Madaktari waanza kuikimbia nchi..

Watanzania tuache ushabiki wa kinafiki kana kwamba hatujazaliwa hapa nchini kwa kutetea vitu ambavyo dhairi kila ambae alishawahi kufika hospital za serikali ni shahidi. Hali za hospitali zetu zinatisha, wagonjwa wanalala chini, wakinamama wanajifungua katika hali hatarishi na wengi wao wanapoteza maisha kwa kuvuja damu nyingi baada ya kujifungua kwa kuwa imekosekana sindano ya kuzuia damu, wenzetu wanakufa mapokezi kwa kukosa huduma staili.
Madaktari wanadai vitu vya msingi kabisa ila sie ambao hayajatukuta na wala hatujui kinachoendelea katika vituo vya afya tumekalili madai ya madaktari ni posho na mishahara.
Hizo 200 bilioni za kuwaleta madaktari kutoka nje zimetoka wapi kama serikali imekiri kupitia kwa rais wetu kwamba haina pesa ya kushughulikia matatizo ya madaktari? Hawa wanaojiita madaktari by experience wanaokuja hawajui kiswahili na isitoshe kuna wengi wao pia hawajui hata kiingereza. Unategemea nini hapo? Na hata kama wakija na vitendea kazi visipoletwa hakuna kitakachofanyika zaidi ya kubebeshwa lawama etc.
Tuache ushabiki wa siasa bali tuchambue uhalisia wa tatizo lenyewe kwa kutazama ukweli halisi.
 
Hata wakiondoka wote serikali haitatishika kwa vile wakubwa wake wanatibiwa nje. Kwa ufupi ni kwamba hawa madaktari wanaoteshwa hata kutishiwa kuuawa hawana maana yote kwa watawala ambao wanaweza kwenda nje wao watoto wao hawara hata marafiki zao kupimwa mafua Ulaya na kwingineko. Who cares when a vet refuses to treat cats or other pets in countries where pets have no rights? Hatari ya kuhama kwa madaktari wataiona wananchi ambao nao wamekuwa kama mazezeta. Walipaswa kuwauliza swali moja watawala:Nyinyi na watu hata wanyama wenu mnatibiwa nje, je sisi tutabitiwa wapi ili tuendelee kuwazalishia kodi za kutibiwa nje? Naomba kuwakilisha.
 
Mwaka huu pekee Tanzania imeshapoteza zaidi ya madaktari 150, na hapo bado mwaka haujaisha. Wako watu wanaweza kufikiri kuwa hili ni jambo la kawaida, lakini just imagine kama mkoa mmoja ungepata madaktari 150 na vifaa tiba sahihi huduma ingekuwaje? Yaani Tanzania inasomesha, wengine wanafaidi kwa sababu tu serikali imemua kuonesha ubabe!

Sikubaliani kabisa na hoja kwamba madaktari wanatumiwa na wanasiasa. Kama vifaa (tena basic) vingekuwa vinapatikana kwenye hospitali zetu, lakini madaktari wakaendelea na migomo basi hapo ningekubali ni siasa. Lakini miaka nenda miaka rudi, mazingira ya utoaji matibabu imekuwa inashuka. Na sasa tunaambiwa mwaka huu pekee serikali imetenga Tsh 8 billion kwa ajili ya matibabu ya viongozi wa juu ambao hawazidi 10, huku hospitali za Taifa zikiwa zimetengea Tshs 5 tu! Yaani watu 10 wana bajeti kuzidi kiwango kilichowekwa kutibu watu milioni 10!

