GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,277
- 6,673
Habarini ndugu zangu wana JF, kuna hii hoja naileta hapa jamvini kwani imekuwa ikinitia mashaka. Matangazo kuhusu kondom yamekuwa mengi tena yenye kutia matumaini. Kwa kawaida watu wanapotaka kukutana kimwili huzingatia sana usafi. Mara nyingi hulazimika kunyoa sehemu za siri. Je iwapo wote watakuwa wamenyoa na tunavyofahamu system zetu za unyoaji hasa vijijini uwezekano wa kujikata ni 100% na wakakutana kimwili hii si sababu nyingine ya uwezekano wa watu kuambukizana ukimwi hata kama watakuwa wanatumia kondom? Labda hiyo kondom itengenezwe kwa mfumo wa chupi yaani unaivaa kama chupi. Je si vizuri sasa tukashauriwa kupunguza Ma***v***z kwa kutumia mikasi badala ya nyembe?. Naombeni mawazo na majibu yenu kwa hili.