Madaktari wapigwa stop kufanya kazi private

Mti mkavu,
Nakuunga mkono sana.. Hali ilifikia kuwa mbaya sana kwa wagonjwa nchini na hakika wanaotetea Madaktari wa serikali kufanya kazi private wanashindwa kuelewa mfumo mzima ulivyokuwa mbovu. KJama hawa madaktari wanataka kuendesha biashara zao binafsi wafanye kazi huko full time na sio kuchukua wagonjwa wa hospital za serikali, kuwaghiribu kisha kuwalipisha gharama kubwa ktk Hospital zao binafsi ati ndiko kwenye huduma nzuri..The same person atakuwaje anahudumia vizuri kwake na siko alikoajiriwa?

Hapa hawa Madaktari wanachezea maisha ya binadamu kabisa, na kulipwa mishahara midogo sio sababu ya kutoa huduma hafifu ktk hospital za serikali..,mshahara mdogo acha kazi fungua yako na ufanye kazi vizuri sio kwenda Muhimbili ili mradi upate kuiba wateja baada ya kazi. Swala la walimu na viongozi ni swala linaloweza kutazamwa pia lakini kwa uangalifu zaidi ya madaktari kwa sababu hawa madaktari wamefikia kucheza na Uhai wa watu.

Hawakatazwi na mtu yeyote kufungua biashara zao binafsi na kutotegemea mshahara wa serikali lakini unapoajiriwa na serikali kisha muda mrefu unautumia ktk hospital yako hii inapunguza huduma za hospital za serikali na matokeo yake kila hospital ina pungukiwa madaktari. Yanayotokea leo hospitali za serikali hayatokani na ukosefu wa Madakari au madawa isipokuwa ni UFISADI wa Madaktari unaoharibu kabisa huduma nzima ya Afya nchini..

Kwa uhakika huduma za Hospital za serikali zmepungua kuliko wakati wowote toka tupate Uhuru.. Wanawake wajawazito wanakugfa kuliko wakati wowote, Malaria, Kufia kikuu ni magonjwa yanayotibika lakini yanaua kuliko hata Ukimwi.

Wanataka ushindani wafungue za kwao na watafute wateja na sii kuwachukua wale wasio na jinsi na kuwahadaa kwa maradhi yasiyoponyeka isipokuwa ktk hospital zao. Halafu sii kweli daktari anaweza kukutibu vizuri ktk zahanati yake kuliko Muhimbili hali kule hana vifaa vya kutosha, huu ni wizi mtupu na maranyingi wanaiba hata madawa na vifaa toka hospital za serikali.

Ikiwa shule au mwalimu sii mzuri unaweza kuondoka sahule hiyo at least mhudumiwa ana choice lakini sii ktk Maradhi. Hao viongozi wetu kufanya biashara ni swala la muda tu...Hili linaangukia ktk miiko na maadili ya viongozi (Siasa) na kama sikosei JK tayari alikwisha piga marufuku viongozi wa serikali kujihusisha na Biashara.. Aliwaomba wachague aidha siasa au Biashara, hivyo kama unamjua Kiongozi yeyote ngazi ya juu serikalini akijihusisha na biashara nadhani bila shaka huyu kiongozi anavunja sheria..Mahakama ya miiko na maadili imeshafunguliwa hivyo ni swala la ku report tu mtuhumiwa.

Generally speaking,tulipofikia ni pabaya mno..hali ya maisha sijui au ni kuendekeza(maana sisi wengine hatujaanza kuingia rasmi kwenye misukosuko ya life)imetufanya tu develop roho ya paka kiasi cha kutothamini kabisa utu na maisha ya mtu.For me,ni bora nisichukue hiyo dhamana ya kuajiriwa na yoyote kuliko ku play around na life ya mtu,ni hatari sana.

