Madaktari Sawa Watatoka Cuba, India na China. Manesi Je?

Katika mgomo huu SLAA ni mtuhumiwa numba moja. Asijifanye kukaa kimya kana kwamba wananchi hawajui hilo.

Mambo yakizidi kuwa mabaya asifikiri atapona , wananchi wataanza naye si alishasema kwamba nchi haitatawalika? kwa nini abaki? Kwanza yupo au kishakimbilia Karatu.

Tumelalama mgomo mgomo, umeanza sasa wasiwasi wetu nini Malengo yetu si yametimia? Tusiisakame tena Serikali. Tuliotaka kuwafurahisha tumeshawafurahisha. Nilifikiri sasa humu JF tungekuwa tunashangilia mgomo kuanza kwa akili zetu finyu tulivyokuwa tukiunga mgomo bila hata haya. Sasa mbona tunachangia kama tumeingia na hofu fulani? kwa nini tusiwe na ujasiri uleule?

Walikuwa wanadai Mawaziri wajiuzulu. Yaani Madaktari bwana thehe thehe thehe, kwa hiyo wasipojiuzulu watoto wa Madaktwari haya hawatakwenda choo? Kazi kweli kweli. Daktari acheni hizo bwana. Mnajua kazi yenu kama kazi nyingine tu. Hivi Daktari ukipewa kazi ya kutengeneza hata stuli utaweza kweli? ukiambiwa umfundishe mtoto wa miaka mitatu hadi ajue kusoma utaweza? ukiambiwa kazi yako ni kuimba kwenye jukwaa ili watoto wako wapate kula utaweza? ukiambiwa ukatembee na viatu unauza mitaani kutoka Igoma hadi Nyakato, Ghana hadi Kirumba utaweza kweli Daktari? Basi hivyo wenzenu tunavyoteseka kuhakikisha familia zetu zinaishi. Kazi yenu kama kazi zingine
Hizi akili kama vile nazi za pale magogoni..
 
Ndugu zangu,

Kuna taarifa zisizo rasmi kuwa Serikali ipo kwenye hatua ya mwisho ya utekelezaji wa mpango wa dharura wa kuleta madaktari kutoka nchi za Cuba, India na Cihina ili kuziba pengo kubwa lililoachwa na madaktari watanzania ambao wamegoma. Ninachojiuliza ni je, madaktari hao wa nje watalipwa na nani na watakaa hapa nchini kwa muda gani? Na je, manesi nao wakiamua kuwasindikiza madaktari, Serikali itafanya nini? Italeta manesi wengine kutoka nje?

Maswali haya na mengine mengi, yananielekeza kuamini kuwa suluhisho la suala hili ni kwa Serikali kuamua KUSHUKA kwa rais kukubali kuwastaafisha mawaziri wake kwa maslahi pana ya umma. Wapo wanaosema kwamba rais akifanya hivyo, atakuwa amejishusha sana. Lakini tujiulize, hivi ni nani mkubwa kati ya rais na wananchi kwa ujumla wao? Kwa nchi inayoheshimu utawala wa demokrasia kwelikweli, rais lazima atajiona kuwa yeye ni mtumwa wa wananchi wake. Kwa hiyo, inapotokea kelele za wananchi wake ambao ndiyo waajiri zimezidi, lazima achukue hatua hata kama wakati mwingine hafurahi kufanya hivyo. Asipofanya hivyo, kama ilivyo sasa kwa kikwete, ataendelea kuwatesa wananchi na kuwasababishia vifo ambavyo kimsingi vingeweza kuepukika.

Kauli ya anayejiita 'Mtoto wa Mkulima' Bw. Mizengo Pinda kwamba madaktari wanafanya makosa kumpa masharti BWANA MKUBWA yaani kikwete, imeniudhi sana. Ni kauli inayoashiria kibuli cha viongozi wa kiafrika. Kwamba rais ni bwana mkubwa asiyeweza kulazimishwa na mtu yeyote kufanya jambo fulani. Hili ndiyo tatizo la msingi la viongozi na hasa wa ccm kujiona kuwa kama MIUNGU MTU. Kwangu mimi, kiongozi anayefuata MATAKWA YA WANANCHI huyo ndiye kiongozi mzuri. Asipofanya hivyo, atuambie anafanya kwa maslahi ya nani!

