yusufummaka
Member
- Apr 7, 2012
- 30
- 20
Tume huru ziundwe kuchunguza nani kateka na kunyasanyasa Dr. Ulimboka hilo halina ubishi. Lakini pia tume huru iundwe kuchunguza madhara yaliyosababishwa na mgomo wa madaktari tangu walipoacha kuona wagonjwa OPD na Mawodini ili tujue uhusika wa kila daktati katika madhara yaliyowapata wananchi (yaani gharama, maumivu, complications, deaths, na usumbuvu) wakati wa mgomo.
Ili kuzui migomo hii isitokee mara kwa mara ndugu na jamaa walioathirika wafungue kesi mahakamani kudai fidia toka kwa madaktari husika, serikali na mifuko ya bima za afya kwa kukosa matibabu siku za mgomo.
Uzalishaji wa madaktari nchini hivi sasa umeongezeka kila mwaka hasa baada ya kuongezeka kwa vyuo vinavyotoa taaluma hii (MUHAS, KCMC, IMTU, KIU, HKMU, BUGANDO), hii inasababisha isiwe vigumu serikali kuwafukuza madakatari 200 wanaowatelekeza wagonjwa mahospitalini, madaktari wasiomheshimu waziri wao wa afya, waziri wao mkuu na hata amri ya mahakama. madaktari wa aina hii wamepoteza sifa na heshima ya kuitwa madakatari ndani ya jamii. Hata huko nje ya nchi pia kuna matatizo, hivyo kusema mtakwenda kufanya kazi huko ni upuuzi mtupu. Mawazo finyu yatakufanya uone kuwa huko nje ya nchi wanaruhusu madaktari wanaoacha kutibu wagonjwa kwa kudai posho zaidi. Nchi ina matatizo mengi sana kila secta sio CT scan na vitanda hospitalini pekee, pia tunakumbwa na njaa kila mara, baadhi ya sehemu hazina maji, umeme, barabara, nyumba za walimu. Ona wale polisi wanaokaa katika jengo la msimbazi police lilivyo chafu, mahakama hazina vitendea kazi, magereza mahabusu wamerundikana, n.k. Mnaposema mnagoma ili kuboresha mazingira ya kutolea huduma ni utoto mtupu. Maslahi yenu hayawataji hata wenzenu mnaoshirikiana nao katika kutoa tiba kama wafamasia, wauguzi, maabara, mortuary, cleaners, mionzi, n.k, hivi hao maisha yao ni mazuri kuliko ya kwenu? Au mna agenda nyingine?
Mwezi wa nane wizara itapokea kakribani vijana 1000 wanaohitimu masomo ya udaktari kwenye vyuo vyetu nchini na kuanza mafunzo ya internship. Hivyo, zama zile zakujiona miungu watu ndani ya jamii zitakwisha. Tuungane tujenge Tanzania yenye neema kwa wafanyakazi na watu wote, sio neema kwa madaktari tu. Unapogoma wewe mfirikirie baba na mama yako, dada, babu, bibi, mpwa na shangazi wanapokwenda kwenye zahanati ya kijiji na kukuta watumishi wamegoma kudai maslahi. Mtalaanika, acheni maandamano yasio na kichwa wala miguu. Enzi zetu pia tulikuwa tunagoma lakini tulikuwa hatuachi wagonjwa, ila tulikuwa tunagoma kuelekea Ikulu tukiwatangunguliza mbele madakatari wenye busara kama prof. Shaba na wengine ili kuonana na waziri mkuu ama Rais kudai maslahi yetu.
Serikali ichukue hatua kali dhidi ya vitendo hivi
Ili kuzui migomo hii isitokee mara kwa mara ndugu na jamaa walioathirika wafungue kesi mahakamani kudai fidia toka kwa madaktari husika, serikali na mifuko ya bima za afya kwa kukosa matibabu siku za mgomo.
Uzalishaji wa madaktari nchini hivi sasa umeongezeka kila mwaka hasa baada ya kuongezeka kwa vyuo vinavyotoa taaluma hii (MUHAS, KCMC, IMTU, KIU, HKMU, BUGANDO), hii inasababisha isiwe vigumu serikali kuwafukuza madakatari 200 wanaowatelekeza wagonjwa mahospitalini, madaktari wasiomheshimu waziri wao wa afya, waziri wao mkuu na hata amri ya mahakama. madaktari wa aina hii wamepoteza sifa na heshima ya kuitwa madakatari ndani ya jamii. Hata huko nje ya nchi pia kuna matatizo, hivyo kusema mtakwenda kufanya kazi huko ni upuuzi mtupu. Mawazo finyu yatakufanya uone kuwa huko nje ya nchi wanaruhusu madaktari wanaoacha kutibu wagonjwa kwa kudai posho zaidi. Nchi ina matatizo mengi sana kila secta sio CT scan na vitanda hospitalini pekee, pia tunakumbwa na njaa kila mara, baadhi ya sehemu hazina maji, umeme, barabara, nyumba za walimu. Ona wale polisi wanaokaa katika jengo la msimbazi police lilivyo chafu, mahakama hazina vitendea kazi, magereza mahabusu wamerundikana, n.k. Mnaposema mnagoma ili kuboresha mazingira ya kutolea huduma ni utoto mtupu. Maslahi yenu hayawataji hata wenzenu mnaoshirikiana nao katika kutoa tiba kama wafamasia, wauguzi, maabara, mortuary, cleaners, mionzi, n.k, hivi hao maisha yao ni mazuri kuliko ya kwenu? Au mna agenda nyingine?
Mwezi wa nane wizara itapokea kakribani vijana 1000 wanaohitimu masomo ya udaktari kwenye vyuo vyetu nchini na kuanza mafunzo ya internship. Hivyo, zama zile zakujiona miungu watu ndani ya jamii zitakwisha. Tuungane tujenge Tanzania yenye neema kwa wafanyakazi na watu wote, sio neema kwa madaktari tu. Unapogoma wewe mfirikirie baba na mama yako, dada, babu, bibi, mpwa na shangazi wanapokwenda kwenye zahanati ya kijiji na kukuta watumishi wamegoma kudai maslahi. Mtalaanika, acheni maandamano yasio na kichwa wala miguu. Enzi zetu pia tulikuwa tunagoma lakini tulikuwa hatuachi wagonjwa, ila tulikuwa tunagoma kuelekea Ikulu tukiwatangunguliza mbele madakatari wenye busara kama prof. Shaba na wengine ili kuonana na waziri mkuu ama Rais kudai maslahi yetu.
Serikali ichukue hatua kali dhidi ya vitendo hivi