Nakumbuka lile sekeseke la mgomo wa ma daktari pale muhi2..dah,yaani jamaa walikuwa wanaenda kukusanya maiti tu wodini.Ni mtihani kwa kweli,mamlaka zote husika zinatakiwa kuwa makini,otherwise sisi vijana tuliopo mashuleni tunaanza kupata fikra za kushika njia kuliko kwenda kuingia kwenye lawama za kuua ndugu zetu
 
Chanzo cha hii mada ni nini? Nani kasema haya? Data zipo wapi.
Watanzania wenzangu mnekuwa wa maana sana kama mngekuwa wakali hivi kwa wana siasa. Wansiasa wana-screw nchi nyie mnashikia bango daktari anayezima njaa yake. Ulishatoa mzigo bandarini ukaona shida yake?
Kila mtu anakula mahali pake pa kazi kama serikali hailipi pesa na nyie ndo mmeiweka madarakani basi ukiingia wavuni kwake anakulamba tu CCD kama kawa. Kama ukijitia macho juu unakufa and no body will give a damn. System imeoza kila mtu anaiba milionea we unataka watoto wake wasisome private kisa analipwa laki tano kama secretary wa TRA wa darasa la saba?
Raisi amesema "changanya na akili yako" nasikitika kwa wanaotangulia mbele ya hukumu lakini ukweli na uwazi ni kuwa wanasiasa wametupeleka hapo, hilo hamlioni mnamwona mwenye njaa mwenzenu.
Kama wakisema watu wafanye hosppitali za serikali tu kwa laki tano tutatibiwa na majanitor huko Muhi2 hakutakuwa na daktari.
Ukweli unauma ila ndo huoo
 
Chanzo cha hii mada ni nini? Nani kasema haya? Data zipo wapi.
Watanzania wenzangu mngekuwa wa maana sana kama mngekuwa wakali hivi kwa wana siasa. Wanasiasa wana-screw nchi nyie mnashikia bango daktari anayezima njaa yake. Ulishatoa mzigo bandarini ukaona shida yake?
Kila mtu anakula mahali pake pa kazi kama serikali hailipi pesa na nyie ndo mmeiweka madarakani basi ukiingia wavuni kwake anakulamba tu CCD kama kawa. Kama ukijitia macho juu unakufa and no body will give a damn. System imeoza kila mtu anaiba milionea we unataka watoto wake wasisome private kisa analipwa laki tano kama secretary wa TRA wa darasa la saba? Na akili anayo kichwani kwake? Does this make sense to you?
Raisi amesema "changanya na akili yako" nasikitika kwa wanaotangulia mbele ya haki lakini ukweli na uwazi ni kuwa wanasiasa wametupeleka hapo, hilo hamlioni mnamwona mwenye njaa mwenzenu.
Kama wakisema watu wafanye hosppitali za serikali tu kwa laki tano tutatibiwa na majanitor huko Muhi2 hakutakuwa na daktari.
Ukweli unauma ila ndo huoo
 
Sasa ule muda ambao anao wa ziada afanye nini? Je, wamekuwa wakitoroka muda wa kazi? Tuletewe sababu ili tujadili vizuri. Wakitoka hapo wataenda kwa waalimu wanaofundisha private tuition!! Baada ya hapo wataenda kwa wamachinga!!
 
Chanzo cha hii mada ni nini? Nani kasema haya? Data zipo wapi.
Watanzania wenzangu mnekuwa wa maana sana kama mngekuwa wakali hivi kwa wana siasa. Wansiasa wana-screw nchi nyie mnashikia bango daktari anayezima njaa yake. Ulishatoa mzigo bandarini ukaona shida yake?
Kila mtu anakula mahali pake pa kazi kama serikali hailipi pesa na nyie ndo mmeiweka madarakani basi ukiingia wavuni kwake anakulamba tu CCD kama kawa. Kama ukijitia macho juu unakufa and no body will give a damn. System imeoza kila mtu anaiba milionea we unataka watoto wake wasisome private kisa analipwa laki tano kama secretary wa TRA wa darasa la saba?
Raisi amesema "changanya na akili yako" nasikitika kwa wanaotangulia mbele ya hukumu lakini ukweli na uwazi ni kuwa wanasiasa wametupeleka hapo, hilo hamlioni mnamwona mwenye njaa mwenzenu.
Kama wakisema watu wafanye hosppitali za serikali tu kwa laki tano tutatibiwa na majanitor huko Muhi2 hakutakuwa na daktari.
Ukweli unauma ila ndo huoo

Ndugu hapa umemaliza!! Kwa nini daktari tu alaumiwe wakati kila mtu anakula pake?? Daktari aliyesoma miaka kumi unamlipa laki sijui 4 sijui 5 huku akiji-expose na magonjwa sababu ya mazingira magumu ya kazi!! Komaeni na Serikali iongeze mshahara:Tupatieni chetu kama BOT uone kazi!!
 
source in kwenye hutuba ya waziri wa afya na ustawi wa jamii kuhusu makadirio ya mapato na matumizi/ huduma za tiba imechapishwa katika mtanzania tarehe 29 june 2010.
 