Naomba ufafanuzi wa jambo hilo la wakuu kutengewa kiasi kikubwa cha pesa za matibabu cha bajeti kuliko wananchi walio milioni 40. Kama ni kweli tunahitaji vithibitisho kwa kuanzisha mada inayojitegemea ili tuijadili kwa mapana na marefu. Thanks
 
JAMANI WAAACHENI WAENDEEEE, HUENDA HII DHAHAMA YA KUTISHANA YA KITOTO KABISA ITAISHA
Mimi nakubali kabisa hawa madaktari walikuwa hawanisaidii ntabaki natibiwa hata na Manesi au MaMedical ambao walipita huko JKT wanaujua Uzalendo, hao wanaojidanganya eti ataenda Botswana wakati Leseni yake imefutwa ni uongo Mtupu hawatapokelewa,
  • Kwanza ni lazima Ubalozi wetu uwachuje,
  • Pili Nchi za wenzetu huwezi kumgusa Raia wao na kumuandikia sindano wakati huna Leseni toka nchi uliosomea au cheti cha Chuo husika
  • Hao Madaktari tuwaombee safari njema kuna kazi nyingi tu huko hata km si za Udaktari wakafanye
  • Ni kweli walikuwa sio wazalendo maana walitaka kujipima na wabunge, hivi na Wahasibu Mainjinia wanajeshi, Polisi wanasheria nao wafanye hivyo?
  • Acheni waende wametumwa hao tutawasiliana nao humuhumu JF wakitutukana lakini msg send na picha imefika THE END tusubiri mgomo wa wengine, Wakulima



Yaonyesha wewe ni mbumbumbu kwelikweli katika yanayoendelea, au umechagua umeamua kutumika;
Si mara ya kwanza kwa madaktari kuondoka nchini, tena wale ambao tu ndio wamemaliza shule hata internship hawajafanya, nafahamu fika kwa kuwa nina jamaa zangu tuliosoma nao sekondari walitimkia kusini

  • Kamwe ubalozi wetu huko hauhusiki kuwachunguza
  • wanachohitaji ni vyeti vyao vya shule na ubongo wao kufanya mitihani ya usajili (katika baadhi ya nchi kama Botswana, Afrika Kusini, USA). Kama hajafanya internship anafanya huko na anasajiliwa, kama alishafanya, anafanya mtihani na kusajiliwa
  • Ni kweli kuna kazi nyingi huko sio zile za kutibu moja kwa moja, kama tu ilivyo hapa. We jiulize kuna chuo kama Muhimbili kila mwaka kinatema si chini ya 80 plus vyuo vingine wote hao wanakwenda wapi mbona mahospitalini mikoani hatuwaoni? Wapo kwenye taasisi na miradi mingine inayohusiana na afya ambayo wala hawahitaji kuwa na usajili (kufanya Internship) ili kufanya kazi hizo! Hata wizarani wapo (Mwinyi akiwa kinara wao hakumaliza internship yake muhi2)
  • Daktari anaweza kuwa mbunge lakini kamwe mbunge yeyote tu hawezi kuwa daktari, injini etc, kokote duniani kazi za kitaaluma kama madaktari wanalipwa zaidi kuliko wanasiasa kama wabunge na beurocrats (refer UK, Germany etc). Ndio maana wameweza ku-retain skilled labour force yao, nyinyi maskini halafu mnaipoteza na kuona sawa.... Kwa upumbavu wenu wa siasa za maji machafu
  • Kwa yeyote kuendelea kufikiri kuwa eti madai ya madaktari ni kwamba wametumwa na watu fulani, either mwenye kufikiri hivyo ni punguani asiyeweza kufikiri (na hivyo kufikiri wote wako kama yeye) au umetumwa kulamba uozo wa uchemfu wa mabwana zako wa serikali!
 
Hata wakiondoka wote serikali haitatishika kwa vile wakubwa wake wanatibiwa nje. Kwa ufupi ni kwamba hawa madaktari wanaoteshwa hata kutishiwa kuuawa hawana maana yote kwa watawala ambao wanaweza kwenda nje wao watoto wao hawara hata marafiki zao kupimwa mafua Ulaya na kwingineko. Who cares when a vet refuses to treat cats or other pets in countries where pets have no rights? Hatari ya kuhama kwa madaktari wataiona wananchi ambao nao wamekuwa kama mazezeta. Walipaswa kuwauliza swali moja watawala:Nyinyi na watu hata wanyama wenu mnatibiwa nje, je sisi tutabitiwa wapi ili tuendelee kuwazalishia kodi za kutibiwa nje? Naomba kuwakilisha.

