Madereva wa Tanzania waswekwa lupango Rwanda: kisa chakachua

Ngambo Ngali

JF-Expert Member
Apr 17, 2009
3,517
1,359
ABOUT 100 Tanzanian truck drivers have been detained by police in Rwanda, Burundi and the Democratic Republic of Congo (DRC) allegedly for stealing products from the tankers while on transit.

The Chairman of Tanzania Trucks Owners Association (TATOA), Mr Zacharia Poppe, confirmed the information yesterday. He told a ‘Daily News’ reporter in Kigali that the drivers were seized at different times at border points into the countries last week.

According to Mr Poppe, the drivers are alleged to be stealing the petrol and diesel from the tanks on transit and then fill them with kerosene or paraffin to maintain the volume. Kerosene or paraffin used for lighting in rural areas is tax free in the country making it cheaper than petrol and diesel.

He said that the drivers were detained in the countries after he (Mr Poppe) reported the matter to the respective authorities in the three countries to help curb the problem that he said was becoming rampant.

“The drivers offload a certain quantity of diesel or petrol from the tanks and fill it with same quantity of kerosene and then sell the stolen diesel or petrol and pocket the proceeds,” he said.

Mr Hanspoppe said he is certain that some individuals in such authorities as Tanzania Revenue Authority (TRA), Energy Water Utilities Regulatory Authority (EWURA) as well as police were allegedly colluding with untrustworthy drivers in what he described as ‘dirty business’ that is earning them good money.

However, the Director of Petroleum at EWURA, Mr Sirili Massay, said that the authority did not deal with the drivers on transit directly. He said that there were many companies that are supplied with the products by EWURA and might be dealing with such drivers.

Mr Massay said, however, that EWURA would soon introduce special tools that would help detect the petrol and diesel that are nitrified by other products while on transit
. Sources from the Tanzania Revenue Authority (TRA) told the ‘Daily News’ that the authority did not deal with the trucks once they were out of the country.

TRA only monitors the trucks while in the country to ensure the products on transit are not sold in the country. When reached for comments, the Police Spokesperson, Mr Abdallha Mssika said that the police have not yet received the information and promised to make a follow- up.
 
Good job on the part of Rwanda. Hawa jamaa utapeli wa Kitanzania wameanza kuu export katika nchi jirani ngoja waswekwe lupango tu.
 
kuna mtu hawajui wabongo? magari yetu tu hapo Dar tunajaziwa mafuya ya maji na mafuata yaliyochanganywa kila siku. sheli kibao zilikuwa nusura zifungiwe, wenyewe wanafikiri kila nchi ina shortcuts za kihuni hizo. nafikiri watatoa fundisho zuri. gud job....
 
Hii issue ya EAC tutajaza jela za nchi nyingine huu ugoigoi wetu huu na ujanja wetu wa kishamba we subiri tu
 
shukrani kwa Mr Zacharia Poppe; hawa jamaa hata hapa bongo wana tuharibia magari sana kwa kuchanganya mafuta sasa wamekwenda kwa watu serious makubwa yanawakuta.

Nafurahi kuona vijana wa Mwema na wahusika wengine katika kukomesha uharifu huu wanafundishwa kazi na wenzao
 
shukrani kwa Mr Zacharia Poppe; hawa jamaa hata hapa bongo wana tuharibia magari sana kwa kuchanganya mafuta sasa wamekwenda kwa watu serious makubwa yanawakuta.