Solution ni kuwapa madaktari mshahara mkubwa utakaofanya wasiwe na haja ya kwenda kufanya kazi kwenye hospitali za private kujiongezea kipato. Kama Mbunge anaweza kupata 'package' ya sh. milioni 7, Daktari anastahili zaidi ya hizo kwa sababu kazi yake ni ya kuokoa maisha ya binadamu.

Napendekeza kila daktari alipwe mshahara wa Sh. milioni 3 kwa saa 9 za kawaida za mfanyakazi yeyote yule. Zaidi ya hapo kama hawalipwi overtime walipwe Sh. 20 hadi 30 elfu kwa kila saa ya ziada anayotumia kutibu wananchi. Kama watu wanaweza kulipana posho zinazofikia kiwango cha Sh. laki tano kwa siku kwa kuhudhuria vikao kwa nini madaktari nao wasilipwe overtime ya aina hiyo.
 
Mti mkavu,
Nakuunga mkono sana.. Hali ilifikia kuwa mbaya sana kwa wagonjwa nchini na hakika wanaotetea Madaktari wa serikali kufanya kazi private wanashindwa kuelewa mfumo mzima ulivyokuwa mbovu. KJama hawa madaktari wanataka kuendesha biashara zao binafsi wafanye kazi huko full time na sio kuchukua wagonjwa wa hospital za serikali, kuwaghiribu kisha kuwalipisha gharama kubwa ktk Hospital zao binafsi ati ndiko kwenye huduma nzuri..The same person atakuwaje anahudumia vizuri kwake na siko alikoajiriwa?

Hapa hawa Madaktari wanachezea maisha ya binadamu kabisa, na kulipwa mishahara midogo sio sababu ya kutoa huduma hafifu ktk hospital za serikali..,mshahara mdogo acha kazi fungua yako na ufanye kazi vizuri sio kwenda Muhimbili ili mradi upate kuiba wateja baada ya kazi. Swala la walimu na viongozi ni swala linaloweza kutazamwa pia lakini kwa uangalifu zaidi ya madaktari kwa sababu hawa madaktari wamefikia kucheza na Uhai wa watu.

Hawakatazwi na mtu yeyote kufungua biashara zao binafsi na kutotegemea mshahara wa serikali lakini unapoajiriwa na serikali kisha muda mrefu unautumia ktk hospital yako hii inapunguza huduma za hospital za serikali na matokeo yake kila hospital ina pungukiwa madaktari. Yanayotokea leo hospitali za serikali hayatokani na ukosefu wa Madakari au madawa isipokuwa ni UFISADI wa Madaktari unaoharibu kabisa huduma nzima ya Afya nchini..

Kwa uhakika huduma za Hospital za serikali zmepungua kuliko wakati wowote toka tupate Uhuru.. Wanawake wajawazito wanakugfa kuliko wakati wowote, Malaria, Kufia kikuu ni magonjwa yanayotibika lakini yanaua kuliko hata Ukimwi.

Wanataka ushindani wafungue za kwao na watafute wateja na sii kuwachukua wale wasio na jinsi na kuwahadaa kwa maradhi yasiyoponyeka isipokuwa ktk hospital zao. Halafu sii kweli daktari anaweza kukutibu vizuri ktk zahanati yake kuliko Muhimbili hali kule hana vifaa vya kutosha, huu ni wizi mtupu na maranyingi wanaiba hata madawa na vifaa toka hospital za serikali.

Ikiwa shule au mwalimu sii mzuri unaweza kuondoka sahule hiyo at least mhudumiwa ana choice lakini sii ktk Maradhi. Hao viongozi wetu kufanya biashara ni swala la muda tu...Hili linaangukia ktk miiko na maadili ya viongozi (Siasa) na kama sikosei JK tayari alikwisha piga marufuku viongozi wa serikali kujihusisha na Biashara.. Aliwaomba wachague aidha siasa au Biashara, hivyo kama unamjua Kiongozi yeyote ngazi ya juu serikalini akijihusisha na biashara nadhani bila shaka huyu kiongozi anavunja sheria..Mahakama ya miiko na maadili imeshafunguliwa hivyo ni swala la ku report tu mtuhumiwa.

safi sana mkuu,nimependa analysis yako.
haya wanayofanya hawa ma-Dr hayana tofauti na ufisadi....mbaya zaidi UFISADI wao unacheza direct na maisha ya binadamu......
ma-Dr wengi hawana utu wala ethics za kazi wanaweka hio mnayoita CCD mbele............
 
Rayase nashukuru sana kwa link.
Kwa maneno yake mwenyewe waziri nacopy na kupaste:

Utaratibu wa watumishi wa vituo vya afya vya umma kufanya
kazi katika Vituo binafsi

79. Mheshimiwa Spika, Wizara itaimarisha huduma binafsi
katika hospitali za umma hasa Hospitali za Kanda kama
zinavyotolewa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na Taasisi
32
ya Mifupa Muhimbili. Wizara itahakikisha kwamba madaktari
na wafanyakazi wengine katika vituo vya kutolea huduma za
afya vya umma hawataruhusiwa kufanya kazi katika vituo
vya kutolea huduma za afya za binafsi bila utaratibu. Pale
ambapo mtaalamu atahitajika kwenda kutoa huduma ili
kuokoa maisha ya mgonjwa kutoka pande zote mbili za umma
na binafsi, itafanyika hivyo kwa makubaliano maalumu kati ya
taasisi husika. Hata hivyo, wataalamu hawa watapewa fursa
ya kuamua kubakia serikalini au kwenda kufanya kazi katika
vituo binafsi vya kutolea huduma za afya. Utaratibu huu pia
utawahusu wafanyakazi katika vituo vya afya na vyuo vya
ustawi wa jamii.
Jamani sokomoko litaibuka. Hjatoa maelezo kwa nini wanaleta hii sera mpya na kwama wizara nyingine zinaitumia pia. Ila kwa ustaarabu uliopo hii ni noma kubwa.
 
hii mada imenigusa sana....thanx alot MCHAPAKAZI kwa ujumbe murua kabisa, tatizo watu wanataka kutibu tatizo na kuacha chanzo cha tatizo. mtu unasoma miaka 6 ( Mitano Shule +mmoja Intern) then unakuja pewa mshahara mdogo katika mazingira magumu ya kazi then ufungwe kujitafutia kwingine nani anaweza fanya biashara kichaa hiyo. nenda katika website ya bunge na soma profile za wabunge uone wana Kofia ngapi kila mmoja, ( ni wajumbe wa bodi mbalimbali) wanamiliki mpk migodi hao hawasemwi ila anaangaliwa daktari ndo wakusemwa....kweli mwizi ni wa KUKU wa Kuiba MABILIONI sio mwizi.
 
Wakuu zangu,
sisi sote tunakubaliana na kwamba matatizo yote haya yametokana na Utawala mbaya. Isingefikia hapa hata kidogo kwani hakuna wakati madaktari walikuwa wakichukua mshahara mdogo kama wakati wa Nyerere na waliifanya kazi yao kwa ufanisi zaidi ya leo hii.

Kwa hiyo maadam mishahara ndio midogo, swala liwe kuongeza mishahara ya hawa Madaktari wetu na sio wao kujiingiza ktk biashara binafsi wakishindana na mwajiri wao pembeni. Hata huku kuliko kubuhu Ubepari, ukiwa unafanya kazi Hospital yoyote iwe ya serikali au Binafsi na ukaanzisha huduma hii kwa kuiba wagonjwa toka sehemu ya kazi na kuifanya pembeni utafukuzwa kazi na pengine kunyang'anywa hata liseni kwa madai yatakavyo kuandama..

Kwa hiyo tuwaunge mkono Madaktari wapate ongezeko la mishahara. Tupinge uongozi uliopo kwa hatua za matumizi mabaya ya fedha za serikali na mengineyo yoote lakini tusije halalisha Ufisadi kwa wote kuwa ndio solution pekee maadam viongozi wetu ni MAFISADI.
 
Chanzo cha hii mada ni nini? Nani kasema haya? Data zipo wapi.
Watanzania wenzangu mngekuwa wa maana sana kama mngekuwa wakali hivi kwa wana siasa. Wanasiasa wana-screw nchi nyie mnashikia bango daktari anayezima njaa yake. Ulishatoa mzigo bandarini ukaona shida yake?
Kila mtu anakula mahali pake pa kazi kama serikali hailipi pesa na nyie ndo mmeiweka madarakani basi ukiingia wavuni kwake anakulamba tu CCD kama kawa. Kama ukijitia macho juu unakufa and no body will give a damn. System imeoza kila mtu anaiba milionea we unataka watoto wake wasisome private kisa analipwa laki tano kama secretary wa TRA wa darasa la saba? Na akili anayo kichwani kwake? Does this make sense to you?
Raisi amesema "changanya na akili yako" nasikitika kwa wanaotangulia mbele ya haki lakini ukweli na uwazi ni kuwa wanasiasa wametupeleka hapo, hilo hamlioni mnamwona mwenye njaa mwenzenu.
Kama wakisema watu wafanye hosppitali za serikali tu kwa laki tano tutatibiwa na majanitor huko Muhi2 hakutakuwa na daktari.
Ukweli unauma ila ndo huoo

Mkuu Mchapakazi,

Tuko pamoja hapa. Kama hao TRA wanaolipwa vizuri zaidi ya madaktari ndio wako msitari wa mbele kudai na kupokea rushwa kwa kutumia loophole ya importers ignorance ya taratibu za kulipa ushuru wa forodha huku wakishirikiana na Clearing agent wenye njaa, tunatarajia hao madakatari ambao wametumia muda mwingi shule kupata huo ujuzi zaidi ya hao wa TRA, kwanini wasifanye wanavyofanya? Hapa nia yangu si kuunga mkono vitendo vya madakatari kutokutimiza wajibu wao, bali tukubali kwamba ni njaa inayowapelekea kufanya hivyo. Hapa tunajadili bila kuona huo waraka wa serikali lakini nitafurahi ikiwa ni kweli kwamba kuna huo waraka unakuja na wakati huo huo waraka huo utangaze kwamba kima chini cha Daktari ni Tshs. 2,500,000 kwa mwezi. Then kama kuna Daktari ataendelea kufanya ujinga wa kutotimiza wajibu na kuwalazimisha wagonjwa kwenda kuwaona huko vichochoroni, huyo daktari itabidi achukuliwe hatua za kinidhamu.

Ni mawazo yangu tu!!!

Tiba
 
Solution ni kusepa Bongo
Hakuna asiyejua thamani ya muda tunaotumia kusoma hii profession,ugumu na risk zake.Tutaenda Burundi,Zambia,Botswana(kwani bado tunapenda kuishi Africa ati) ambako wapata gari ya kutembelea,nyumba,mshahara 2000+ us$(kwa bachelor) at least unafanya kazi bila stress za kuzidi.
 

Utaratibu wa watumishi wa vituo vya afya vya umma kufanya
kazi katika Vituo binafsi


79.
Mheshimiwa Spika,

Wizara itaimarisha huduma binafsi katika hospitali za umma hasa Hospitali za Kanda kamazinavyotolewa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na Taasisi 32 ya Mifupa Muhimbili. Wizara itahakikisha kwamba madaktari na wafanyakazi wengine katika vituo vya kutolea huduma za afya vya umma hawataruhusiwa kufanya kazi katika vituo vya kutolea huduma za afya za binafsi bila utaratibu. Pale ambapo mtaalamu atahitajika kwenda kutoa huduma ili kuokoa maisha ya mgonjwa kutoka pande zote mbili za umma na binafsi, itafanyika hivyo kwa makubaliano maalumu kati ya taasisi husika. Hata hivyo, wataalamu hawa watapewa fursa ya kuamua kubakia serikalini au kwenda kufanya kazi katika vituo binafsi vya kutolea huduma za afya. Utaratibu huu pia utawahusu wafanyakazi katika vituo vya afya na vyuo vya ustawi wa jamii.

