MVUMBUZI
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 5,182
- 2,304
Baadhi ya madaktari na Manesi katika hospitali ya Mt .Meru Arusha wamethibitika kufanya kile ambacho watu wengi wamekuwa wakikilalamikia licha ya wao kuendelea kukana uovu huo. Imedhihirika kwamba baadhi ya madaktari wamekuwa wakitumia taaluma yao vibaya kwa kuharakisha vifo vya wagonjwa badala ya kuwapa huduma itakayo wawezesha kuongeza angalau siku kadhaa za kuishi na kufurahiwa na watoto, wake, waume, wazazi na hata ndugu zao.
Uchunguzi uliofanywa siku tatu mfululizo katika wodi namba 6 ya wanaume umeshuhudia madaktari vijana wakishawishiwa na manesi wazoefu wa kuua (a.k.a watoa roho za watu) ili kuwanyima baadhi ya wagonjwa drip makusudi ili zibaki za kuuza kwa kisingizio kwamba ugonjwa wake hauwezi tibika na kwamba drip haimsadii chochote. Hali hii ilijidhihirisha pale mgonjwa mmoja aliyekuwa na tatizo la kumeza chakula alipoletwa na ndugu zake ili angalau apate drip ya Glucose zimwongezee nguvu huku wakitafuta utaratibu wa kumpeleka KCMC. Siku alipoletwa ndugu hawa waliwapa Manesi Shilingi 2000 na ndugu yao akawekewa drip tatu. Siku iliyofuata manesi hawakupewa hela kwa hiyo wakamwekea drip moja tu kwa masaa 24 ilihali wakijua kabisa mgonjwa huyu alikuwa anategemea drip kama chakula.
Tatizo la mgonjwa lilikuwa ni chakula tu kwani alikuwa anaongea vizuri na kutembea mwenyewe bila shida yoyote. Nesi mmoja aliyekuwa zamu siku ya Jumanne saa sita na nusu mchana tarehe 3/5/2011 katika wodi 6 ya wanaume na Dk aitwaye Israeli Kasago wakaenda mbali na kumpa discharge kuliko wampe drip ambazo siyo mali yao bali zimegharamiwa na fedha za walipa kodi kwa ajili ya kuwasaidia watanzania.
Mgonjwa alipoomba kuwekewa drip ili ake angalau apate nguvu kidogo yule nesi akamkataza Dr. Israeli Kasago na alipoulizwa kwa nini anafanya hivyo akasema huyu mgonjwa amechanganyikiwa. Niliposikia hivyo nilitaka kumzaba kofi au ngumi ila hekima ikanizuia.
Wasifu wa huyu Nesi aliyekuwa zamu siku ya tarehe 3/5/2011 saa sita na nusu mchana hadi saa 7:20 ni Mnene mweupe aliyekuwa amevalia white . Sikufanikiwa kupata jina lake ila niliambiwa ni mmachame feki kwani wamachame ninavyowafahamu hawana roho mbaya hivyo.
Ndugu zake wakamwomba angalau mgonjwa apewe drip wakati wanajipanga kifedha kumhamishia KCMC lakini huyu Dr. Akamsikiliza zaidi huyu Nesi muuaji badala ya kutumia taaluma yake na hivyo kwa makusudi wakam-discharge mgonjwa akafie mbali. Katika siku hiyo hiyo wagonjwa wengine watatu ambao pia hali zao zilikuwa mbaya wakaandikiwa discharge waondoke wodini kwa sababu tu Manesi hawapati chochote kutoka kwao.
Katika hali kama hii sichelei kusema kwamba Wataalam hawa waliosoma kwa kodi za wagonjwa haohao na watanzania kwa ujumla balala ya kutumia taaluma yao kutetea uhai wa watanzania wamekuwa wakiharakisha mauti yao.
Hii ni dhambi na ninajua vyama vyao vitawatetea ila ukweli utabakia kuwa ukweli kwa ninayooandika hapa nimeyashuhudia mimi mwenyewe na nathubutu kuwaita hawa madaktari wauaji kwani kwa siku tatu za uchunguzi mambo waliokuwa wakiwafanyia wagonjwa yamethitisha kwamba ndiyo tabia yao..
Uchunguzi uliofanywa siku tatu mfululizo katika wodi namba 6 ya wanaume umeshuhudia madaktari vijana wakishawishiwa na manesi wazoefu wa kuua (a.k.a watoa roho za watu) ili kuwanyima baadhi ya wagonjwa drip makusudi ili zibaki za kuuza kwa kisingizio kwamba ugonjwa wake hauwezi tibika na kwamba drip haimsadii chochote. Hali hii ilijidhihirisha pale mgonjwa mmoja aliyekuwa na tatizo la kumeza chakula alipoletwa na ndugu zake ili angalau apate drip ya Glucose zimwongezee nguvu huku wakitafuta utaratibu wa kumpeleka KCMC. Siku alipoletwa ndugu hawa waliwapa Manesi Shilingi 2000 na ndugu yao akawekewa drip tatu. Siku iliyofuata manesi hawakupewa hela kwa hiyo wakamwekea drip moja tu kwa masaa 24 ilihali wakijua kabisa mgonjwa huyu alikuwa anategemea drip kama chakula.
Tatizo la mgonjwa lilikuwa ni chakula tu kwani alikuwa anaongea vizuri na kutembea mwenyewe bila shida yoyote. Nesi mmoja aliyekuwa zamu siku ya Jumanne saa sita na nusu mchana tarehe 3/5/2011 katika wodi 6 ya wanaume na Dk aitwaye Israeli Kasago wakaenda mbali na kumpa discharge kuliko wampe drip ambazo siyo mali yao bali zimegharamiwa na fedha za walipa kodi kwa ajili ya kuwasaidia watanzania.
Mgonjwa alipoomba kuwekewa drip ili ake angalau apate nguvu kidogo yule nesi akamkataza Dr. Israeli Kasago na alipoulizwa kwa nini anafanya hivyo akasema huyu mgonjwa amechanganyikiwa. Niliposikia hivyo nilitaka kumzaba kofi au ngumi ila hekima ikanizuia.
Wasifu wa huyu Nesi aliyekuwa zamu siku ya tarehe 3/5/2011 saa sita na nusu mchana hadi saa 7:20 ni Mnene mweupe aliyekuwa amevalia white . Sikufanikiwa kupata jina lake ila niliambiwa ni mmachame feki kwani wamachame ninavyowafahamu hawana roho mbaya hivyo.
Ndugu zake wakamwomba angalau mgonjwa apewe drip wakati wanajipanga kifedha kumhamishia KCMC lakini huyu Dr. Akamsikiliza zaidi huyu Nesi muuaji badala ya kutumia taaluma yake na hivyo kwa makusudi wakam-discharge mgonjwa akafie mbali. Katika siku hiyo hiyo wagonjwa wengine watatu ambao pia hali zao zilikuwa mbaya wakaandikiwa discharge waondoke wodini kwa sababu tu Manesi hawapati chochote kutoka kwao.
Katika hali kama hii sichelei kusema kwamba Wataalam hawa waliosoma kwa kodi za wagonjwa haohao na watanzania kwa ujumla balala ya kutumia taaluma yao kutetea uhai wa watanzania wamekuwa wakiharakisha mauti yao.
Hii ni dhambi na ninajua vyama vyao vitawatetea ila ukweli utabakia kuwa ukweli kwa ninayooandika hapa nimeyashuhudia mimi mwenyewe na nathubutu kuwaita hawa madaktari wauaji kwani kwa siku tatu za uchunguzi mambo waliokuwa wakiwafanyia wagonjwa yamethitisha kwamba ndiyo tabia yao..