Nafurahi kuona vijana wa Mwema na wahusika wengine katika kukomesha uharifu huu wanafundishwa kazi na wenzao
So u r not serious n u knw it n funny enough u r not doing anythng abt it ahhahahahaha
 
Rwanda yarejesha malori 18 ya mafuta yaliyochakachuliwa




Na Richard Makore



23rd June 2010


email.png




printer.png




comment_bubble.png







headline_bullet.jpg
TRA wasema watakiona cha moto
headline_bullet.jpg
Ewura yachunguza sampuli zake




Sakata la kuchakachua mafuta hapa nchini limeingia katika sura mpya, baada ya maroli 18 yaliyokuwa yamebeba bidhaa hiyo kurudishwa Tanzania kutoka Rwanda kwa madai kuwa shehena iliyokuwa imebebwa ilikuwa imechakachuliwa.
Nipashe ilipata taarifa kutoka vyanzo vya kuaminika kuwa malori hayo yalirejeshwa nchini wiki iliyopita, baada ya mamlaka za Rwanda kuyakataa.
Kutokana na hali hiyo, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetaka kampuni zilizosafirisha mafuta hayo kutoa maelezo.
Mamlaka hiyo imeshangazwa na hali hiyo kwa kuwa kabla mafuta hayo hayajasafirishwa kwenda Rwanda iliyakagua na kujiridhisha kuwa yalikuwa safi na kufikia viwango ndipo iliporuhusu yasafirishwe kwenda huko.
Akizungumza na Nipashe ofisini kwake jana, Mkurugenzi wa Elimu na Idara ya Walipa Kodi wa TRA, Protas Mmanda, alithibitisha kuwa mamlaka yake inayashikilia malori hayo tangu mwishoni mwa wiki.
Mmanda alisema kuwa malori 15 wanayashilikia katika ghala lao lililopo Kibaha mkoani Pwani na matatu yamekwama njiani baada ya kuharibika wakati yakirejeshwa nchini kutoka Rwanda.
Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa malori mawili yaliharibikia mkoani Dodoma na moja mpakani mwa Tanzania na Rwanda eneo la Rusumo.
Mmanda alisema kuwa ikiwa mafuta hayo yatapimwa na kuonekana yalichanganywa na mafuta ya taa, TRA itayabana makampuni yaliyoyasafirisha ili yalipe kodi ya Sh. milioni 340 pamoja na adhabu ya Dola za Marekani 10,000 (Sh.13,930,000) kwa kila kampuni itakayobainika kuhusika.
Alisema malori hayo yalikamatwa muda mrefu huko Rwanda yakitokea Tanzania, lakini akasema kama kuna matatizo yatakuwa yamesababishwa na wamiliki wa kampuni zilizoyasafirisha kutoka Dar es Salaam kwa kuwa wao waliyakagua na kuridhika kabla malori hayo kuondoka.
Mmanda alisema mafuta hayo hayakulipiwa kodi kwa kuwa yalikuwa yanasafirishwa kwenda nje na kwamba kama yamerudishwa na yakabainika kuwa yamechakachuliwa lazima wayabane makampuni husika ili yalipe mapato ya serikali.
"Kila gari linapopakia mafuta, maofisa wetu wa TRA wanakuwepo, hivyo suala la kuchakachua mafuta hapa nchini sio rahisi kwa kuwa zoezi lote lilisimamiwa kikamilifu," alisema.
Kwa upande wake, maofisa wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), walipoulizwa kuhusiana na suala hilo, walithibitisha na kuongeza kuwa wamechukua sampuli za bidhaa hiyo kwa ajili ya kwenda kuipima kama ilichakachuliwa.
Mmoja wa ofisa wa Ewura aliliambia Nipashe kuwa upimaji wa sampuli hiyo huchukua kati ya siku nne hadi saba kabla ya kutoa matokeo.
Alisema matokea hayo yatatolewa hadharani ili kila mtu aweze kuyajua kwa lengo la kupambana na tatizo hilo la kuchakachukua mafuta.
Hivi karibuni, tatizo hilo limezidi kushamiri ambapo mwezi uliopita magari ya Ikulu yaliwekewa mafuta yaliyochakachuliwa mkoani Kilimanjaro na kuyafanya yashindwe kuwaka.



CHANZO: NIPASHE
 
Maskini Madereva hawana hatia, dhambi ya mabosi wao na uzembe wa viongozi wao unawaweka pabaya tena ugenini.
Ewura walishasema dawa ni kuongeza ushuru wa mafuta ya taa ili uwe sawa na wa diseli.(Very poor idea)
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom