Madaktari wote waliogoma kufukuzwa kazi na utumishi!

Uongo wewe. Hawako considerate? Sasa mbona na wao serikali haiwapi consideration?
Dr.Chichi kumbe bado hujaona tofauti ya mgomo uliopita na huu wa sasa! Ule wa mwanzo hakukua na amri ya serikali, hivyo serikali ingewafukuza kazi ingebidi iwalipe, which is another burden to the gvt. Safari hii imecheza tricky ambayo wengi wenu hamjaijua, ukifukuzwa hupati chochote maana umedharau amri halali ya mahakama, chezeya dola weye!

Halafu mkuu mjifunze kusoma alama za nyakati. Safari hii hamna back-up ya wananchi, watu wengi hawako upande wenu kwa sababu mmekuwa too demanding and not considerate!
 
Hakuna cha kunywea hawa MaDr wapuuzi wacha watimuliwe na wasiruhusiwe hata kutuubu kuku ni wauaji si wazalendo tutakula miti shamba km mm nina Typhod napiga Konyagi km kifo kipoKipo tu Dr Uli hawezi niepushia umeambiwa Baba Serikali haina hela wenyewe wanatumwa kisiasa TIMUA kweli Mh Pinda na Dr Mwinyi mkishindwa ntajua Serikali yetu DHAIFU
Ukwaju nakujua vizuri ndugu yangu sasa tunakusubiri upatwe na tatizo uje kwetu !! Vipi kile kikombe cha babu kilikusaidia?
 
Wachina wanaweza kuichukua hospitali nzima na hao wafanyakazi kulipwa na serikali yao ya uchina ,kuna madaktari kama milioni moja hawana kazi nchini China.

Kwa akili yako unadhani madaktari kutoka China watakuja kufanya kazi bure hapa....:A S confused:
 
Chama nani kakuuliza lakini kama upo US halafu acha uongo unasema huko US huna maisha ya kubahatisha yaani kuokota makopo ya vinjwaji na kufanya usafi McDonald na kutandika vitanda kwenye hotel za wazungu hayo ndio unaona maisha? Ebu pitia orodha ya madai ya Madaktari ya Wizara ya Afya.

Ritz
Mbona una hamki deal zilikataa mjini leo nini? Kazi yangu iwe ni Mcdonald, kutandika vitanda vya wazungu inanipa kapato halali kinachokidhi mahitajia yangu ya kila siku ndio sababu nakwambia sibahatishi maisha, ule mwaliko wangu uko palepale ukibahatika kuja US ni PM ili tuonane, hapo Kempinsk si vitanda vinatandikwa kila siku na wageni wenyewe ndio hao wazungu unawaongelea?sasa ajabu ipo wapi? Madai ya madaktari nimeyaona ila lile lako la kudai wanataka walipwe mil. 13.5 ndio bado sijaliona

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Ritz, hivi sisi hatuwezi kuendesha mambo kwa diplomasia? Hawawezi kulipwa hivyo but we could do something...hakuna kitu kibaya kama kuahidi kushughulikia tatizo halafu kila mtu anasahau yale aliyosema baada tu ya kumaliza makubaliano yenu ya kuanza kufanyia kazi. Napenda kujua, Serikali imefanyia kazi madai ya madaktari kwa kiwango gani ili tuone basi hata kama kuna dalili za kuonyesha kweli dhamira ya kutatua hayo matatizo ipo.
Vinginevyo hapa ni kutesa wananchi tu...
Mizengwe pita pinda alishasema kwamba Intern atapata call allauns 15,000; Registrar 20,000; postmortem 100,000. Kwa tafsiri ya haraka ni kwamba serikali ya mizengwe pita pinda inathamini zaidi huduma kwa maiti na wala sio kwa wagonjwa; lakini pia kwamba huyo intern anayesota kama hana akili nzuri kutwa kuchwa hana umuhimu sana kwa sababu hata postmortem haendi na itamtosha buku 15 tu akikataa aishie. Vilevile, second on call ambaye mara moja moja anaweza kuitwa na intern akatishe usingizi wake anao umuhimu zaidi na kwa hiyo atapata buku 20. Specialist wanamwogopa kidogo, kwa kweli huyu ni nadra sana kuitwa maana mambo kumfikia kuitwa ujue ni issue, lakini kwa kuwa asije akatoroka nchini atalambishwa pipi ya buku 25 tu, maana anaweza kuja kuwa waziri siku moja na hivyo anapaswa kuangaliwa vizuri asifikirie kuleta ushindani kwenye sirikali, apewe tu 25 atanyamaza. Mpasua maiti ololooooh! Lazima apate tenga zima, maana maiti inaheshimiwa sana na mwenye nchi asije akauliza msibani (never miss) kimepatikana nini wakashindwa kujibu. Sirikali yetu ni wasanii wazuri sana. Wanajua wanachokifanya. Mizengwe pita pinda kasema liwalo na liwe, kweli la kwanza limeshakuwa. SItashangaa akifyongo tena, kwa sababu alishaahidi hagombei tena siasa 2015, hata bosi wake harudi tena ikulu, kwa hiyo hawajali kikitokea chochote sababu hawarudi tena kuomba kura uswahilini. Wanaongea lugha ya asali wanapotambua uchaguzi upo karibu. Hawapo kwa ajili ya watu ila kwa ajili yao wenyewe na matumbo yao hata kama watalazimika kuua ili kutimiza nia zao.