Mkuu Mpayukaji, umeshapayuka tayari kusema mitanzania ni mizezeta, uzezeta wetu ndiyo turufu wanayoitumia ccm kuchezea haki zetu. mfano mzuri humu jf. wanazi wa ccm watakuwa tayari kushabikia jambo lolote hata kama serikali yao itapitisha kwamba wanaume wote wa tz tuwetunalawitiwa, manazi wa ccm wao wataunga mkono.
 
JAMANI WAAACHENI WAENDEEEE, HUENDA HII DHAHAMA YA KUTISHANA YA KITOTO KABISA ITAISHA
Mimi nakubali kabisa hawa madaktari walikuwa hawanisaidii ntabaki natibiwa hata na Manesi au MaMedical ambao walipita huko JKT wanaujua Uzalendo, hao wanaojidanganya eti ataenda Botswana wakati Leseni yake imefutwa ni uongo Mtupu hawatapokelewa,
  • Kwanza ni lazima Ubalozi wetu uwachuje,
  • Pili Nchi za wenzetu huwezi kumgusa Raia wao na kumuandikia sindano wakati huna Leseni toka nchi uliosomea au cheti cha Chuo husika
  • Hao Madaktari tuwaombee safari njema kuna kazi nyingi tu huko hata km si za Udaktari wakafanye
  • Ni kweli walikuwa sio wazalendo maana walitaka kujipima na wabunge, hivi na Wahasibu Mainjinia wanajeshi, Polisi wanasheria nao wafanye hivyo?
  • Acheni waende wametumwa hao tutawasiliana nao humuhumu JF wakitutukana lakini msg send na picha imefika THE END tusubiri mgomo wa wengine, Wakulima

kwa taarifa yako tu madaktari vyeti wanavyo kutoka chuo alichosoma, pili zipo nchi kwa kutumia loop hole ya Tz kufukuza madaktari zimetoa offer kuwasimamia wale ambao hawajamalizia intern upo then inawaabsorb. Wezako wanafikiria kutumia akili wewe unafikri kutumia mata.ko hamuwezi kulingana hata kidogo. Hii nchi ni ya vilaza kuanzia rais mapaka raia wake ambao hata wakanyanyaswa namna gani hawaoni hayo.
 
Yaonyesha wewe ni mbumbumbu kwelikweli katika yanayoendelea, au umechagua umeamua kutumika;
Si mara ya kwanza kwa madaktari kuondoka nchini, tena wale ambao tu ndio wamemaliza shule hata internship hawajafanya, nafahamu fika kwa kuwa nina jamaa zangu tuliosoma nao sekondari walitimkia kusini

  • Kamwe ubalozi wetu huko hauhusiki kuwachunguza
  • wanachohitaji ni vyeti vyao vya shule na ubongo wao kufanya mitihani ya usajili (katika baadhi ya nchi kama Botswana, Afrika Kusini, USA). Kama hajafanya internship anafanya huko na anasajiliwa, kama alishafanya, anafanya mtihani na kusajiliwa
  • Ni kweli kuna kazi nyingi huko sio zile za kutibu moja kwa moja, kama tu ilivyo hapa. We jiulize kuna chuo kama Muhimbili kila mwaka kinatema si chini ya 80 plus vyuo vingine wote hao wanakwenda wapi mbona mahospitalini mikoani hatuwaoni? Wapo kwenye taasisi na miradi mingine inayohusiana na afya ambayo wala hawahitaji kuwa na usajili (kufanya Internship) ili kufanya kazi hizo! Hata wizarani wapo (Mwinyi akiwa kinara wao hakumaliza internship yake muhi2)
  • Daktari anaweza kuwa mbunge lakini kamwe mbunge yeyote tu hawezi kuwa daktari, injini etc, kokote duniani kazi za kitaaluma kama madaktari wanalipwa zaidi kuliko wanasiasa kama wabunge na beurocrats (refer UK, Germany etc). Ndio maana wameweza ku-retain skilled labour force yao, nyinyi maskini halafu mnaipoteza na kuona sawa.... Kwa upumbavu wenu wa siasa za maji machafu
  • Kwa yeyote kuendelea kufikiri kuwa eti madai ya madaktari ni kwamba wametumwa na watu fulani, either mwenye kufikiri hivyo ni punguani asiyeweza kufikiri (na hivyo kufikiri wote wako kama yeye) au umetumwa kulamba uozo wa uchemfu wa mabwana zako wa serikali!

mkuu muhimbili kwa sasa inatema 200 kila mwaka, mimi nimemaliza 2010 tulikuwa 192 imagine. Otherwise nasupport mchango wako 100%
 
KUna wakati family doctor wangu huku ughaibuni alikuwa mtanzania aliyesomea Muhimbili, ila sijui njia aliyopitia baada ya kumaliza Muhimbili hadia akafikia kufanya kazi huku ughaibuni. Tulikuwa tunakutana na kuchoma mishikaki nyumbani kwangu karibu kila week-end. Baadaye akahamia hospitali nyingine nje ya state ambako alipata maslahi mazuri zaidi kwenye eneo la infectious diseases.

Nina uhakika kuwa madakatari wote ambo serikali yetu imewakomoa watapokelewa sehemu nyingine za dunia na watatulia na kutumia taaluma zao vizuri tena kwa amani sana.
 
Mwenyezi mungu amesikia kilio cha wanyonge, madaktari wakatili hao ametuepushia. Waende huko wakajiuze.
Zaman kwetu kulikuwa na msemo mbaya!-Ukienda kuwinda na mtoto wa jiran muombee achome/apige mkuki katika mapembe-watu wa matambiko bwana!
 
Mwaka huu pekee Tanzania imeshapoteza zaidi ya madaktari 150, na hapo bado mwaka haujaisha. Wako watu wanaweza kufikiri kuwa hili ni jambo la kawaida, lakini just imagine kama mkoa mmoja ungepata madaktari 150 na vifaa tiba sahihi huduma ingekuwaje? Yaani Tanzania inasomesha, wengine wanafaidi kwa sababu tu serikali imemua kuonesha ubabe!

Sikubaliani kabisa na hoja kwamba madaktari wanatumiwa na wanasiasa. Kama vifaa (tena basic) vingekuwa vinapatikana kwenye hospitali zetu, lakini madaktari wakaendelea na migomo basi hapo ningekubali ni siasa. Lakini miaka nenda miaka rudi, mazingira ya utoaji matibabu imekuwa inashuka. Na sasa tunaambiwa mwaka huu pekee serikali imetenga Tsh 8 billion kwa ajili ya matibabu ya viongozi wa juu ambao hawazidi 10, huku hospitali za Taifa zikiwa zimetengea Tshs 5 tu! Yaani watu 10 wana bajeti kuzidi kiwango kilichowekwa kutibu watu milioni 10!

95% Madai yao binafsi 5%Madai ya Vifaa...subiri Chadema wakichukuwa nchi mtawaita halafu mnawapa mshahara wa milioni 10.
 
Tunawatakia mafanikio mema huko walipo, hawa madakatari walivyokuwa na tamaa na pesa wanaweza kweli kujitolea kwenda kutibu watu bure sehemu zenye vita...Daktari gani anataka watu wafe ili madai yake yafanikiwe hizo ni tabia za magaidi.
 
