Madaktari Sawa Watatoka Cuba, India na China. Manesi Je?

nakosa pa kulalia maana madai ya madaktari ni ya msingi, lakini pia serikali imekwama kuyatekeleza kwa wakati ambao madaktari inataka si kwamba haiwezi inaweza shida ni muda kwao ndilo nililosoma mpaka sasa kulingana na kauli ya pinda ila sijui wazo la kuleta madaktari toka nje ni suluhu..............SIPO KOKOTE MAANA PIA YANIPASA KUMFIKIRIA NDUGU,MTOTO,MAMA,BABA,DADA,KAKA NA JAMAA ZANGU WALIOLAZWA..... Mhhhhh!!!!!!!!! ngoja nikae pembeni kwanza
 
Hahaha wabaki na madai yao ya msingi, wakatafute shughuli nyingine wafanye kwani lazima wote wafanye kazi hospitali? si wanaweza kuwa mafundi bomba, au wakaenda veta kozi fupi ya upishi!
bwahahahhaaaaaaaaaaaaa:lol:
 
Maundumula: "Hahaha wabaki na madai yao ya msingi, wakatafute shughuli nyingine wafanye kwani lazima wote wafanye kazi hospitali? si wanaweza kuwa mafundi bomba, au wakaenda veta kozi fupi ya upishi!

Hao wa kutoka Cuba na China hatuwalipi pesa yeyote nchi hizo ni marafiki zetu watalipwa na serikali zao hapa kwetu watafanya kazi bila gharama yeyote. Tunawalipia nauli tu ya kuja na kuondoka likizo. Na huko India madokta ni wakumwaga wapo wapo tu hawana job hata dollar 200 wanaingia mzigoni as long as wana pakulala.
"

quote_icon.png
By Wang'ayo

Too late. Ushabiki wa Wanaharakati, wanasiasa na hata baadhi ya watu wengine wa kawaida kabisa hata ambao hawana uwezo wa kwenda kutibiwa nje ya Kata zao hatukuliona kama hilo ni tatizo lililochangia kukua kwa hamasa ya madaktari kugoma. Tuache Serikali itekeleze majukumu yake. Tukianza kuhoji kama Serikali itaweza hayo sasa majungu. Suala la wageni watalipwa shilingi ngapi , ni lazima tukubali hizo ndizo gharama zenyewe hasa pale wazalendo wanapokosa uzalendo. Ikibidi sasa hata mishahara ya Watumishi ipunguzwe zaidi ili kukabiliana na tatizo , hii ni kama vita huwezi kukwepa uwe unaunga mkono mgomo au la. Letu sote."

By NdasheneMbandu: "Safi sana serikali hiyo ndio maana ya kuwa na Plan B. Serikali haiwezi kushinikizwa na madaktari kumuingilia Rais madaraka yake. Leo madaktari, kesho waje walimu waseme huyu hatumtaki, kweli itakuwa utawala gani huo ?. Madaktari someni katiba ya nchi na umjue madaraka ya Rais, km hayo mnayotaka yakuchagua viongozi subirini uchaguzi mkuu 2015 au myaweke ndani ya katiba mpya."

GREAT THINKERS wa JF.

 
Nadhani mradi wa Madokta kutoka CUBA na INDIA ni another Richmond na baadaye Dowans,mradi ulio otesha Nyasi kibarua cha Edward Lowassa.

This time mchakato huu wa MaDR wa darura Kibarua cha Jakaya Mrisho Kikwete mwenyewe kitaota nyasi.

Kibaya zaidi wakienda huko CUBA watatuletea washona viatu wakidai Surgery Drs, Wahunzi wakidai ni Madaktari wa meno tutapona kweli.

Si unaajua Tena Viongozi wetu wakiona ngozi nyeupe hasa mademu na mapaja wanaota kupiga miti tu.

Watasign mikataba ya Madokta Fake wa kihindi na kikyuba wakiwa vyumbani Hotelini juu ya Vifua vya akina dada na wale machoko njemba zitakuwa makalioni mwao kama walivyosign mikataba ya madini kule London.

Umeme wa dharura ambao ni suala la kuleta machuma yasiyo ongea wameshindwa kabisa, wataweza wapi kuleta watu wenye sifa za UDr??? Labda serikali nyingine si hii wa Mahabithi wa CCM.

Serikali makini haijidanganyi kwa kuwa na mipango ya dharura ambayo inaharibu bajeti ya Nchi
bali inakua makini kwenye kutatua matatizo hayo kiumakini
umeme wa Dharura umechukua kipindi kizima cha urais wa jk na sasa madaktari wa dharura kama
wataletwa sijui itakuaje "Mungu ibariki TANZANIA,Mungu ibariki Afrika"
 
Mimi sijaona sehemu ambapo hao madaktari wamezungumzia hoja za kuwasaidia wagonjwa, kama wangekuwa na nia ya dhati wangerudi kazini wafanye kazi huku madai yanashughulikiwa..

Mkuu, ndiyo maana nimeeleza kuwa kabla hujasema hoja, tafuta taarifa sahihi, taarifa sahihi hazinyeshi tu kama mvua za vuli. Kama hoja ni kuboresha mazingira ya utabibu, ikiwa ni pamoja na mfano wa kukosekama vitu kama X Ray, wewe hujui hiyo ni kwa manufaa ya mgonjwa? Kwa nini hospitali za binafsi ziwe na mashine basic tu kama X Ray, halafu hospitali yako ya RUFAA isiwe nayo, na wewe unayefanya kazi hapo bado ujione uko kazini?
 
JK ana kazi ngumu. Serikali imefilisika, halafu waagize madaktari kutoka nje? kwa gharama ya nani? Mimi nafikiri mwisho wa utawala huu uko mlangoni, na hizi ndizo dalili zake. Waalimu nao wakigoma na kumtaka Kawambwa ajiuzulu kwa kushindwa kazi, tutawaagiza kutoka wapi?. JK acha kiburi, jali raia wako, unazidi kukimaliza chama chako cha CCM.
 
Kufanya kazi ya udaktari Tanzania ni lazima uwe na moyo wa chuma! Acha waje tuwakope, baada ya wiki wataanza kutimka mmoja baada ya mwingine. Kwanza lugha kuelewana na wagonjwa itakuwa tabu lakini pia mazingira ya kazi. Kule kwao walishazoea mazingira safi, malipo safi na allowance zingine kibao.

Na tutawakopa mwanzo mwisho,chezea serikali ya Magamba! halafu wanakutana na vifaa hakuna sijui wataenda kufanya operation theater bila gloves!
 
Hao wa kutoka Cuba na China hatuwalipi pesa yeyote nchi hizo ni marafiki zetu watalipwa na serikali zao hapa kwetu watafanya kazi bila gharama yeyote. Tunawalipia nauli tu ya kuja na kuondoka likizo. Na huko India madokta ni wakumwaga wapo wapo tu hawana job hata dollar 200 wanaingia mzigoni as long as wana pakulala.

Kina mangungo na Msovelo (na mikataba ya kina Karl Peters) kumbe bado wapo zama hizi pia!!
 
Nimepita mahala hapa nimewasikia madaktari wakiongea kwenye East Africa Radio sasa hivi katika Supa Mix wanaelezea kwa kina madai yao.
 
Hahaaaa na watafanya kazi kwa muda gani??
Haina shaka maana wana hela za kuwalipa hao ila za kuwapa watanzania hazipo
sasa ngoja madaktari wa kitanzania nao waondoke ndio watajua umuhimu wa kutenganisha ujuzi na siasa.
 
Hao madaktari wa kutoka India wanajua kiswahili?lazima tujiulize watawatibu vipi watanzania ambao asilimia kubwa hawaongei kingereza?kumbuka zaidi ya madaktari tutahitaji kila daktari kuwa na mkalimani hizo garama zitalipwa na nani?ni bora kugharamia hao madaktari kutoka nje au kuwawajibisha hao mawaziri?Serikali yetu haifikiri kwa kina juu ya mambo inayofanya inakurupuka tu ngoja hao madaktari waje na manesi wagome tuone hao madaktari kama watafanya kazi bila manesi.
 
Hahaaaa na watafanya kazi kwa muda gani??
Haina shaka maana wana hela za kuwalipa hao ila za kuwapa watanzania hazipo

Madaktari wenu wa kitanzania hawataki hela, wanataka siasa inabidi serikali iwapatie fursa waingie kwenye Politics kwa kuwaleta madokta ambao wapo passionate na kazi yao.
 
Hao madaktari wa kutoka India wanajua kiswahili?lazima tujiulize watawatibu vipi watanzania ambao asilimia kubwa hawaongei kingereza?kumbuka zaidi ya madaktari tutahitaji kila daktari kuwa na mkalimani hizo garama zitalipwa na nani?ni bora kugharamia hao madaktari kutoka nje au kuwawajibisha hao mawaziri?Serikali yetu haifikiri kwa kina juu ya mambo inayofanya inakurupuka tu ngoja hao madaktari waje na manesi wagome tuone hao madaktari kama watafanya kazi bila manesi.

Kwani mtanzania akienda kufanya biashara China anatumia lugha gani? Au unadhani wote wanaoenda China wanajua kiingereza? au unadhani wale wachina kule wanajua kiswahili?

Unafikiri ile hospitali ya Wapalestina pale Sinza wakati wapalestina wenyewe wapo walikuwa wanatibia vipi?
 
Kwa maoni yangu ni kwamba wakati wa matatizo kama huu ni muhimu kila mtanzania akajali masilahi mapana ya Nchi
yetu kwanza.katika hili nadhani Mheshimiwa Rais anashauriwa vibaya kwanza kwasababu kwa vyovyote vile hawa MAWAZIRI hawakutakiwa kuwajibu madaktari kwa namna ambayo imechochea MGOMO HUU ZAIDI.Walipaswa kuelewa
kiini cha mgomo halafu wawape ufafanuzi wa madai yao kwa upole, unyenyekevu na kwa namna ambayo madaktari
wangejua halihalisi ya uwezo wa serikali na pengine wangeweza kuwa na subira na wangeahirisha mgomo wao.lakini
ukiwajibu kwa kiburi cha kulewa madara na kwamba nani aliwatuma kusomea udaktari,hii siyo lugha ya kusuluhisha
migogoro sehemu za kazi bali inachochea na kukatisha tamaa.Na kwasababu hawakutumwa kuwajibu vibaya watendaji
wao,nadhani ni vizuri wakakubali kujiuzuru kwa hiari yao na mheshimiwa RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
akubali kwa masilahi mapana ya NCHI.
Kuleta madaktari kutoka nje ya NCHI ni kuendeleza tug of war kusiko na lazima yoyote.katika hili hakuna mshindi wala mshindwa.madaktari ni watoto wa watanzania hawahawa,serikali ikiamua kuwatosa ijue kuwa imejitengenezea maadui wengi wa ndani kuliko inavyojijengea heshima! KUKIRI MAPUNGUFU SIYO UDHAIFU,ni vizuri serikali ikarudi chini wawasikilize madaktari na baadhi ya madai yao wayatekeleze kwa heshima ya NCHI yetu.
mwisho, kila mgogoro unakawaida ya kuujenga upande mmoja na kuubomoa upande mwingine.NI VIZURI
WAKALIPIMA HILI.Je, mpaka mwisho wa sakata HILI tutabaki kuwa wamoja? CCM JE,watakuwa salama kama awali?au
fursa imetolewa vyama vingine viaminiwe zaidi na wananchi?
 
Du,hii imekaa vizuri,ngoja nijiandae kuomba post ya ukalimani muhimbili,maana najua nafasi zitakuwa nyingi kwa sisi ambao ni billingual,hao madaktari wa Cuba na China kila mmoja atahitaji mkalimani wa kukaa naye wakati anamsikiliza mgonjwa wa kibantu,pia prescription ya Kichina manesi na watu wa Pharmacy watahitaji wa kuwatafsiria.Nadhani ahadi ya kuongeza ajira kwa watanzania itakuwa imetimia.Kidumu chama cha mapinduzi.


Mkuu unatisha!. Hili ni bonge la dili. Tuombee walimu nao wagome ili waletwe wa kichina hadi kwenye shule za kata. Hii itaboresha sana ubora wa elimu yetu haswa katika hizi shule za St Kayumbas.
 
Walete vipi?? kwani wanasheria wamegoma au wahandisi?? Hao ni watu makini hawwajiingizi katika migogoro hasi kwa Taifa

hela uliyohongwa ikisha utaelewa maana ya sentensi hiyo kwa sasa huwezi elewa, umelewa rushwa. Walimu kila siku wanadai mishahara halafu serikali inajidai ina ubavu wa kuleta madokta wa kigeni!!!!!!!!!!!!!!!
 
hilo wa si la dharura , Maktari walifikiri wao tu ndiyo wamesomea fani hiyo. Big up Government.
Sisi tuendelee na majungu yetu humu JF wakati Serikali ikiwajibika.

sawa kabisa, wanaringia vi dispensary walivyofungua kwa kuiba madawa msd, sasa tunafilisi kabisa ili kurudisha heshima. Dai la kutaka lazima waziri wa afya na naibu wake wafukuzwe ni la kipumbavu..
 
Hizo ni hadithi za sungura na fisi, serikali yenyewe imefilisika kisha iwe na uwezo wa kuleta madaktari toka nje, aaaaaaaaaaaaaaah hilo ni tishio tu ila uwezo haupo kabisa.Swali ni Je hao wadaktari watahudumu mpaka kule kwetu Kantalamba ambako bado sindano tunachemsha ili tuweze tumia tena, huo sio ukweli.
 
Wageni wa kudumu, wa muda hadi mgomo uishe au?? Maamuzi mengine yana walakini!!!
 
Back
Top Bottom