Vancomycin
Senior Member
- Jan 7, 2011
- 171
- 111
Heshima kwenu wanaJF,
Wakuu kama mtakumbuka wakati mwenyekiti wa jumuia ya kuratibu mgomo wa madaktari Dr.Ulimboka alivyotangaza kwenye taarifa yake ikumbukwe alisema mgomo UMEAHIRISHWA na wala HAUJASITISHWA na kutoa nafasi kwa serikali kushugulikia madai ya madaktari ambayo yalikubaliwa na serikali na yasingeweza kupatiwa ufumbuzi kwa wakati ule kwa haraka hivyo serikali iliomba wiki mbili.Kama ambavyo taarifa ile ilivyotanabaisha kuwa kikao cha kutathmini utekelezaji wa msingi wa maridhiano yaliyofikiwa kitafanyika tarehe 3/3/2012.
Taarifa za uhakika zilizonifikia mkutano wa madaktari wote utanyika kesho kama ilivyotangazwa hapo awali kuanzia saa tatu asubuhi katika ukumbi wa WATERS FRONT jijini Dar es Salaam.
Pamoja na taarifa hizo madaktari wengi wanaonyesha kutokuridhishwa na utekelezaji wa madai yao kwa wakati kama ambavyo walivyoombwa na serikali kuwa ndani ya wiki mbili wangekuwa wamemaliza zoezi zima la kutanabaisha nini serikali itafanya juu ya madai hayo.Wengi wakionyeshwa kukerwa na serikali kutowafuta kazi ya uwaziri, waziri wa Afya na Naibu wake ambao mpaka sasa bado wako ofisini.
Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinazidi kupasha kuwa maamuzi magumu yanaweza kufikiwa kwa mgomo ambao uliahirishwa sasa unaweza kuendelea kuanzia jumatatu.
Zaidi wamekerwa na taarifa juu ya madaktari iliyotolewa jana na TBC iliyokuwa kipropaganda ili kuwagawa na kada nyingine na kuonyesha kuwa madaktari hawataki kwa makusudi kufikia maridhiano ya mwisho.
Habari zitatolewa zaidi kadri itakavyowezekana kutoka kwenye chanzo changu huko Dar es Salaam.
UPDATES
Gazeti la Mwananchi leo tarehe 03/03/2012 inapasha kuwa
Wakuu kama mtakumbuka wakati mwenyekiti wa jumuia ya kuratibu mgomo wa madaktari Dr.Ulimboka alivyotangaza kwenye taarifa yake ikumbukwe alisema mgomo UMEAHIRISHWA na wala HAUJASITISHWA na kutoa nafasi kwa serikali kushugulikia madai ya madaktari ambayo yalikubaliwa na serikali na yasingeweza kupatiwa ufumbuzi kwa wakati ule kwa haraka hivyo serikali iliomba wiki mbili.Kama ambavyo taarifa ile ilivyotanabaisha kuwa kikao cha kutathmini utekelezaji wa msingi wa maridhiano yaliyofikiwa kitafanyika tarehe 3/3/2012.
Taarifa za uhakika zilizonifikia mkutano wa madaktari wote utanyika kesho kama ilivyotangazwa hapo awali kuanzia saa tatu asubuhi katika ukumbi wa WATERS FRONT jijini Dar es Salaam.
Pamoja na taarifa hizo madaktari wengi wanaonyesha kutokuridhishwa na utekelezaji wa madai yao kwa wakati kama ambavyo walivyoombwa na serikali kuwa ndani ya wiki mbili wangekuwa wamemaliza zoezi zima la kutanabaisha nini serikali itafanya juu ya madai hayo.Wengi wakionyeshwa kukerwa na serikali kutowafuta kazi ya uwaziri, waziri wa Afya na Naibu wake ambao mpaka sasa bado wako ofisini.
Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinazidi kupasha kuwa maamuzi magumu yanaweza kufikiwa kwa mgomo ambao uliahirishwa sasa unaweza kuendelea kuanzia jumatatu.
Zaidi wamekerwa na taarifa juu ya madaktari iliyotolewa jana na TBC iliyokuwa kipropaganda ili kuwagawa na kada nyingine na kuonyesha kuwa madaktari hawataki kwa makusudi kufikia maridhiano ya mwisho.
Habari zitatolewa zaidi kadri itakavyowezekana kutoka kwenye chanzo changu huko Dar es Salaam.
UPDATES
Gazeti la Mwananchi leo tarehe 03/03/2012 inapasha kuwa
Ofisi ya Waziri Mkuu ilieleza kuwa moja ya sababu za kuvunjika kwa kikao hicho ni madaktari kupinga hoja ya kuhusisha makundi mengine kutoka sekta ya afya kama wafamasia na wauguzi.
Lakini Rais wa chama cha Madaktari Tanzania (MAT) Dk Namala Mkopi aliliambia Mwananchi kuwa wao walikwenda katika ofisi za Waziri Mkuu kufuata majibu ya barua yao waliyoiwasilisha kabla ya mkutano, lakini hawakupewa barua ya majibu.
Alisema barua hiyo pamoja na mambo mengine ilikuwa na maswali kadhaa yanayotaka ofisi hiyo ijibu huku ikieleza namna wao wanavyotaka mkutano wa majadiliano baina yao na Serikali uwe.
"Sisi hatukwenda kukutana kwa ajili ya majadiliano na wahusika bali tulifuata majibu ya barua yetu tuliyowasilisha kwao kabla ya mkutano huo, taarifa ya kuwa sisi tulitoka kwenye mkutano kutokana na kukataa makundi mengine ni za uongo na wameamua kufanya propaganda katika hilo, lakini sisi ni watu wazima tunaelewa.
"Acha wao wafanye propaganda, sisi ni watu wazima tunajua itafika wakati tutakaa nao chini na kufanya uamuzi wenye kuzingatia masilahi yetu na ya umma," alisema Mkopi.