Madaktari kwanini wamtibu Dr Ulimboka wakati wapo kwenye mgomo?

Jimy P Analysis yako ni bomu kabisa. Kama nchi ni maskini kiasi cha kutoweza kuwalipa mishahara hiyo madaktari basi serikali ingekuwa imepunguza matumizi yake ikiwa ni pamoja na mishahara ya vi9ongozi wa serikali kama wabunge, mawaziri na watu wa aina hiyo. Vile vile serikali isingekuwa inatumia pesa hovyo hovyo kama kununua rada isiyofanya kazi. Marekani mshahara wa Senator ($180,000) kwa mwaka ni karibu sawa na huenda ukawa chini ya mshahara wa daktari ambao huanzia $150,000 hadi $400,000 kwa mwaka; Tanzania mshahara wa mbunge ni zaidi ya mara tano ya mshahara wa dakatri, haki iko wapi hapo?

Vipaumbele vibovu vya serikali ndivyo vinavyofanya watu waone kuwa ina pesa lakini haitaki kuwalipa wafanya kazi wake mishahara sahihi.
 
Last edited by a moderator:
Acheni jazbar...mtoa mada yuko sahihi madaktari wameawa na rushwa za kila aina. pampja na ufisadi... Ni Daktari yupi wewe umjuaye hana duka la madawa? Dawa wanazuza madukani mwao zinatoka wapi....majority wanakuwa wamezipora katika hospitali zetu za wananchi......theni ukienda hospital unaambiwa hapa dawa hii hakuna nenda famasi ya fulani pal mjini ndo anauza dawa nzuri...kumbe duka ni la kwao.....wanaJF hawa hamwajui? au hamjawahi kuugua mkaambiwa hayo? kama bado subirini....

Uwe unauliza kwanza we mbuzi, sio kila mvaa koti jeupe mwenye duka la dawa ni daktari, ht bucha ni duka na wauza nyama huvaa makoti meupe!
 
Haya mambo yatatushughulisha sana,,,na naamin tunavosafa na watawala wanahaha hivyohivyo kuja na suluhisho mujarabu
kinachofanyika au kuonekana sasa ni labda labda tu,,,,kiukweli ukimwambia mtu kuwa nchi maskin na hakuna uwezo,basi onesha kwa vitendo kuwa ni kweli nchi maskin,vinginevyo raia wanaweza wasielewe kama nchi maskini(kwa sababu ya matumizi mabaya ya pesa na pia wizi wa pesa unaoendelea),,,
 
mimi nashangaa sana watz wanamuhurumia sana huyu dr.ulimboka mnasahau maelfu ya watz wanaoathirika kutokana na mgomo huu.mm binafsi bora na yeye aonje wanachokipata watz ili iwe fundisho kwa wengine
 
Alafu Jimy P,
Unasema Madaktari wanaiba madawa wanapeleka kwenye Maduka yao. Mimi naomba nikuulize, wakati wanaiba Serikali ipo wapi? Na kwa nini mseme haya wakati wa Migomo tu?
 
Mimi nafikiri hili la madaktari kudai mishahara ya kuanzia Tshs 3.5m kwa kila daktari anayemaliza chuo si sahihi na haliwezi kuwa justified kwa namna yoyote ile. Kama serikali itakubaliana na dai hili hii itafanya wafanyakazi wa fani nyingine nao wadai mishahara yao iongezwe, hivyo kuzua tatizo jingine badala ya katatua. Isitoshe kuwapa madaktari Tshs 3.5m haina maana madaktari wataacha kupokea rushwa, kutibu wagonjwa wa upendeleo/kujuana, na wala haimaanishi kwamba wataongeza ufanisi, kupunguza utoro au kuchelewa kazini. Kwa BOT,TRA,TPA etc kupewa mishahara mikubwa hii haipo kwenye madai yao.

Ila Wabunge kupokea Milioni 10 kwa mwezi ni sawa? Tena Mbunge ambaye hata Logarithim hajui (Livingstone Lusinde)! Unasema pia kwamba kuwapa madaktari Tshs 3.5m haina maana madaktari wataacha kupokea rushwa. Hivi yule Mbunge wa Bahi ndugu Badwel mbona anapokea rushwa licha ya kulipwa hizo 10 Million. Tuache ubinafsi jamani. Kama keki ya Taifa ni ndogo basi kila mtu alipwe kidogo kujustify kweli kwamba hazina yetu imekauka.