Cuba nasikia wana makabila kama tanzania, hivyo watapelekwa mikoa mbalimbali kutokana na lugha zao wanazoongea...mpaka kimasai wapo na kichanga, kikwere, kirangi kudadadek..madr wa tz hawakujua hilo
 
Du,hii imekaa vizuri,ngoja nijiandae kuomba post ya ukalimani muhimbili,maana najua nafasi zitakuwa nyingi kwa sisi ambao ni billingual,hao madaktari wa Cuba na China kila mmoja atahitaji mkalimani wa kukaa naye wakati anamsikiliza mgonjwa wa kibantu,pia prescription ya Kichina manesi na watu wa Pharmacy watahitaji wa kuwatafsiria.Nadhani ahadi ya kuongeza ajira kwa watanzania itakuwa imetimia.Kidumu chama cha mapinduzi.

Well said, yaani i were about to say comment about the need of translators, ukaniwahi!......na wabantu lugha za kigeni tulivyo kimeo mbona itakua shughuli....kiingereza tu cha shule shida itakua kichina au kicuba!
 
Kadandia vipi sasa? asitoe maoni yake? hao madaktari wasiwe kama watoto wadogo ambao wana demand kitu papo kwa papo,, naunga mkono serikali kuleta madaktari mbadala, tuone watakula wapi. Tusitake kunyanyasa wananchi hapa kisa eti daktari!! Na sisi wabeba zege tukigoma nani atawajengea majumba yenu? acheni upuuzi. Piga chini hao
Sidhani kama umeelewa point yangu kamanda wangu, ni yaleyale tu gari laenda Pugu, we waenda Kimara unalipanda. Utafika lini kwenu?!!! Kwa ufupi mnauza ng'ombe kwa kesi ya kuku? Au unachinja ng'ombe kwa order ya maini?
 
Kweli nimefurahi sana kwa serikali kuchukua hatua hii. Hawa jamaa wangetusumbua sana huko mbele endapo serikali itasikiliza kila wanachotaka. Kesho wanaweza kuamka na kumwambia Rais amwache Mama Salma fasta la sivyo watagoma!! Upuuzi huu na huwezi kuamini eti ni wasomi,,,, watu wengi wamesoma na wana taaluma tofauti, vipi hawa wanajiona matawi sana? walimu je? hata wabeba zege na mama lishe, kila mtu ana nafasi yake kwenye ujenzi wa Taifa. No wonder jana kwenye taarifa ya habari ITV wagonjwa na wananchi Hospital ya Temeke, hasira zao si kwa serikali sasa, bali kwa madaktari,, wameshasema sasa wataanza kutembeza kipondo kwa kila daktari. Ukionekana na magwanda meupe tu,, unapewa za uso,,, kwishney!!
I am very very happy,, hongera serikali....wacha sisi tuendelee na umbeya humu
 
Serikali haikuwahi kudhani itafika siku au majira wenye nchi watazinduka na kufuatilia kila kitu wanachofanya. Pazia limepasuka watu wanaona, wanasikia na wanachukua hatua kwa yale waliyoyaona na kusikia. Mi naona huu ni mwanzo, mengi sana yanafukura chini kwa chini na yatfumuka tu.

Sasa badala ya vitisho, ulaghai na kauli za kisiasa za Pinda nk, huu sio wakati wa wake, waeoneshe uwajibikaji kivitendo na kutatua kero za afya (ikiwemo ya madaktari). Warudi chini (basics), wajifunze kutumikia na sio kuwa miungu watu ktk kutawala. For sure serikali haiwezi hata kidgo kushindana na wenye nchi ambao ni 40m+. Ukitoa wana ccm 5-3m still the extreme majority will discipline it any way.
 
