NdasheneMbandu
JF-Expert Member
- Jan 2, 2012
- 940
- 308
Ndugu zangu,
Kuna taarifa zisizo rasmi kuwa Serikali ipo kwenye hatua ya mwisho ya utekelezaji wa mpango wa dharura wa kuleta madaktari kutoka nchi za Cuba, India na Cihina ili kuziba pengo kubwa lililoachwa na madaktari watanzania ambao wamegoma. Ninachojiuliza ni je, madaktari hao wa nje watalipwa na nani na watakaa hapa nchini kwa muda gani? Na je, manesi nao wakiamua kuwasindikiza madaktari, Serikali itafanya nini? Italeta manesi wengine kutoka nje?
Maswali haya na mengine mengi, yananielekeza kuamini kuwa suluhisho la suala hili ni kwa Serikali kuamua KUSHUKA kwa rais kukubali kuwastaafisha mawaziri wake kwa maslahi pana ya umma. Wapo wanaosema kwamba rais akifanya hivyo, atakuwa amejishusha sana. Lakini tujiulize, hivi ni nani mkubwa kati ya rais na wananchi kwa ujumla wao? Kwa nchi inayoheshimu utawala wa demokrasia kwelikweli, rais lazima atajiona kuwa yeye ni mtumwa wa wananchi wake. Kwa hiyo, inapotokea kelele za wananchi wake ambao ndiyo waajiri zimezidi, lazima achukue hatua hata kama wakati mwingine hafurahi kufanya hivyo. Asipofanya hivyo, kama ilivyo sasa kwa kikwete, ataendelea kuwatesa wananchi na kuwasababishia vifo ambavyo kimsingi vingeweza kuepukika.
Kauli ya anayejiita 'Mtoto wa Mkulima' Bw. Mizengo Pinda kwamba madaktari wanafanya makosa kumpa masharti BWANA MKUBWA yaani kikwete, imeniudhi sana. Ni kauli inayoashiria kibuli cha viongozi wa kiafrika. Kwamba rais ni bwana mkubwa asiyeweza kulazimishwa na mtu yeyote kufanya jambo fulani. Hili ndiyo tatizo la msingi la viongozi na hasa wa ccm kujiona kuwa kama MIUNGU MTU. Kwangu mimi, kiongozi anayefuata MATAKWA YA WANANCHI huyo ndiye kiongozi mzuri. Asipofanya hivyo, atuambie anafanya kwa maslahi ya nani!
Kuna taarifa zisizo rasmi kuwa Serikali ipo kwenye hatua ya mwisho ya utekelezaji wa mpango wa dharura wa kuleta madaktari kutoka nchi za Cuba, India na Cihina ili kuziba pengo kubwa lililoachwa na madaktari watanzania ambao wamegoma. Ninachojiuliza ni je, madaktari hao wa nje watalipwa na nani na watakaa hapa nchini kwa muda gani? Na je, manesi nao wakiamua kuwasindikiza madaktari, Serikali itafanya nini? Italeta manesi wengine kutoka nje?
Maswali haya na mengine mengi, yananielekeza kuamini kuwa suluhisho la suala hili ni kwa Serikali kuamua KUSHUKA kwa rais kukubali kuwastaafisha mawaziri wake kwa maslahi pana ya umma. Wapo wanaosema kwamba rais akifanya hivyo, atakuwa amejishusha sana. Lakini tujiulize, hivi ni nani mkubwa kati ya rais na wananchi kwa ujumla wao? Kwa nchi inayoheshimu utawala wa demokrasia kwelikweli, rais lazima atajiona kuwa yeye ni mtumwa wa wananchi wake. Kwa hiyo, inapotokea kelele za wananchi wake ambao ndiyo waajiri zimezidi, lazima achukue hatua hata kama wakati mwingine hafurahi kufanya hivyo. Asipofanya hivyo, kama ilivyo sasa kwa kikwete, ataendelea kuwatesa wananchi na kuwasababishia vifo ambavyo kimsingi vingeweza kuepukika.
Kauli ya anayejiita 'Mtoto wa Mkulima' Bw. Mizengo Pinda kwamba madaktari wanafanya makosa kumpa masharti BWANA MKUBWA yaani kikwete, imeniudhi sana. Ni kauli inayoashiria kibuli cha viongozi wa kiafrika. Kwamba rais ni bwana mkubwa asiyeweza kulazimishwa na mtu yeyote kufanya jambo fulani. Hili ndiyo tatizo la msingi la viongozi na hasa wa ccm kujiona kuwa kama MIUNGU MTU. Kwangu mimi, kiongozi anayefuata MATAKWA YA WANANCHI huyo ndiye kiongozi mzuri. Asipofanya hivyo, atuambie anafanya kwa maslahi ya nani!