TUMBIRI (PhD, University of Hull - UK),
tumbiri@jamiiforums.com
 
Mie nawasikitia sana wagonjwa wote waliorudishwa majumbani kuna jamaa yangu kapoteza Mama yake mzazi siku ya mgomo kafia mapumzika Muhimbili.
 
hao majambazi waliomteka walikosea sana kumwacha hai. halafu kuna watu wanafikiri labda hao walikuwa polisi au usalama wa taifa, au labda walidhamiria kumuua. hivi kweli kama walidhamiria kumuua wangempiga tu, wakati walikua na bunduki si wangemlenga tu kichwani na kumuua mara moja...ukiona walimpiga ujue ilikuwa ni kumpa adabu tu afu arudi uraiani, na yeye kama ana akili akipona afyate mkia, la sivo akiendelea atamalizwa. unaweza kuta ni watu ambao ndugu zao walikufa kwasababu ya yeye kuhamasisha mgomo, au hata kama wangekuwa ni watu wa serikali naamini kuwa hawakuwa na lengo la kumuua, bali kumpa adhabu tu ili ajue hapa tz yeye si kimungu mtu.
 

Ila Wabunge kupokea Milioni 10 kwa mwezi ni sawa? Tena Mbunge ambaye hata Logarithim hajui (Livingstone Lusinde)! Unasema pia kwamba kuwapa madaktari Tshs 3.5m haina maana madaktari wataacha kupokea rushwa. Hivi yule Mbunge wa Bahi ndugu Badwel mbona anapokea rushwa licha ya kulipwa hizo 10 Million. Tuache ubinafsi jamani. Kama keki ya Taifa ni ndogo basi kila mtu alipwe kidogo kujustify kweli kwamba hazina yetu imekauka.

TUMBIRI (PhD, University of Hull - UK),
tumbiri@jamiiforums.com
Nashukuru mkuu kwa kunisaidia kujustify point yangu kwamba kumlipa mtanzania mshahara mkubwa hakumfanyi aache kupokea rushwa. (ref.Baduwel anayepata Tshs 10m na marupurupu kibao ya ubunge lakini bado alipokea/alikamatwa kwa rushwa ya 1m). Kwa maoni yangu Tatizo la watanzania na mishahara ya wafanyakazi kutokutosheleza mahitaji yao ni ufisadi na ubinafsi na hasa kwa viongozi. Kibaya zaidi ni kwamba Raisi naye hana uwezo au hataki kushughulikia suala hilo, matokeo yake uchumi umekufa. Suluhisho ni Raisi akubali ameshindwa Uongozi na ajiuzulu.
 
Acheni jazbar...mtoa mada yuko sahihi madaktari wameawa na rushwa za kila aina. pampja na ufisadi... Ni Daktari yupi wewe umjuaye hana duka la madawa? Dawa wanazuza madukani mwao zinatoka wapi....majority wanakuwa wamezipora katika hospitali zetu za wananchi......theni ukienda hospital unaambiwa hapa dawa hii hakuna nenda famasi ya fulani pal mjini ndo anauza dawa nzuri...kumbe duka ni la kwao.....wanaJF hawa hamwajui? au hamjawahi kuugua mkaambiwa hayo? kama bado subirini....


Baelezeee Baelezeeeeeeee .............. Labda wengine hawajawahi kuugua na kwenda hospitali(au kuwa na mgonjwa hospitali au mke mwenye ujauzito).
 
Mleta mada mimi siungi mgomo ila unadai tanzania ni masikini hapo unatusanifu,uliza ni pesa ngapi wameficha uswis,sisi ilikuwa tuwe tunatoa misaada kwa vinchi vidogo kama somali na sio kuomba ila wewe na hao magamba ndio mmetufikisha hapa ,na hizo pesa wanataka kukodi madaktari wamezitoa wapi
 
Mi napendekeza kwenye katiba mpya viongozi hakuna kutibiwa nje ya nchi ,watibiwe hapa bongo kama sisi tusiokuwa na kitu na akilazimisha aende kwa gharama zake
 
Mdaktari wanahitaji Mshahara wa Milioni 3.5, Katika nchi Maskini ni Vigumu kulipwa mshahara huu, Nadhani wafanye Analysis kama inawezekana kwani kwa sasa anayetoka Chuoni analipwa Kuanzia Laki Tisa, Na Serikali imewaongezea Posho walizokuwa wanahitaji isipokuwa la kulipwa mshahara huo na nadhani imefika wakati kama unaona kazi unayofanya hailipi badilisha kazi au usisomee kitu ambacho halilipi, nawashauri wote wanaosoma Udaktari na Wanaotarajia kusomea kama unadhani hailipi au Ukimaliza Chuo lazima uajiriwe na Serikali usisome au acha unachosome somea kitu kingine,

Nadhani imefika wakati tujue kuwa Professional nyingine ni muhimu pia kama wanavyodhani Madaktari wao ni muhimu zaidi halafu Board ya mikopo inatoa asimilimi 100% kwa wanafunzi wanaosomea Udaktari hizi ni Kodi za Watanzania ambazo lazima muwatumikie,

Idara ya afya ni miongoni mwa idara zinazooongoza kwa Rushwa Tanzania,

Madakri wamegoma kuwatibu Watanzania lakini Dr Ulimboka kafika wameacha Mgomo wameenda kumshughulikia wanaacha watanzania wanaendelea kufa

Madaktari mnachelewa ofisini, mnapokea Rushwa haya yote hamsemi mtayerekebisha vipi,

Umefika wakati Serikali kutumia Sheria za Utumishi la sivyo itafika sehemu Watumishi wote wa Serikali wahitaji Milion 3.5

Viongozi wenye dhamana fanyeni maamuzi magumu whether is wrong or Right,
Mhe EL Alishawahi kusema Msiogope kufanya Maamuzi whether is wrong or Right.

Mhe Waziri mkuu kila kitu lazima mseme Top Leaders kwani huko mikoani hakuna viongozi au Wilayani.
Watekeleze wajibu wao na Fanya Maamuzi kama kiongozi Mkuu wa serikali lazima mbadilike ili nchi iende.
Hao wanaotaka kushika nchi watanzania wanafikiri hawatacheka na mtu anayekwenda kinyume na Sheria Na taratibu za Kazi na ndivyo itakuwa hivyo
Hivi unafikiri kwa kutumia makalio au ubongo?una maana gani kusema nchi maskini?bilioni 64 sherehe za miaka 50 bila maji,wanafunzi wanakaa chini,reli mbovu,ndege moja tu yaani tunazidiwa hata na RWANDA,NCHI YENYE UKUBWA SAWA NA UBUNGO?NA INAONEKANA UNA UFINYU WA KUFIKIRI YAANI UNAJUA MADKTARI WANAGOMEA POSHO TU!KUKOSA VPIMO KWENYE HOSPITALI KAMA TEMEKE,SEKOU TOURE NA NYINGINE NYINGI HUONI?YAANI MKOA KAMA WA TANGA UNAKOSA X-RAY,HILO HUONI,MWISHO WENU UMEFIKA,ENDELEENI KUTUMIA MAKALIO KUFIKIRI,KWANI MTU ANAYEFILISIKA HAJUI KUWA ANAFILISIKA,MUNGU MBARIKI KAKA ULIMBOKA APONE,LA SIVYO TUPO TAYARI KUMWAGA DAMU JAPO HATUPENDI,INAUMA SANA,MATESO ALIYOPATA HAYAELEZEKI.
 
Mdaktari wanahitaji Mshahara wa Milioni 3.5, Katika nchi Maskini ni Vigumu kulipwa mshahara huu, Nadhani wafanye Analysis kama inawezekana kwani kwa sasa anayetoka Chuoni analipwa Kuanzia Laki Tisa, Na Serikali imewaongezea Posho walizokuwa wanahitaji isipokuwa la kulipwa mshahara huo na nadhani imefika wakati kama unaona kazi unayofanya hailipi badilisha kazi au usisomee kitu ambacho halilipi, nawashauri wote wanaosoma Udaktari na Wanaotarajia kusomea kama unadhani hailipi au Ukimaliza Chuo lazima uajiriwe na Serikali usisome au acha unachosome somea kitu kingine,

Nadhani imefika wakati tujue kuwa Professional nyingine ni muhimu pia kama wanavyodhani Madaktari wao ni muhimu zaidi halafu Board ya mikopo inatoa asimilimi 100% kwa wanafunzi wanaosomea Udaktari hizi ni Kodi za Watanzania ambazo lazima muwatumikie,

Idara ya afya ni miongoni mwa idara zinazooongoza kwa Rushwa Tanzania,

Madakri wamegoma kuwatibu Watanzania lakini Dr Ulimboka kafika wameacha Mgomo wameenda kumshughulikia wanaacha watanzania wanaendelea kufa

Madaktari mnachelewa ofisini, mnapokea Rushwa haya yote hamsemi mtayerekebisha vipi,

Umefika wakati Serikali kutumia Sheria za Utumishi la sivyo itafika sehemu Watumishi wote wa Serikali wahitaji Milion 3.5

Viongozi wenye dhamana fanyeni maamuzi magumu whether is wrong or Right,
Mhe EL Alishawahi kusema Msiogope kufanya Maamuzi whether is wrong or Right.

Mhe Waziri mkuu kila kitu lazima mseme Top Leaders kwani huko mikoani hakuna viongozi au Wilayani.
Watekeleze wajibu wao na Fanya Maamuzi kama kiongozi Mkuu wa serikali lazima mbadilike ili nchi iende.
Hao wanaotaka kushika nchi watanzania wanafikiri hawatacheka na mtu anayekwenda kinyume na Sheria Na taratibu za Kazi na ndivyo itakuwa hivyo

Jamani masaburi yana kazi kwa watu wanaoyatumia kufikiri lol!
 
Sasa huko alikopelekwa Dr. Ulimboko akikuta madakitari wa huko nao wamegoma itakuwaje
 
Back
Top Bottom