Mwenyezi mungu amesikia kilio cha wanyonge, madaktari wakatili hao ametuepushia. Waende huko wakajiuze.

Unajitafutia laana kulitaja bure jina la BWANA MUNGU. Lakini inawezekana pia kuwa huyo uliemtaja ni shetani kwa wacha Mungu.
 
Mkuu tuweni objective na madai ya madaktari wetu (hapo kwa red). Wanachopigania ni maslahi yao, hili la vifaa ni kipandio tu ili wapate public support. Hivi unajua vifaa ni one point ktk orodha yao yenye madai 12?

ofcourse vifaa ni jina la ujumla sababu vifaa vyote havipo au kama vipo havitoshelezi hivyo hamna sababu ya kuviorodhesha zaidi ya kuvipa jina la ujumla 'mazingira ya kazi'.
 
95% Madai yao binafsi 5%Madai ya Vifaa...subiri Chadema wakichukuwa nchi mtawaita halafu mnawapa mshahara wa milioni 10.

kama vifaa ni asilimi 5% na serikali imeshindwa kuwatimizia ilo la vifaa na badala yake wanatimiza la posho ya kuchunguza maiti basi ni wazi tanzania maiti inathaminiwa kuliko wewe mgonjwa ambaye dactari anaitaji kifaa kukuongezea siku za kuishi.
 
Naomba ufafanuzi wa jambo hilo la wakuu kutengewa kiasi kikubwa cha pesa za matibabu cha bajeti kuliko wananchi walio milioni 40. Kama ni kweli tunahitaji vithibitisho kwa kuanzisha mada inayojitegemea ili tuijadili kwa mapana na marefu. Thanks

Candid Scope,
Matatizo yetu leo yanatoka na kukubali kujenga matabaka ndani ya wafanyakazi wa umma na jamii kwa ujumla. Kama tusingeweka kazi fulani fulani ndio zenye umaana na zenye maslahi mazuri, haya matatizo mengi yasingelikuwepo.

Specifically kwa huduma za afya, kwanini serikali inatumia gharama kubwa kutibu vigogo wachache nje ya nchi wakati mamilioni wanaokwenda kwenye hospitali za umma wanalazwa mpaka chini, bila dawa wala vitendea kazi muhimu kwa wauguzi na madaktari?

Hata iweje, haiingii akilini kabisa serikali inataka ku justify nini kwa kuwaburuza hovyo madaktari kama nao ni madereva dala dala. Mimi binafsi nafikiri madaktari wameonyesha njia...mambo yote huwa yanaanza taratibu.

Wengine sio vigogo so tukiugua lazima tukatibiwe kwenye hospitali za umma. Vifaa na madaktari wenye ari ya kazi ni muhimu. Nyinyi endeleeeni kuwapeleka watu mabepandwe kama mnafikiri ndiyo hivyo sustainable future inavyojengwa.
 
Tunawatakia mafanikio mema huko walipo, hawa madakatari walivyokuwa na tamaa na pesa wanaweza kweli kujitolea kwenda kutibu watu bure sehemu zenye vita...Daktari gani anataka watu wafe ili madai yake yafanikiwe hizo ni tabia za magaidi.

swala la kufanya kazi bure ni swala la kujitolea na sio kila mtu analiweza, jaribu kuwaambia hao viongozi wako wauze mashangingi then tukanunua madawati kisha ndo turudi tumwambie dactari afanye kazi kwa kujitolea, hivi mnadhani dactari supernatural being??
 
Tunawatakia mafanikio mema huko walipo, hawa madakatari walivyokuwa na tamaa na pesa wanaweza kweli kujitolea kwenda kutibu watu bure sehemu zenye vita...Daktari gani anataka watu wafe ili madai yake yafanikiwe hizo ni tabia za magaidi.

I thought mgomo ulimaliza baada ya kumshughulikia mwenyekiti wa mgomo?
 
Back
Top Bottom