Nafikiri haya ni maneno ya kuombea kura 2010, wanajua kuwa hawawezi kuwazuia kwani hawawalipi mshahara kwa kuishi mwezi mmzima. Serikali imgekuwa imefanya jambo la maana sana kama wangesema wanawazuia wafanyabiashara kujihusisha na kugombea nafasi za uongozi wa nchi kwani wao ndiyo chanzo cha ufisadi
 
au Swala hili limegawanyika ktk sehemu kuu mbili (1)ni uwajibikaji mbovu wa viongozi wetu ktk ugawaji wa keki ya taifa na hasa mishahara kwa watumishi karibu wote wa serikali huku wao kuona ndiyo wastahili pekee wa marupurupu na mishahara ya juu hata pale ambapo mishahara haiyendani na vigezo vya kupewa mishahara mikubwa au marupurupu.
(2)Upande wa pili ni wa ndugu zangu Madaktari hivi unapokula kiapo baada ya uhitimu inamaanisha nini?Dhamana kubwa madaktari waliyojaliwa na muumba na kuidhibitisha kwa viapo vyao baada ya uhitimu inatakiwa iambatane na matendo yao kwa wagonjwa wanaowahudumia.CCD bila ya kujali maisha ya mgonjwa udhalimu uliopindukia na hili si swala la kulifumbia macho hata bila ya kujali sababu ya aina yeyote iliyopelekea Daktari kuomba CCD.
Nianze kwa kuelezea sababu ya upande wa awali niliyoianisha hapo juu Nchi yetu kwasasa ni moja ya nchi masikini sana kutokana na takwimu zilizopo sasa ktk medani ya ulimwengu huu pamoja na kujaliwa rasilimali nyingi za dhamani.Viongozi wameshindwa kuweka dira mkakati ya kuitoa nchi hapo ilipo na kuipeleka kwenye Nchi ya ndoto yaani TANZANIA TUNAYOITAKA KUIONA NA KUITWA NCHI ILIYOENDELEA NA SI NCHI MASIKINI BALI Viongozi wanamkakati wa familia ndoto ninayoitaka kuiona yaani kuzitoa familia zao hapo zilipo na kuzipeleka ktk Familia zenye maendeleo hata kama maendeleo hayo yanatokana na ubathirifu wa rasimali za taifa unaosababishwa na sera potofu na maamuzi yasiyozingatia tija kwa watu waliowapa dhamana ya uongozi wa Taifa letu.Madhalani Dhana ya uwekezaji ilivyopotoshwa na kuingiza nchi ktk hasara kubwa mfano unamleta mwekezaji achimbe dhahabu,almasi,Tanzanite n.k Lkn mwekezaji huyu halipi kodi,hatoi ajira kwa watanzania na hanunui hata bidhaa zinazozalishwa na Tanzania pamoja na kutofanya hayo yote yenye Faida kwa mtanzania lkn anaondoka na rasimali mwisho mwa yote ukiuliza unaambiwa tunawasemehe kodi kwakuwa ni wawekezaji ili kuweka vivutio waje sasa wakiwa hapa jee sisi kama watanzania tunafaidikaje na uwepo wao au na rasilimali zetu ni HAKUNA na ni ZERO.
TUMEUZA MASHIRIKA MBALI MBALI KWA BEI YA KUTUPA BILA ya kuweka mikataba yenye tija ikiwemo ubia mabao tungefaidika nao hapa ni ZERO!
Kuendelea kulipa makampuni ambayo hayatoi huduma vizuri pamoja na ama kushindwa kutoa huduma au kupewa dhamana ya uwekezaji kwa kutumia fedha za nchi na bado tunawaita wawekezaji kwa kupitia mikataba yetu mibovu mfano shirika la reli,simu,n.k
mikataba mibovu na ufisadi mfano Richmond n.k ni weza kurudia we lkn mwisho ni hasara.Kuongeza idadi ya majimbo,mishahara inayozidi uwezo kwa wanasiasa na wabunge.Haya yote yangeweza kuipukika na kuelekeza rasimali zetu na kipato chetu kwenye kubweresha maisha ya wananchi wote.
Kwa Upande wa pili wa Daktari ninapenda kusema CCD ilikuwepo tangu nchi hii inaasisiwa na mishahara midogo ilikuwepo ktk hii fani pia kwa muda mrefu tofauti ya sasa na hapo awali ni kwamba Madaktari walitekeleza kazi zao kwa uadilifu na upendo wa hali ya juu kwa wagonjwa na wagonjwa waliliona hili na walikuwa wanasafiri hata na kuku na mavuno kuleta kwa madaktari hata bila ya kuombwa lkn hivi leo hili ni yamkiniki mtu hamjali mgonjwa kisa mshahara mdogo na mgonjwa atamwacha ateseke ili awakabe ndugu hata kama hawana wampe kidogo kitu wakati huo muda unaenda na wagonjwa wengi wanapoteza maisha ambayo kama wangeonwa ktk muda muafaka wangeweza kupata ufumbuzi wa matatizo yao.
Kuhusu mfumo wa mahospitali binafsi kwa wafanyakazi wa serikali(MADAKTARI) KWA WALIOWENGI umejengeka chini ya nadharia ya kwamba wanakuajiri ili uhamishe wagonjwa hospitali za serikali ulete kwao na hili linafanyika kwa njia nyingi mojawapo kumueleza mgonjwa nione hospitali fulani hapa sina nafasi au kumzungusha mgojwa kwa kujifanya wape busy au hawaonekani kwenye vituo vya kazi,au wanalipua kukimbilia kwenye hivyo viosiki hili kwangu mimi naona ni dhambi kubwa na si swala la kufumbiwa macho hata kidogo. Kama serikali inataka kumpa changu Daktari kuchagua serikalini au hospitali nafikiri hilo ni swala muhimu ili kuondoa mgongano wa kimasilahi na pili una uchaguzi kama unaona serikali hailipi basi nenda huko wanapolipa vizuri.Na kama unakubali kubaki serikali fanya kazi kwa uwezo wako wote na mbane muajiri abwereshe maslahi yako na si mgonjwa ambaye anahitaji huduma ktk hali tete ya kuokoa maisha yake.
 
Hao au huyo aliyetoa huo waraka/maagizo; analake jambo, angejiuliza kwanza kwa nini Doctors wanakwenda kwenye private Hospitals, akishagunduwa sababu atafute suruhu ambayo ni positive kwa Doctors na professional nyingine, watu wajifunze kufikiria si kuamka na kutoa mawazo ambayo mwisho wa siku yanaonekana ni kichekesho, maana kwa mtu anayefikiria huwezi kukurupuka kuongea utumbo huo, kwani wanaofanya kazi serikalini na kujitafutia vipato vya ziada kwenye private sectors ni Madaktari tu? au hii nchi inawasomi madaktari tu? aache zake huyo anazeeka vibaya maana ameanza kuzeeka akili badala ya viuongo vya mwili.
 
Hapo Tz ni taaluma ipi inayoweza kujivuna kwamba wanafanyakazi kama inavyotakiwa. Tangu Rais hadi muhudumu. Woote ni usanii tu!
 
Hao au huyo aliyetoa huo waraka/maagizo; analake jambo, angejiuliza kwanza kwa nini Doctors wanakwenda kwenye private Hospitals, akishagunduwa sababu atafute suruhu ambayo ni positive kwa Doctors na professional nyingine, watu wajifunze kufikiria si kuamka na kutoa mawazo ambayo mwisho wa siku yanaonekana ni kichekesho, maana kwa mtu anayefikiria huwezi kukurupuka kuongea utumbo huo, kwani wanaofanya kazi serikalini na kujitafutia vipato vya ziada kwenye private sectors ni Madaktari tu? au hii nchi inawasomi madaktari tu? aache zake huyo anazeeka vibaya maana ameanza kuzeeka akili badala ya viuongo vya mwili.
Aliyetoa waraka huu ni daktari pia by profession ila yeye anakitu cha kuzidi kidogo. Ni mwana siasa pia.
 
Mti mkavu,
Nakuunga mkono sana.. Hali ilifikia kuwa mbaya sana kwa wagonjwa nchini na hakika wanaotetea Madaktari wa serikali kufanya kazi private wanashindwa kuelewa mfumo mzima ulivyokuwa mbovu. KJama hawa madaktari wanataka kuendesha biashara zao binafsi wafanye kazi huko full time na sio kuchukua wagonjwa wa hospital za serikali, kuwaghiribu kisha kuwalipisha gharama kubwa ktk Hospital zao binafsi ati ndiko kwenye huduma nzuri..The same person atakuwaje anahudumia vizuri kwake na siko alikoajiriwa?

