Vancomycin
Senior Member
- Jan 7, 2011
- 171
- 111
Kwa taarifa zilizonifikia pamoja na taarifa ya habari ya STAR TV jioni hii chama cha madaktari kanda ya ziwa MAT LAKE ZONE leo walikuwa na mkutano kuanzia saa sita mchana ambapo baada ya mkutano huo wameungana na wenzao wa Muhimbili na nchini kote kupinga hatua ya wizara ya afya kupuuza madai yao na kuazimia kusimama kwa pamoja kutetea taaluma yao ambayo sasa imepuuzwa kiasi cha madaktari kugeuzwa waandika rufaa za mabwana wakubwa kwenda kutibiwa INDIA wakifuata sophisticated diagnostc and therapeutic machines ambazo hawanunua zihudumie watanzania wote.
Wamelalamikia upotoshwaji wa kuwaita INTERNS wanafunzi wakati nimadaktari walio-graduate na kula kiapo cha udaktari na INTERN ni muda wa kujiongezea uzoefu zaidi.Akiongea kwa hasira rafiki aliyenipa taarifa hizi amesisitiza hawatarudi nyuma.
Wameazimia kusubiri mazungumzo na waziri mkuu na muafaka usipofikiwa wataweka vifaa chini
UPDATES
Katika ukurasa wa facebook Dr.Hamis Kigwangala ameandika
Wamelalamikia upotoshwaji wa kuwaita INTERNS wanafunzi wakati nimadaktari walio-graduate na kula kiapo cha udaktari na INTERN ni muda wa kujiongezea uzoefu zaidi.Akiongea kwa hasira rafiki aliyenipa taarifa hizi amesisitiza hawatarudi nyuma.
Wameazimia kusubiri mazungumzo na waziri mkuu na muafaka usipofikiwa wataweka vifaa chini
UPDATES
Katika ukurasa wa facebook Dr.Hamis Kigwangala ameandika
Naibu Waziri, Wizara ya Afya, Dr. Lucy Nkya (MB) naye avuliwa uanachama kwa kipindi cha mwaka mmoja kama mwenzake Daktari Mkuu wa Serikali, Dr. Deo Mtasiwa, kwa kosa lile lile la kusaliti fani ya udaktari na lile la kuvunja miiko na maadili ya udaktari kama yanavyosomeka kwenye kiapo cha udaktari, kwamba kila daktari atawatambua na kuwathamini madaktari wenzake kama ndugu zako na kuwatendea wema, kuwapenda na kuwaheshimu. Chama cha Madaktari Tanzania kitawafikiria kwenye Mkutano ujao wa kawaida. Hii maana yake nini? Wamepoteza sifa ya kuwa medical 'professionals!' Wamebaki kuwa wataalam wa Udaktari tu!
Akaandika tena hivi
Hivi ni nini chanzo cha kiburi na madharau ya watendaji wa serikali? Maana hata kura hawakumwombea Rais, sasa kwa nini wanakosa heshima kwa wapiga kura wetu kiasi hiki? Viongozi wa CCM wanasubiri nini kuilazimisha Wizara itoe majibu kwa madaktari? Hivi mpaka wagome ndiyo watasikilizwa kweli? Sasa tayari Bugando, KCMC wameishashika kasi, hawa Wizara ya AFya wanatoa wapi kiburi cha kutowasikiliza askari wao? Wanataka watu wafe ndiyo waje wawasikilize?