKA haufikiwi kwa kuwa na double standards.Hakuna mahali popoye duniani, amani na mafanikio vimetawala kwa vile nguvu na upendeleo vilitumika.
Madaktari siyo kama makarani useme wakilazimishwa kurudi kazini, utawalazimisha kuandika na kupeleka makabrasha unapotaka wewe mwajiri.Pia siyo kama wafanyakazi wengine useme hata wakivuta miguu hakuna madhara.Hawa wameshikilia roho za watu tena wengi ni maskini, mikononi mwao.
Serikali hamlioni hili?
Na nyie wabunge kwanini mnatafuta kutuletea balaa sisi wapiga kura tuliowachagua?