Sidhani kama umeelewa point yangu kamanda wangu, ni yaleyale tu gari laenda Pugu, we waenda Kimara unalipanda. Utafika lini kwenu?!!! Kwa ufupi mnauza ng'ombe kwa kesi ya kuku? Au unachinja ng'ombe kwa order ya maini?
Hapo penye rangi nadhani swali hilo linawahusu sana madaktari ambao eti kwa madai yao, wanaweka rehani maisha ya watu!! Hivi nani hana madai Tanzania hii? Watu wafe ili wewe upate unachotaka?? si ndiyo kuchinja ng'ombe upate maini?? Wee hii methali unaijua au umei copy tu?? Rudi darasani
 
manesi wataazimwa hospitali ya apolo, india.
Na pia watafunza wengine kwa crush program.
Ila hawa viongozi wetu, sidhani kama ni wazima.
 
Hivi hiyo orientation hao wahindi na wacuba watapewa na nani?. Nasikia wajeshi wenyewe walizimia walipoingia Muhimbili. Na je wataweza kuwaleta katika kila kituo cha mkoa? kwa gharama ya nani? kwa manufaa ya nani?
 
Watanzania hawajaelewa ukweli kuhusu madai ya Madaktari. Its not about the money. Kuna recognition ya mchango wao kwenye taifa. Kupotea kwa thamani ya profession ya Udaktari. Ilifikia kiwango yule Mama anawaambia eti Nani aliwatuma mkasomee udaktari. Its about time the country places priority and value to this special and rare profession. From working environment to supportive facilities Waache siasa wasolve matatizo yanayo wakabili madakatari kitaalamu. Kwani

Mwalimu wako aliyekufundisha udaktari utampa recognition gani!
 
Tatizo la nchi hii hatuna viongozi wenye uwezo wa kufikiri. Basi na walete walimu, wanasheria, wahandisi na wengineo kutoka huko wanakosema.
 
Hivi hiyo orientation hao wahindi na wacuba watapewa na nani?. Nasikia wajeshi wenyewe walizimia walipoingia Muhimbili. Na je wataweza kuwaleta katika kila kituo cha mkoa? kwa gharama ya nani? kwa manufaa ya nani?
Hilo si tatizo,, kwanza elewa kwamba si mikoa yote wamegoma. Morogoro, KCMC, Singida, Tabora etc madaktari wanachapa kazi kama kawaida. Sasa hapo ndipo serikali itayumia divide and rule,, kwamba wanaotaka kazi apply upya kushirikiana na hawa wanaotoka nje. Na pia si taabu maana tunao madaktari wanajeshi ambao watatoa ushirikiano mzuri tu kwa wataalamu wa "UKWELI" toka nje. Karibuni sana wataalamu nchini kwetu. Unauliza kwa gharama ya nani?? wee unaijua gharama ya uhai wa watu wanaoathirika na mgomo huu?? mbona hilo unalifumbia macho? ni gharama ya nani? Unauliz kwa faida ya nani?? Hapa napata mashaka kuhusu uelewa wako.
Angalizo: Wale tuliokuwa tunashabikia saaaaana,, inueni mioyo....
 
kulikua na mpango wa dharura uliopitishwa na tanesco kuhusiana na umeme.

Sasa na huu mpango wa dharura wa madaktari kama utafanikiwa kupita itakuwa ni historia.

Just imagine mtu unamaiti inakuozea ndani badala ufanye mpango wa kumpumzisha mwili wa marehemu,ndo kwanza unataka utumie watu wengine waje kukusaidia kuzika,wakati hata hao unaotaka kuwatumia kwao watokako kuna maiti pia wanaohitaji kupumzishwa.

Hii ndiyo.....
Tanza-NIA.
 
Tatizo la nchi hii hatuna viongozi wenye uwezo wa kufikiri. Basi na walete walimu, wanasheria, wahandisi na wengineo kutoka huko wanakosema.
Walete vipi?? kwani wanasheria wamegoma au wahandisi?? Hao ni watu makini hawwajiingizi katika migogoro hasi kwa Taifa
 
manesi wataazimwa hospitali ya apolo, india.
Na pia watafunza wengine kwa crush program.
Ila hawa viongozi wetu, sidhani kama ni wazima.

Karibu sana Makene.
Nitafurai kujua kamando wewe nikujuaye.
 
Ndugu Serikali imedinda na Madokta wamegoma..
Wananchi tufanye nin? Tupunguze Siasa.
 
Ndugu zangu,

Kuna taarifa zisizo rasmi kuwa Serikali ipo kwenye hatua ya mwisho ya utekelezaji wa mpango wa dharura wa kuleta madaktari kutoka nchi za Cuba, India na Cihina ili kuziba pengo kubwa lililoachwa na madaktari watanzania ambao wamegoma. Ninachojiuliza ni je, madaktari hao wa nje watalipwa na nani na watakaa hapa nchini kwa muda gani? Na je, manesi nao wakiamua kuwasindikiza madaktari, Serikali itafanya nini? Italeta manesi wengine kutoka nje?!

This will be one of those foolish decision the govt of JK will do. Yaani serikali iingie gharama za kubwa kwaaajili ya watu wawili tu Drs. Mponda and Nkya! Mind you hadi hii leo 08/03/12 baadhi ya Idara na Taasisi za Serikali hazipata mshahara wa mwezi Februray because HAZINA imekauka!

Hii inanikumbusha SIASA kutumikia UCHUMI wakati wenzetu walioendelea UCHUMI ndiyo unatumikia SIASA. We real have inveted priorities!
 
Ndugu zangu, Kuna taarifa zisizo rasmi kuwa Serikali ipo kwenye hatua ya mwisho ya utekelezaji wa mpango wa dharura wa kuleta madaktari kutoka nchi za Cuba, India na Cihina ili kuziba pengo kubwa lililoachwa na madaktari watanzania ambao wamegoma. Ninachojiuliza ni je, madaktari hao wa nje watalipwa na nani na watakaa hapa nchini kwa muda gani? Na je, manesi nao wakiamua kuwasindikiza madaktari, Serikali itafanya nini? Italeta manesi wengine kutoka nje?!

This will be one of those foolish decision the govt of JK will do. Yaani serikali iingie gharama za kubwa kwaaajili ya watu wawili tu Drs. Mponda and Nkya! Mind you hadi hii leo 08/03/12 baadhi ya Idara na Taasisi za Serikali hazipata mshahara wa mwezi Februray because HAZINA imekauka!

Hii inanikumbusha SIASA kutumikia UCHUMI wakati wenzetu walioendelea UCHUMI ndiyo unatumikia SIASA. We real have inveted priorities!
 
Too late. Ushabiki wa Wanaharakati, wanasiasa na hata baadhi ya watu wengine wa kawaida kabisa hata ambao hawana uwezo wa kwenda kutibiwa nje ya Kata zao hatukuliona kama hilo ni tatizo lililochangia kukua kwa hamasa ya madaktari kugoma. Tuache Serikali itekeleze majukumu yake. Tukianza kuhoji kama Serikali itaweza hayo sasa majungu. Suala la wageni watalipwa shilingi ngapi , ni lazima tukubali hizo ndizo gharama zenyewe hasa pale wazalendo wanapokosa uzalendo. Ikibidi sasa hata mishahara ya Watumishi ipunguzwe zaidi ili kukabiliana na tatizo , hii ni kama vita huwezi kukwepa uwe unaunga mkono mgomo au la. Letu sote.

Suala hapa ni hizi nguvu na uwezo wa kushughulikia dharura utakuwa umepatikana wapi wakati mambo madogo yaliyo katika madai ya madaktari serikali imeshindwa kuyafanya? Unadhani hata kama watumishi wote wa serikali wakistaafishwa ghafla ili pesa itumike kulipia hao madaktari watokao nje ya nchi, pesa hiyo itakuwa njugu tu. Ni upuuzi kufikiria kujenga ukuta wa muda wakati ufa uliuona tangu mwanzo. Of course sina hakika kama serikali yetu hii inalifikiria hili hata kidogo. Yenyewe itasubiri tu kutoa takwimu za vifo na kuzitangaza ili madaktari waonekane kama si binadamu. Kama unadhani itajihangaisha kukuletea madaktari, subiri uone. Wao watazifuata huduma huko huko zilipo. Ndugu zangu mimi watasubiri tiba ya m-Cuba hadi kaburini!!
 
Back
Top Bottom