Madaktari nisaidieni: Ugonjwa gani huu!

Polisi

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
2,082
639
Nimekuwa nikisumbuliwa na ugonjwa ambao unanichanganya sana na nimedumu nao kwa miaka 12 sasa. Mwili kuwaka moto na maumivu kwenye kifua. Mara nyingi huanza maumivu makali kwenye kifua, si kubana bali ninavyosikia ni dhahiri kama kuna vidonda maana wakati fulani panaweza kupoa kabisa, lakini labda ukipata chakula fulani au hata kinywaji maumivu yanaanza. Hapo viungo vingi vya mwili huanza kuwaka moto ikiwemo mikono, miguuni kwenye nyayo, sehemu yote ya kichwa pamoja na maumivu kwenye mgongo. Wakati mwingine nasikia maumivu makali kwenye kifua lakini baadhi ya viungo hususani mikono huonekana kama inauma lakini kana kwamba ina ganzi.

Mwanzoni ilibainika ni ulcers, nikatumia sana dawa za hospitali na nikapima vipimo pale muhimbili na kuendelea na dawa za hospitali na kienyeji ikiwemo ya dr . rahabu. Hivi karibuni nimepima mara mbili na kuambiwa ulcers imepona. Cha kushangaza bado maumivu makali kwenye kifua.

Nimeona niulize hili maana wiki hii nina appointment na dr. mmoja ambapo nataka nimwombe anipige x ray.Naomba mnisaidie kuutambua ugonjwa huu ili niwe na input ya kutosha kumsimulia daktari. Kuna daktari mmoja alishawahi guess kuwa yawezekana ini likawa na tatizo na akanishauri nitumie mitishamba. nilitumia kwa siku 7/15 nikakatisha dozi baada ya maumivu kuzidi kuliko kawaida.

Naombeni msaada wenu wakuu

UPDATE 13/09/2011
Nilikwenda hospitali ya muhimbili kama watalaamu humu walivyonishauri na kufanyiwa kipimo cha endoscopy. Majibu ni kwamba hakuna vidonda vya tumbo bali kuna fungus kwenye kifua na nikapewa dawa inaitwa fluconazole kwa siku 14. Baadaye nikaenda regency kwa ajili ya x ray na majibu hakuna tatizo.

Hali yangu baada ya kumaliza dozi
Kwa kweli najisikia vizuri ingawa bado maumivu nayasikia wakati fulani ingawa si makali kama awali. Nadhani fungus hazijaisha. So naombeni ushauri nirudie dozi au nitumie dawa gani tena.
Wasalaam
 
Nimekuwa nikisumbuliwa na ugonjwa ambao unanichanganya sana na nimedumu nao kwa miaka 12 sasa. Mwili kuwaka moto na maumivu kwenye kifua. Mara nyingi huanza maumivu makali kwenye kifua, si kubana bali ninavyosikia ni dhahiri kama kuna vidonda maana wakati fulani panaweza kupoa kabisa, lakini labda ukipata chakula fulani au hata kinywaji maumivu yanaanza. Hapo viungo vingi vya mwili huanza kuwaka moto ikiwemo mikono, miguuni kwenye nyayo, sehemu yote ya kichwa pamoja na maumivu kwenye mgongo. Wakati mwingine nasikia maumivu makali kwenye kifua lakini baadhi ya viungo hususani mikono huonekana kama inauma lakini kana kwamba ina ganzi.

Mwanzoni ilibainika ni ulcers, nikatumia sana dawa za hospitali na nikapima vipimo pale muhimbili na kuendelea na dawa za hospitali na kienyeji ikiwemo ya dr . rahabu. Hivi karibuni nimepima mara mbili na kuambiwa ulcers imepona. Cha kushangaza bado maumivu makali kwenye kifua.

Nimeona niulize hili maana wiki hii nina appointment na dr. mmoja ambapo nataka nimwombe anipige x ray.Naomba mnisaidie kuutambua ugonjwa huu ili niwe na input ya kutosha kumsimulia daktari. Kuna daktari mmoja alishawahi guess kuwa yawezekana ini likawa na tatizo na akanishauri nitumie mitishamba. nilitumia kwa siku 7/15 nikakatisha dozi baada ya maumivu kuzidi kuliko kawaida.

Naombeni msaada wenu wakuu
Pole sana mkuu,Ngoja tuwasubiri watalaam waje watujuze!
 
pole sana polisi.umewahi kufikiria inaweza kuhusiana na kazi unayofanya?kama hutojali,siku yako ya kawaida inakuwa kwenye mazingira gani?
 
pole sana polisi.umewahi kufikiria inaweza kuhusiana na kazi unayofanya?kama hutojali,siku yako ya kawaida inakuwa kwenye mazingira gani?

Asante mkuu. wakati mwingine kutokana na mazingira huwa nashawishika kuwa kuna uhusiano kati ya maumivu haya na kazi ninayoifanya. Mfano wakati nikiwa UDSM maumivu ya mwili kuwaka moto hasa miguu nilikuwa nahusisha sana na zile movement za kubadilisha madarasa, kupanda ngazi na ile kimbia kimbia kuwahi lecture. Pia maumivu ya kifua na kichwa kuuma kwa kuwaka moto ilikuwa inatokea sana wakati wa mitihani hususani course work. Si unajua mkuu, wakati mwingine unaletewa karatasi umepata 2/15 n.k. Kazi yangu ya sasa ina involve a lot of decision making. karibu
 
Pole Polisi,

Kuna wakati daktari kama binadamu 'anastuck' kuwa na uhakika ni nini hasa kinamsumbua mgonjwa wake, sababu ugonjwa una sehemu mbili naweza sema....1. physical component/illness, hii inaweza tambulika kwa mgonjwa kujieleza na pia kujibu maswali ya daktari, na kisha vipimo vikaonyesha na akapata matibabu...2. psychological component, hii mgonjwa anaweza kujisikia na physical illness, au alikuwa na physical illness akatibiwa akapona lakini akaendelea kujisikia anaumwa bado wakati hana physical illness (soma Somatoform disorders). Mara nyingi hii huwa vipimo vyote vinaonyesha hakuna illness lakini mgonjwa anajisikia mgonjwa kabisa (sio anadanganya).

Sisemi kuwa una somatoform disorder, lakini ni vigumu sana kuwa na ugonjwa ambao kwa miaka 12 haujajulikana na wala haujatibiwa ipasavyo. Maumivu unayoyaongelea kifuani karibu na chembe mara nyingi ni ulcers, na kama yanakuwa makali zaidi baada ya kula ni tabia ya vidonda vya tumbo sehemu ya duodenum (unapoanzia utumbo mdogo).

Ushauri: Njia nzuri ya kutatua tatizo lako ni kuonana na daktari bingwa, akaufanyia vipimo vyote muhimu, na vikithibitisha huna physical illness, basi hudhuri clinic ya somatoform disorders Muhimbili na counselling tu itakutibu!
 
.
Pole Polisi,

Kuna wakati daktari kama binadamu 'anastuck' kuwa na uhakika ni nini hasa kinamsumbua mgonjwa wake, sababu ugonjwa una sehemu mbili naweza sema....1. physical component/illness, hii inaweza tambulika kwa mgonjwa kujieleza na pia kujibu maswali ya daktari, na kisha vipimo vikaonyesha na akapata matibabu...2. psychological component, hii mgonjwa anaweza kujisikia na physical illness, au alikuwa na physical illness akatibiwa akapona lakini akaendelea kujisikia anaumwa bado wakati hana physical illness (soma Somatoform disorders). Mara nyingi hii huwa vipimo vyote vinaonyesha hakuna illness lakini mgonjwa anajisikia mgonjwa kabisa (sio anadanganya).

Sisemi kuwa una somatoform disorder, lakini ni vigumu sana kuwa na ugonjwa ambao kwa miaka 12 haujajulikana na wala haujatibiwa ipasavyo. Maumivu unayoyaongelea kifuani karibu na chembe mara nyingi ni ulcers, na kama yanakuwa makali zaidi baada ya kula ni tabia ya vidonda vya tumbo sehemu ya duodenum (unapoanzia utumbo mdogo).

Ushauri: Njia nzuri ya kutatua tatizo lako ni kuonana na daktari bingwa, akaufanyia vipimo vyote muhimu, na vikithibitisha huna physical illness, basi hudhuri clinic ya somatoform disorders Muhimbili na counselling tu itakutibu!

Asante mkuu
 
Pole sana . Fuata ushauri uliopewa na uzidishe maombi Mungu atakusaidia.
 
pole sana Mkuu Polisi kwanza kabisa nakushauri nenda Hospitali ukapige picha ya ( X Ray.) ili tuweze kupata majibu ya kutoka kwa Daktari tujuwe unaumwa kitu gan. tukisha pata hayo majibu ndio tutaweza kukupa ushauri mzuri
 
Pole sana.
Ina maana kuna mitandao fulani ya mwili haifanyi kazi vizuri. Tumia maji hai yaani biowater yaliyotengenezwa kwa bio disc. tembelea Amezcua .UNAWEZA NIANDIKIA NJE YA FORUM HII
UNIQUE
 
pole sana Mkuu Polisi kwanza kabisa nakushauri nenda Hospitali ukapige picha ya ( X Ray.) ili tuweze kupata majibu ya kutoka kwa Daktari tujuwe unaumwa kitu gan. tukisha pata hayo majibu ndio tutaweza kukupa ushauri mzuri

