Madaktari wenzangu: Only "Mass resignation" itawaamsha watawala!

Mkuu mawazo ni mazuri sana lakini hilo haliwezekanio tz hakuna ushirikiano wa wafanyakazi na ndani ya wafanyakazi hao kuna system at work kwa hiyo mobilization ni ngumu sana bora hivyo walivyofanya ujumbe umefika japo kwa ghrama ya watz wenzao ilikuwa hakuna namna nyingine ya kufikisha ujumbe ispokuwa mgomo
Sio kweli kabisa kwa sababu nakumbuka vizuri Jumuiya ya Wafanyakazi nchini TUCTA waliomba kuhusishwa, Chadema waliomba kuhusishswa wakiwakilishwa na mjumbe wetu Mnyika wote wakapigwa chini tena wakisisitiza kwamba hili sio swala la kisiasa wala hawataki kusaidiwa. Ni lao wao na watakwenda nalo sambamba.

Kama unakumbuka toka siku ile mimi sikukubaliana na PR yao, na baadaye taasisi ya haki za Binadamu ambao walikuwa wakijihusisha kulingana na kazi zao wakaandaa maandamano lakini hakuna jumuiya yoyote iliungana nao isipokuwa baadhi watu wachache sana.. Ni muhimu sana ukumbuke tu ya kwamba UNION zinaundwa kutambua na kulinda haki za wafanyakazi hasa ktk mfumo huu wa Kibepari na kama jumuiya hizi hazipati nguvu ya wananchi wenyewe kwa kupitia jumuiya hizi hakuna litakalo fanyika...

Kifupi tazama matatizo tulokuwa nayo tumeshindwa tu ku coordinate maanake Madaktari hawaridhiki na mishahara, walimu, Polisi, watumishi wote wa serikali ngazi za chini wote hawa wanalia na joto la jiwe kwa maisha magumu. Na wote hawa ni waajiriwa wa serikali iweje useme haiwezekani wakati wote wanapanga kufanya migomo wakisikilizia mgomo wa kwanza utatoa matunda gani?

Serikali hii sii wajinga, wanajua fika wakiwakubalia Tucta, wengine watafuata ndio maana JK akaweka ngumu lakini akipanga kuongeza mishahara chini chini, halafu Madaktari nao waliposikia posho za Wabunge wakaja juu..maana haingii akilini mbunge kuvuta karibu mil 7 kwa mwenzi wakati Daktari hafiki mil1.5 kwa mwaka. The only way out ni wananchi wenyewe kuwa kitu kimoja na muhimu zaidi ni kuonyesha kwamba mnathamini UTU (Humanity) hapo lazima mtazoa walalahoi.

Jambo moja baya sana lililotokea nchini ni kuzaliwa kwa Taifa jipya lililotengana - A Devided society - Mfumol uliopo tunatengeneza kundi la MATAJIRI na jingine la MASKINI kwa kugawana umaskini ambao mwenye nguvu ndiye anayekula nyama ktk sinia hili la biriani..

Madaktari wameshindwa kuelewa hivyo kwamba tupo kt process, transition of making millionaires in a poor country tofauti kabisa na nchi tajiri ambazo kuna utajiri na The rich getting richer through their investment and the poor getting poorer for not having Capital.
Sasa in the making ya Matajiri ndani ya umaskini hapa ni uwanja wa fisi..hakuna mtu anayejali profession ya mtu wala elimu bali nguvu ya kunyakua na obvious Politician are winners maan wako jikoni wao! Huwezi kushindana nao kwa madai kama ilivyo nchi za magharibi ambao wanajali profession ili kuboresha na kuimarisha investment zao ktk dunia hii ya ushindani.

Sisi bado tupo ktk Ujamaa wa kisiasa wakati wananchi wanaibiwa na hivyo Madaktari walitakiwa kutumia elimu zao kutambua kwamba njia pekee wanayoweza kushinda mgogoro huu ni kutumia vigezo vya HUDUMA..Kuonyesha hali za Wagonjwa na Mazingira mabaya ktk kutoa huduma za Afya na hapo kupata support kubwa ya wananchi walalahoi wakati mawaziri, makatibu wakuu na Wabunge wanatumia mabillioni ya fedha kwa posho na mafuta ya magari.

Na hakuna madai yoyote yanayoweza kuwekwa dhidi ya serikali yasiwe Political.. Hakuna. Unapoilaumu serikali ktk uongozi wake hata iwe mishahara ni lazima iwe political maana serikali ndio siasa yenyewe haiendeshwi bila sera. Let them say Chadema na CUF wamehusika kuweka madai ya huduma bora lakini mnapiga pale panapoumiza zaidi. Kam serikali itashindwa kukata matumizi yake yasiyokuwa ya lazima, kujipangia mishahara mikubwa na anasa za posho za vikao visivyokuwa lazima, safari zisizokuwa lazima, chai na kadhalika tunaweza kabisa kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi..

Bila shaka wananchi watajiunga nanyi, walimu, Polisi na watumishi wote nchini watagundua kumbe tunaliwa kiasi hiki! Hapo ndipo mwanzo wa mabadiliko ya jumla na sii mabadiliko ya kundi moja moja la watu kwa sababu uwanja wa fisi hauchaguwi profession ya mtu.

Na ndio maana kuna walalahoi ambao wanaona mshahara wa daktari wa Laki 9 na posho juu za Ths 20,000 kwa kikao ni mkubwa sana maana wao wanakula wali mkavu. Na mkisema Viongozi mbona hivi maa vile wanashindwa kuwaelewa kwa sababu wao wanajua viongozi ndio wako jikoni.. utauliza kweli shibe ya mpishi? au ugonvi wetu ni sisi tulokuwa janvini tukigombania nyama walizotuletea. Waheshimiwa ni wa kuheshimiwa na jukumu lao kubwa kuliko daktari kwa sababu ndio wanaogawa chakula, kwani hujasikia CCM wakitangaza kwamba wao ndio wanapeleka maendeleo kwa wananchi sio Chadema wala CUF?.

Narudia kusisitiza siku zote tazama WATU na MAZINGIRA kisha jenga PR yenye kulingana na sura kamili inayojitokeza mbele yako..Na kikubwa zaidi never underestimate power of the people!
 
Sio kweli kabisa kwa sababu nakumbuka vizuri Jumuiya ya Wafanyakazi nchini TUCTA waliomba kuhusishwa, Chadema waliomba kuhusishswa wakiwakilishwa na mjumbe wetu Mnyika wote wakapigwa chini tena wakisisitiza kwamba hili sio swala la kisiasa wala hawataki kusaidiwa. Ni lao wao na watakwenda nalo sambamba......

Kaka umeniandikia ukurasa mzima nashukuru kwa kutumia muda wako juu ya jambo hili lakini swali langu ni moja tu kwamba kama utafahamu nini kinafanya ushirikiano usiwepo katika makundi haya yanayo lalamikia mishahara midogo lakini hayaungani kudai wanachotaka, ndiyo utajua system ni nini!!

Tofauti ya hapo sina lugha ya kukuelewesha kwa njia hii tunayotumia mfano mzuri Walimu walisema July wanagoma kimetokea nini? Kama hujui siri ya urembo sitaki niwe mwalimu wako.

Mgomo uliofanikiwa katika historia ya nchi hii ni wa madaktari na wafanyakazi wa benki NMB basi hakuna cha tucta wa cwt wote wako undercontrol by system. Chukua muda mwingi kufanya utafiti utapata jb.
 
mkuu Bulole Bukombe..it seems kugoma kwa pamoja kama agency(TUCTA) ni ngumu kwani viongozi wakirubuniwa au kutishwa hupoteza mwelekeo na hivyo bora kugoma selfwise kama vile waalimu, polisi, madaktari nk lakini kwa pamoja baada ya kuanza hawa wafuate hawa, simaanishi nchi isikalike na kutawalika bali viongozi watatambua kilio cha wananchi!
 
Ningependa kutoa pole kwa yale yaliyotokea na yanayoendeleakutokea katika nchini na nje ya nchi kuhusu sisi(madaktari).Pole kwa kumuuguzamwenzetu Ulimboka Steven(Dkt), Kushtakiwa kwa MAT, Kuhojiwa kwa Rais wetu NamalaMkopi(Dkt), Kufukuzwa kwa madaktari walio mafunzoni (Intern doctors), vitisho kwa wakuu wa idara n.k.

Mwaka huu Vyuo vikuu na shirikishi vya afya na tibavinategemea kutoa wahitimu kama ifuatavyo:

-MUHAS (150), KCMC(80), WBUCHS(50), HKMU(55), IMTU(45) naUDOM(0).
Kati ya hawa wapo wageni(foreigners) watakaorudi ktk nchizao, wapo ambao watakwenda kufanya internship katika hospitali za binafsi, nawapo wataenda kufanya kazi katika asasi zisizo za kiserikali(NGO)-kwaniinternship si lazima kufanya, ila hadi pale utakapoamua kufanya kazi katikahospitali. Kinachonishangaza serikali inasema inategemea madaktari 700 kutokavyuoni, inawatoa wapi?......

Wazo zuri, tafadhali anza na tukuunge mkono!
 
Kaka umeniandikia ukurasa mzima nashukuru kwa kutumia muda wako juu ya jambo hili lakini swali langu ni moja tu kwamba kama utafahamu nini kinafanya ushirikiano usiwepo katika makundi haya yanayo lalamikia mishahara midogo lakini hayaungani kudai wanachotaka, ndiyo utajua system ni nini!! Tofauti ya hapo sina lugha ya kukuelewesha kwa njia hii tunayotumia mfano mzuri Walimu walisema July wanagoma kimetokea nini? Kama hujui siri ya urembo sitaki niwe mwalimu wako. Mgomo uliofanikiwa katika historia ya nchi hii ni wa madaktari na wafanyakazi wa benki NMB basi hakuna cha tucta wa cwt wote wako undercontrol by system. Chukua muda mwingi kufanya utafiti utapata jb.
Tatizo wewe una underestamate nguvu ya Umma. Na pengine unashindwa kuelewa kwamba palipo na nia siku zote ipo njia...Nitakueleza tena napokataa mimi..

Wakati Tucta wanajiandaa na malalamiko ya Wafanyakazi wa serikali, MAT, sijui chama cha walimu na wengine wote walisikilizia Upepo wakati hawa wote ni watumishi wa serikali. Kama kweli kuna sababu ya watu kufikia kugoma kufanya kazi kwa sababu sawa nini wanafanya kwa ubinafsi!...

Tatizo lipo kwa waajiriwa wote wa serikali ngazi zote sasa kama system ndio una control vyombo hivi mnavitumia vya nini? Jiungeni wenyewe mfanya maandamano na poengine mgomo kwa pamoja ndivyo wenzenu hufanya..Na huu mgomo wa Madaktari huwezi kusema umeleta mafanikio yoyote kwa sababu hakuna kilichoongezeka kwa wananchi pengine wao wameongezewa mishahara japokuwa sii kwa kiwango walichotaka.

Kifupi maandalizi ya migomo yote hii ni mibovu na kama unasema System ina control vyombo hivi then kuna haja gani ya kufanya migomo wakati wawakilishi ndio hawa wanaokwenda kuongea na viongozi?. Sisi Ubinafsi wetu ndio sababu hakuna jingine kila mmoja amebeba msalaba wake. Na hili ndio CCM imefanikiwa sana kutika kuwategeni. Mkianza tu maandamano mnadaiwa kushirikiana na chama cha Upinzani, kwa hofu mnajitoa haraka kwamba hatushirikiani na mtu wala chama chochote.. Hivyo mnajiengua wenyewe na kubakia wepesi...Ndio hayo tu..
 
You dont have to mobilise peopple to table 'Mass resignation'. The message is crystal clear, 'If you feel & think that this little you get as salary isnt enough just table your letter and move foward' We all know that our claims are far beyond gvt budget, a wise thing would be 'HOW TO IMPROVE OUR ECONOMY SO THAT OUR SPENDING POWER IMPROVE'

Gvt is me, you and others, Let us work hard and put reality on table rather than looking selfish.
Teachers are now on strike demanding 150-155% increment.Arent they special tooo????????would you be there????????

TULICHAGUA CHANNEL MBAYA, we should have known this.
 
Hii imewekwa vizuri, kiakili na ukiisoma inasikitisha. Inatoa wito kwa madaktari kuangalia wanachogombania ni nini hasa na kwa manufaa ya nani. Kama madaktari hawawezi kulazimisha serikali kukaa nao chini hakuna mfanyakazi wa kada nyingine yoyote atakayeweza kufanya hivyo.

I support the doctors!
Nawaunga mkono madr wa bongo katika madai yenu yote dhidi ya serikali,ni dhahiri serikali yetu sasa inaendeshwa kibabe. Drs jiulizeni baada ya Dr. Uli kuteswa na kuumizwa kiasi kile na Dr. Mkopi kupelekwa mahakamani kwa ajili yenu na kufutwa kwa leseni za madr walioko mafunzoni ndiko kumewafanya kunyamaza kimya?

Nadhani hii si sahihi kwenu wala kwa mstakabali wa kile mlichokuwa mnakipigania. Nadhani mpango mbadala umekwisha ainishawa hapo juu, wenzenu wa Kenya walithubutu na serikali yao ikashika adabu.

Jipangeni na kuwa na dhamira moja ya kuwasilisha barua za kuacha kazi kwa notice ya 24 hrs kwa pamoja then kitaeleweka na hapo ndipo tutajua unafiki wa viongozi wa serikali yetu.
 
Tanzania bila migomo ya wafanyakazi haiwezekani!!Wafanya kazi kutumikishwa kama punda bila kujali ugumu wakazi zao, muda wa kazi n.k..viongozi walioko madarakani wanasahau nani aliyewaweka, na wanadhani watakaa madarakani milele na kwamba hawatarudi huku mitaani!!
 
Back
Top Bottom