Balantanda
JF-Expert Member
- Jul 13, 2008
- 12,476
- 4,752
Binafsi navutiwa sana na huyu dada/mama kwa jinsi anavyojituma katika shughuli zake hasa katika kampuni ya BenchMark Production ambayo naweza nikasema ndiyo kampuni bora zaidi kwa uzalishaji wa 'video' za muziki na matangazo mbalimbali ya biashara kwa Bongo na uandaaji wa majukwaa ambayo hutumika kwa matukio mbalimbali kama vile mashindano ya Miss Tanzania nk..Pia dada huyu ni mbunifu wa program za Bongo Star Search na Mchezo Wimbo ambazo kwa kiasi kikubwa zimesaidia kuibua vipaji vya muziki vilivyokuwa vimejificha kwa baadhi ya vijana wa Tz..Kwa haya machache naomba kumpongeza dada yetu..Keep it up Madame