Madereva acheni kabisa hili!

Mwanamayu

JF-Expert Member
May 7, 2010
11,342
6,467
Nimekuwa naendesha gari kwa muda sasa, jambo ambalo silitaki kabisa ni kugonga binadamu na kuua kwani yule atakayekufa anaweza kuwa ni bread winner hivyo kuacha msiba mkubwa kwa dependants wake. Pili, mimi mwenyewe naweza kuishia jela na kuwaacha dependants wangu pabaya.

Ninachosema ni kwamba USI-OVERTAKE GARI LA MBELE YAKO HASA LILILOSIMAMA KWENYE ZEBRA CROSSING kwani huyo dereva atakuwa amesimama kupisha watembea kwa miguu kuvuka barabara (watu wazima, wazee, watoto, wagonjwa, wanafunzi). Kama uki-overtake, ujue unatembeza MASSACRE!! Kwa kifupi kitendo hiki ni ujinga na upumbavu!!!
 
He hongera kwa kutoa somo. Ucheki na akili za baadhi ya madereva maana siyo kuovertake kwenye zebra tu hata kwenye mlima ambapo mtu haoni mbele
 
Nimekuwa naendesha gari kwa muda sasa, jambo ambalo silitaki kabisa ni kugonga binadamu na kuua kwani yule atakayekufa anaweza kuwa ni bread winner hivyo kuacha msiba mkubwa kwa dependants wake. Pili, mimi mwenyewe naweza kuishia jela na kuwaacha dependants wangu pabaya.

Ninachosema ni kwamba USI-OVERTAKE GARI LA MBELE YAKO HASA LILILOSIMAMA KWENYE ZEBRA CROSSING kwani huyo dereva atakuwa amesimama kupisha watembea kwa miguu kuvuka barabara (watu wazima, wazee, watoto, wagonjwa, wanafunzi). Kama uki-overtake, ujue unatembeza MASSACRE!! Kwa kifupi kitendo hiki ni ujinga na upumbavu!!!
Ushauri mzuri, but how do you know kwamba pana zebra, na alama zetu za barabarani za kibongo. Unakweda kujua pana tuta au zebra baada ya hatua kama tano hivi kupafikia. wewe haijawahi kukutokea ukalivaa tuta bila kukusudia? Vivyo hivyo kugonga mtu kwenye zebra. Wewe ukiona umeendesha salama siku hiyo mshukuru sana Mungu.
 
Muombe Mungu akuepushe na ajali siyo kujisifia unachojua kukifanya.
MM nilikuwa nadrive tena very slowly kwa sababu nilikuwa naingia kwenye kibao kilichokuwa kikionesha spidi 50 ila kuna mtu alitoka porini na lori la mchanga akaja kuigonga gari ya nyuma yangu kwa ubavuni na kuuwa watu wa3. Hakuna kinga ya ajari zaidi ya kumuomba Mungu atuepushie mbali
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom