Madereva wa Mabasi yaendayo mikoani tokea Ubungo wamegoma!

Mimi niliondoka, vipi kuna updates zozote? maana sasa nimeshapita Chalinze nipo kwene Coaster but hakuna basi lolote lililotupita
 
Naambiwa kuna basi la kusini liliondoka wadau wamelifukuza wamemtandika dereva yuko hoi na vioo wamevunja

Ni kweli, ni basi la Southern linakwenda Mtwara, Fatima limebaki kando, naona hata madereva wamekua na mshikamano wa ajabu, nilimwacha Kova na FFU wake ila uwezekano wa kusolve ni mdogo sana, they are determined to achieve wht they demand!!!
 
mabasi yote yametoka na pana foleni kubwa hapa ubungo sijui huko njiani racing yake itakuwaje! ila wamehaidiwa kufanya kikao jumanne pamoja na wamiliki wote
 
Huu ndio ubepari wenyewe, tuliukubali bila kuujua sawasawa; tajiri anawanyonya wafanyakazi wake!

Madai yao ni ya haki kabisa; nakumbuka enzi za Mwaibula SUMATRA walijaribu kuweka sawa maslahi ya madereva lakini hawakumpa ushirikiano hadi alipoodoka hatukuona mabadiliko.

Iwapo safari isingekuwepo leo na wamiliki wa mabasi wakapata hasara ya kurudisha nauli labda wangekubali kuzungumza na madereva, lakini hili la kuwapa adahabu abiria kwa kuwachelewesha kisha safari ikaendelea sioni kama ni sawa. Tena itapita miezi 6 au hata mwaka na mambo yatakuwa vilevile.
 
hii safi sana,huu ndio mwanzo wa kuwapo na ajira rasmi ya udereva kwenye makampuni binafsi,wamezidi kunyanyasika.pia walazimishe bei ya mafuta kushuka.

Hili la kushinikiza bei ya mafuta ishuke hawatoliweza wao peke yao. kinachotakiwa sisi sote wenye magari walau kwa hapa dar tuungane na kufanya mgomo, wa ukweli tena tukiwa na mshikamano sisi sote, tufanye mgomo wenye manufaa utakaozaa matunda.

Tatizo watu wengi japo bei imepanda, wakijiangalia wao wanauwezo wa kumudu, hivyo wakisikia kugoma wala hawajisumbui, wanaona kama haiwahusu vile, ukweli ni kuwa bei ya mafuta inaumiza sana ss 2,200, tunahitaji suluhisho la kudumu la kushusha bei hii inayoelekea kushindikana kulipika, though hadi sasa sijui ni nani atakaefanikisha hili.........
 
usimtishe bana, lazima watanzania tuzienzi lugha zetu

Nashukuru Preta,ati ulikuwa woga wangu tu. Hizi lugha tamu kuzungumza hata kuandika kuliko Kiswahili vinginevyo unakasumba ya kudharau kwenu.
Nami nitakuwa "natowezea" kidogo kidogo hayo maneno ya lugha yetu.

Ati, nilikuwa naogopa "ban"
 
Hili la kushinikiza bei ya mafuta ishuke hawatoliweza wao peke yao. kinachotakiwa sisi sote wenye magari walau kwa hapa dar tuungane na kufanya mgomo, wa ukweli tena tukiwa na mshikamano sisi sote, tufanye mgomo wenye manufaa utakaozaa matunda.

Tatizo watu wengi japo bei imepanda, wakijiangalia wao wanauwezo wa kumudu, hivyo wakisikia kugoma wala hawajisumbui, wanaona kama haiwahusu vile, ukweli ni kuwa bei ya mafuta inaumiza sana ss 2,200, tunahitaji suluhisho la kudumu la kushusha bei hii inayoelekea kushindikana kulipika, though hadi sasa sijui ni nani atakaefanikisha hili.........

Umoja ni jambo la msingi kwani niliona nikisema na sisi wenye magari DSM tugome kuweka mafuta tutakuwa mimi na wewe tu,wengine wanazo za wizi hawajali kwanza watatushangaa wadanganyika hatuna nguvu hiyo tupo kwenye matabaka.Nashangaa nchi nyingine wanashirikiana sana.
 
Yameanza kutoka saa saba kasoro, na madai yako yatajadiliwa zaidi siku ya jumanne! Sipati picha spidi yake huko njiani!
 
Yameanza kutoka saa saba kasoro, na madai yako yatajadiliwa zaidi siku ya jumanne! Sipati picha spidi yake huko njiani!

Kwa hali hiyo tumuombe mungu ili atuepushe na balaa manake watataka kufika mapema na huku wameumana yaani wanafukuzana!! Tuwaombee tu safari njema. Mimi nimeahirisha kusafiri
 
bado mambo ni magumu? ndio naingia Moro sasa! sijaona basi lolote toka Dar
 
Umoja ni jambo la msingi kwani niliona nikisema na sisi wenye magari DSM tugome kuweka mafuta tutakuwa mimi na wewe tu,wengine wanazo za wizi hawajali kwanza watatushangaa wadanganyika hatuna nguvu hiyo tupo kwenye matabaka.Nashangaa nchi nyingine wanashirikiana sana.