Hapa hawa Madaktari wanachezea maisha ya binadamu kabisa, na kulipwa mishahara midogo sio sababu ya kutoa huduma hafifu ktk hospital za serikali..,mshahara mdogo acha kazi fungua yako na ufanye kazi vizuri sio kwenda Muhimbili ili mradi upate kuiba wateja baada ya kazi. Swala la walimu na viongozi ni swala linaloweza kutazamwa pia lakini kwa uangalifu zaidi ya madaktari kwa sababu hawa madaktari wamefikia kucheza na Uhai wa watu.

Hawakatazwi na mtu yeyote kufungua biashara zao binafsi na kutotegemea mshahara wa serikali lakini unapoajiriwa na serikali kisha muda mrefu unautumia ktk hospital yako hii inapunguza huduma za hospital za serikali na matokeo yake kila hospital ina pungukiwa madaktari. Yanayotokea leo hospitali za serikali hayatokani na ukosefu wa Madakari au madawa isipokuwa ni UFISADI wa Madaktari unaoharibu kabisa huduma nzima ya Afya nchini..

Kwa uhakika huduma za Hospital za serikali zmepungua kuliko wakati wowote toka tupate Uhuru.. Wanawake wajawazito wanakugfa kuliko wakati wowote, Malaria, Kufia kikuu ni magonjwa yanayotibika lakini yanaua kuliko hata Ukimwi.

Wanataka ushindani wafungue za kwao na watafute wateja na sii kuwachukua wale wasio na jinsi na kuwahadaa kwa maradhi yasiyoponyeka isipokuwa ktk hospital zao. Halafu sii kweli daktari anaweza kukutibu vizuri ktk zahanati yake kuliko Muhimbili hali kule hana vifaa vya kutosha, huu ni wizi mtupu na maranyingi wanaiba hata madawa na vifaa toka hospital za serikali.

Ikiwa shule au mwalimu sii mzuri unaweza kuondoka sahule hiyo at least mhudumiwa ana choice lakini sii ktk Maradhi. Hao viongozi wetu kufanya biashara ni swala la muda tu...Hili linaangukia ktk miiko na maadili ya viongozi (Siasa) na kama sikosei JK tayari alikwisha piga marufuku viongozi wa serikali kujihusisha na Biashara.. Aliwaomba wachague aidha siasa au Biashara, hivyo kama unamjua Kiongozi yeyote ngazi ya juu serikalini akijihusisha na biashara nadhani bila shaka huyu kiongozi anavunja sheria..Mahakama ya miiko na maadili imeshafunguliwa hivyo ni swala la ku report tu mtuhumiwa.

TATIZO LENU WABONGO MMEZOWEA BURE MNO KILA SIKU MAMA MJA MZITO MAMA MJA MZITO,..HUduma za afya SERIKALINI ZITAENDELEA kuwa mbovu KAMA ZITAENDELEA kutolewa bure ,..ONA SASA MNALETEWA AMBULANCE ZA PIKIPIKI na hamna anaye lalamika unajua ni kwanini?mmzoea bure ,.Kama mngekuwa mnalipia mgeweza kupiga kelele ,.lakini hamuwezi sababu mnapenda bure na wimbo wenu wa mama mja mzito..,mtaendelea kulala chini,.na kujifungulia kwenye bajaji,..eti huduma bure kwa mama na mtoto,.wazazi mnakuwa wazembe hata kujiwekea akiba ya kujifungua .,?
.ndio maana.,.vipimo vyenyewe hamna kazi kuvimaintain mara vikiharibika hamna hela ya matengenezo inatoka baada ya mwezi,.ukiambiwa kapime sehemu fulani sababu hapa kimeharibika ndio mnaaza kutafutana na kuitishiana michango huku mkiwalaumu madaktari,...kumbe uzembe ni wenu na yenu SERIKALI iliowazoesha bakuli la misaada ya wafadhili,,..huduma bora lipia isipotoka idai,...kilicho bora kinalipiwa,..
BURE MBAYA SANA
 
Back
Top Bottom