Nene mvifile hilo.
 
jipe moyo mkuu.. idadi ya madaktari wote TZ ni chini ya 2500...hawa ndio MD, and specialist, of which for them it requires them to spend atleast 6yrs(intern inclusive)...na hawa ndio wanahitajika huko nje, unaosema wewe ni
A.M.O, C.O.. ba kunatofauti kubwa kati yao.


Nazungumzia MDs. Kikubwa cha kuelewa ni kuwa hospitali za binafsi hapahapa Tanzania haziwezi kuajiri madaktari wote waliogoma. Ukichukulia Botswana bado wanawahitaji madaktari kutoka nje lakini siyo wengi kama watu wanavyofikiria. Botswana ina watu milioni mbili tu na imeamua kusomesha madaktari wake. Vilevile kumbuka kuwa kiwango cha elimu Tanzania kimeshuka kutokana na sababu mbalimbali na hiyo inagusa vilevile fani ya udaktari kwa hiyo uwezekano wa madaktari wetu kupata kazi nje unazidi kupungua.
 
00181924:42e2ce094ac480cbf72ba44db3f0bb70:h450.jpg
 
Ccm ndo inafanya mgomo usiishe. kwanini hela za epa wasipewe madokta wakati swala lao linaendelea kushughulikiwa badala yake zinaenda kutekeleza ilani ya ccm tena bara tu?. sina imani na viongozi wa nchi. Mia


Mm cna uhakika kama hilo ndo suluhisho kwan hao madaktari wanasemwa kutoka nje ya nchi watalipwa kiasi gani kulinganisha na cha hawa tunaowasema kugoma? Je hao kutoka nje be it from EAC/somewhere else, mazingira ya kaz yakoje?? Vifaa wanavyodai hawa ma-Dr wa kwetu wao sio lazima au watatoa/watatibu kwa msaada????
Mungu ibariki TZ pamoja na Watu/Wananchi wake!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kwa mujibu wa chanzo muhimu katika wizara ya afya, Serikali imejiandaa kuchukua hatu kali kwa madaktari wote waliogoma ifikapo kesho Ikiwa ''Ni pamoja kuwafukuza kazi na utumishi'' baada ya juhudi za Serikali na za Kimahakama ''KUTOHESHIMIWA''.

Pamoja na hatua hizo pia taratibu za kuandaa madktari mbadala toka taasisi nyingine za Serikali ikiwa ni pamoja na uwezekano wakupata msaada wa dharura wa Madaktari toka mojawapo ya Nchi za Afrika Mashariki, zinaendelea vizuri. Aidha ulinzi nao unaendelea na utaendelea kuimarishwa katika sehemu na maeneo mbalimbali.

Kauli hii bila shaka ina underline tamko la Serikali leo Bungeni kuwa '' LIWALO NA LIWE''


Ndivyo walivyo. Akili zao ndivyo zifanyavyo kazi! Nchi za wenzetu zikuze madaktari, sisi tukachukue! Kweli Dhaifu
 
Back
Top Bottom