Unajua kinachozidi kuumiza kwenye huu upandaji wa bei ya mafuta ni kwamba, sio tu bei ya mafuta imepanda sana sana sana kiasi cha watu kuanza sushindwa kumudu na kutulazimu kupaki magari katika baadhi ya siku, na foleni ya barabara zetu dar es s salaam zinazidi kuumiza, yan unaweka mafuta ya 10,000 asubuhi kutoka mikocheni ukitokea coca-cola, unakaa kwenye foleni masaa 3 haujafika posta unapofanya kazi, yaani mafuta yenyewe yote uliyoweka yanaisha wakati haujaendesha, jioni kurudi tena foleni ndio usiseme, yan taa ya mafuta kuisha inawaka ukiwa salenda, means ununue tena mafuta ya 10,000 ili uweze kufika tena kazini posta kesho,

Jamani, kwa maisha gani hasa tuliyonayo watanzania kutumia wastani wa 10,000 ya mafuta kwa siku kwa gari la cc 1,300 kutoka mwenge hadi posta na kurudi (bila mzunguko mwingine wowote)? hapo namaanisha kwa mwezi unatumia 300,000 kwenye mafuta, bado haujala wewe kazini mchana wala kuacha bajeti ya nyubani kwako, haujamlipa dada anayesawaidia kazi nyumbani wala kununua umeme ambao kwa matumizi ya kawaida binafsi minimum kwa mwezi natumia 50,000, haya hapo hujaweka bajeti ya ada na matumizi ya shule ya watoto wanaosoma shule za ST., bado ndugu hawajaja na kukulilia shida zao,

Hapo sijagusa mfumuko wa bei wa vyakula na kila kitu kingine unachotakiwa kutumia hapa duniani. Halafu mtu anakuajiri anakuambia nitakulipa Shs. 400,000 gross pay, aaaaaaaah bora akae na hela yake me ntahangaika tu mtaani ntaipata hiyo, maana nikiifikiria naweza kulia bure,

Maisha yamepanda sana sana sana, na vyanzo vya upandaji wa gharama za maisha tunavijua, ni bei kubwa ya mafuta (inayo beba usafirishaji wa kila kitu tunachotumia) na umeme (unao beba uzalishaji wa vitu vya viwandani na),

Bad thing hela imepotea kabisaaaaaaa, yani haionekani jamani tutaishije? na huku tunaotegemea kutuokoa na janga hili wakitusahau na ku'consetrate na kujivua magamba tu?
 
Hayo mabasi ni majeneza yenye magurudumu. Mengi yake yana hali mbaya sana na hayastahili kutumika kusafirishia watu hata kidogo. Lakini kwa umaskini wa mali tulionao hiyo hali hata hatuioni. Ama tunaona ni sawa tu kuyatumia au kwa vile hatuna jinsi basi inatubidi tukubaliane tu na hali halisi.

Umaskini mbaya sana.
 
Hapo sijagusa mfumuko wa bei wa vyakula na kila kitu kingine unachotakiwa kutumia hapa duniani. Halafu mtu anakuajiri anakuambia nitakulipa Shs. 400,000 gross pay, aaaaaaaah bora akae na hela yake me ntahangaika tu mtaani ntaipata hiyo, maana nikiifikiria naweza kulia bure,

Mkuu haupo sirias kabisa, medical attendant analipwa 135,000/- pm, CO anayeanza si zaidi ya 350,000/-, mwalimu? polisi?

Naamini haupo katika level hii tuliopo sisi wengine (mimi ni mwalimu) lakini hiyo laki nne usiyoitaka sisi ndio bado tunaifanyia bargain!
 
Hayo mabasi ni majeneza yenye magurudumu. Mengi yake yana hali mbaya sana na hayastahili kutumika kusafirishia watu hata kidogo. Lakini kwa umaskini wa mali tulionao hiyo hali hata hatuioni. Ama tunaona ni sawa tu kuyatumia au kwa vile hatuna jinsi basi inatubidi tukubaliane tu na hali halisi.

Umaskini mbaya sana.

Umenikumbusha kitu. Kuna wakati walisema mabasi yenye chasis za fuso na malori mengineyo ambayo yamewekewa mabodi ya mabasi yatapigwa marufuku siku nyingi za nyuma lakini wapi. Nadhani hii itabidi tuijadili kama thread inayojitegemea ili tumkumbushe afande mpinga
 
Kwa hali hiyo tumuombe mungu ili atuepushe na balaa manake watataka kufika mapema na huku wameumana yaani wanafukuzana!! Tuwaombee tu safari njema. Mimi nimeahirisha kusafiri

sasa yule dereva wa Kilimanjaro si ndio watamkoma leo, na hii mvua huko njiani, tuwaombee wafike salama, mm nitasafiri kesho
 
Mkuu haupo sirias kabisa, medical attendant analipwa 135,000/- pm, CO anayeanza si zaidi ya 350,000/-, mwalimu? polisi?

Naamini haupo katika level hii tuliopo sisi wengine (mimi ni mwalimu) lakini hiyo laki nne usiyoitaka sisi ndio bado tunaifanyia bargain!

kweli mdau,kweli kabisaa,maana walimu tena hata sekta binafs wanatunyonyaaaa,aaaghhh
 
Back
Top Bottom