Mkuu mzizimkavu, heshima yako. nilitembelea https://www.jamiiforums.com/jf-doctor/106773-vidonda-vya-tumbo-vilivyo-kwenye-kati-utumbo-mkubwa-na-mdogo%5Cduodinal-ulcers.html na kukutana na ushauri wa kapotolo. Nilipiga x ray na kuanza. Nilichomwa sindano 5, omeprazole na metronidazole na paracetamol. Sikupata ahueni, niliporudi rudi hospitalini nilimwomba dk anibadilishie dozi cimetine 1 x 2/10, secnidazole 2x1/3 na amoxilline 2 x 3/5. Dozi ya cimetidine namalizia kesho na to be sincere there are some changes, but let me wait at least 7 days after completion of doze to declare improvement. Karibu
 
wakuu nilifanyia kazi ushauiri wenu na nime edit post yangu kwa kuonesha nilichopata baada ya ushauri wenu. Naomba ushauri wenu baada ya majibu ya vipimo
 
''Mwili wa binadamu unapopungukiwa maji, hutoa ishara (indicators) tumeziita ishara hizo kuwa ni magonjwa, hauumwi una kiu, usiitibu kiu kwa madawa - dr. Batmanghelidj''.

mpaka utakapoupa mwili kile unachokiihitaji ndo utaacha kukuletea ishara hizo!!. hakuna mubadala wa maji. maji ni maji. ndo maana miaka 12 bado unasumbuliwa, ni mpaka hapo utakapoupa mwili kile unachokihitaji. kama utaweza polisi, niambie unywaji wako wa maji kwa siku. tembelea: Utangulizi | maajabu ya maji
 
ni mara chache sana kunywa zaidi ya lita 1.5 kwa siku. mara nyingi ni nusu lita na kushuka chini kwa siku
 
ni mara chache sana kunywa zaidi ya lita 1.5 kwa siku. mara nyingi ni nusu lita na kushuka chini kwa siku

Nashukuru sana kwa kunijibu mkuu. sasa kuanzia leo usinywe kinywaji kingine chochote zaidi ya maji. utarudia kunywa kingine chochote pale utakapokuwa husumbuliwi na ugonjwa wowote. usisubiri kiu ndipo unywe maji, tena usinywe ya maji ya baridi. tafadhari usikimbilie kwenda kunywa maji kibao, taratiiiiiiiiiiiibu, leo glasi moja (ml 250), kesho mbili, keshokutwa tatu, mtondogoo nne.... mpaka ufikie glasi nane kwa siku katika mfululizo ufuatao:

Muda gani unywe maji?:


  • Kitu cha kwanza kufanya mara uamkapo tu, ni kunywa glasi 2 za maji (ml 500) kwakuwa umetumia glasi 2 za maji kwa kulala mpaka asubuhi.
  • Kunywa glasi 1 robo saa au glasi 2 nusu saa kabla ya chakula cha asubuhi, mchana na jioni, kisha hesabu masaa 2 au 2 na nusu kila baada ya chakula cha asubuhi, mchana na jioni bila kunywa wala kula chochote, ndipo unywe glasi 1 ya maji.
  • Kunywa glasi 1 ya maji kila uendapo kulala.
  • Muda wowote uamkapo usiku kwenda bafuni, kunywa nusu glasi ya maji na kipande cha chumvi kisha rudi kulala.
  • Muda wowote unapopatwa na kiu kunywa maji.
Badili pia chumvi, anza kutumia chumvi ya mawe, ukiizidisha kidogo katika chakula usihofu kula tu ni nzuri zaidi. halafu kila baada ya kumaliza kula meza vidonge viwili vya multivitamins(hivi siyo dawa ni lishe), kwanini?, mlo wetu kwa siku unatakiwa uwe asilimia 80 mbogamboga na matunda na asilimia 20 vyakula vingine, lakini sisi hufanya kinyume chake ndiyo maana nakushauri kunywa multivitamini kila baada ya kumaliza kula.

unaweza kunitumia email yako katika 0769779533. tembelea na usome taratibu: Utangulizi | maajabu ya maji
 
asante sana mkuu. nimetembelea hiyo website na nimejifunza mengi mno. Nimechukua namba yako na nitakutumia email yangu
 
Ulishawahi pima HIV, a.k.a damu kubwa? Maana fungus wa kooni wanaendana na aka kaugonjwa japo kuwa sio wakati wote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom