MADAI YA SERUKAMBA, SITA NA MWAKYEMBE WANAIHUJUMU CCM IPI?
Mbunge wa kigoma mjini, peter serukamba, amekaririwa na gazeti la mtanzania la leo linalomilikiwa na mbunge wa igunga, akiwalumu spika sita na mwakyembe kuwa wanakihujumu chama cha mapinduzi yaani ccm, kwa mujibu wa habari hiyo iliyochapishwa katika kurasa wa mbele wa gazeti hilo, serukamba anarusha madongo zaidi kwa spika na mwaKyembe kwa kuwaonya kuwa si wabunge pekee wenye akili nchini. Yeye anadhani kuwa kitendo cha spika na mwakyembe kutoa maoni yao kuishauri serikali iachane nna mitambo kukuu ya dowans ni kuihujumu ccm.
Sisi ambao siku zote tunakereketwa zaidi na utaifa wetu kuliko ufurukutwa au ukereketwa wa chama chochote cha siasa, tuna kila sababu ya kujiuliza maswali mengi kuhusu matamshi ya mheshimiwa huyu .
Tunajiuliza kwa kukataa kukubaliana na hoja ya kununua mitambo kukuu yenye harufu ya ufisadi, na kwamba kwa kuinunua mitambo hiyo ingekuwa kinyume cha sheria ya manunuzi ambayo serukamba kama mbunge alishiriki kuitunga, akina sita na mwakyembe wanaihujumu ccm ipi?
Kwamba spika sita na mwakyembe wamekuwa mstari wa mbele kukemea ufisadi katika bunge letu kwa ukereketwa wa taifa letu na kwa ajili ya wananchi wake ambao wako kwenye lindi zito la umaskini tofauti na serukamba na wateule wachache , akina sita wanaihujumu ccm ipi?
Kwamba inafahamika wazi kuwa hata mmiliki wa dowans ni ghost, yaani mtu asiyejulikana , na kuwa mtu huyu asiyejulikana amefungua mashtaka dhidi ya tanesco, na hao hao tanesco wanataka kununua mitambo hiyo ya mmiliki asiyejulikana , je wanaopinga hili wanaihujumu ccm ipi?
Ni wazi kuwa ccm anayozungumzia serukamba si hii tunaoifahamu, yaani kile chama kilichoanzishwa kwa kuunganisa vyama vya ASP, NA TANU vyama vilivyokikomboa nchi hii. Hivyo ccm chama kilichojijengea umaarufu kwa kuongozwa na watu kama akina marehemu sokoine na nyerere ambao walifanya kazi usiku na mchana kumkomboa mwananchi bila hila wala ufisadi, ningetaka serukamba anipe jibu, je ni ccm hii anayosema inahujumiwa au ni ingine?
Hivi serukamba angetaka mwakyembe na sita, pamoja na sisi wengine tunyamaze wakati kundi la watu wachache kama yeye na wengine wasiozidi ishirini wakiendelea kuikomba asali ya taifa? Yaani tunyamaze wakati wao kupitia kagoda, wakiendelea kukomba hazina ya nchi pale benki kuu,hadi imalizike. ? tunyamaze wakati vijana wetu wakishindwa kuendelea na elimu ya chuo kikuu licha ya kufaulu kwa kukosa ada, wakati serukamba akiwashangilia na kuwalinda mafisadi?
Ni wazi na nakutaka serukamba unielewe kuwa wewe ni kibaraka wa kikundi cha watu wachache wanaoijiita ccm ambao ni majambazi wa rasilimali za taifa letu, wewe serukamba unaonekana kufaidi kwa ujangili huo wa mali zataifa letu. Kwa kuwa wewe ndiwe msemaji wa washenzi hawa. Au kwa namna au lugha sahihi wewe ni kibaraka namba wani wa wezi wa Richmond, deep green, epa, dowans, nk.
Kwa hiyo mheshiwa serukamba, ni kweli kuwa sita na mwakyembe na wengine tunaolipenda taifa letu, tunaihujumu ccm ile unaoijua wewe yaani chama chama mafisadi na Wala siyo ile ccm ilyoasisisiwa na mwalimu nyerere.
Huu ni wakati muafaka kwako na vibaraka wenzako muamue kumtambua mama yenu ambaye ni taifa la Tanzania, na kusahau kushujudia majangili na wezi wa rasilimali za taifa. Kama bado hujatambua hili umechelewa sana, na huna nafasi tena kwa kuwa mapambano yameanza na kamwe hatutshindwa damu ikiwa bado inazunguka katika mishipa yetu ya damu
ALUTA CONTINUA
MWIKIMBI M. MWITORI
Mbunge wa kigoma mjini, peter serukamba, amekaririwa na gazeti la mtanzania la leo linalomilikiwa na mbunge wa igunga, akiwalumu spika sita na mwakyembe kuwa wanakihujumu chama cha mapinduzi yaani ccm, kwa mujibu wa habari hiyo iliyochapishwa katika kurasa wa mbele wa gazeti hilo, serukamba anarusha madongo zaidi kwa spika na mwaKyembe kwa kuwaonya kuwa si wabunge pekee wenye akili nchini. Yeye anadhani kuwa kitendo cha spika na mwakyembe kutoa maoni yao kuishauri serikali iachane nna mitambo kukuu ya dowans ni kuihujumu ccm.
Sisi ambao siku zote tunakereketwa zaidi na utaifa wetu kuliko ufurukutwa au ukereketwa wa chama chochote cha siasa, tuna kila sababu ya kujiuliza maswali mengi kuhusu matamshi ya mheshimiwa huyu .
Tunajiuliza kwa kukataa kukubaliana na hoja ya kununua mitambo kukuu yenye harufu ya ufisadi, na kwamba kwa kuinunua mitambo hiyo ingekuwa kinyume cha sheria ya manunuzi ambayo serukamba kama mbunge alishiriki kuitunga, akina sita na mwakyembe wanaihujumu ccm ipi?
Kwamba spika sita na mwakyembe wamekuwa mstari wa mbele kukemea ufisadi katika bunge letu kwa ukereketwa wa taifa letu na kwa ajili ya wananchi wake ambao wako kwenye lindi zito la umaskini tofauti na serukamba na wateule wachache , akina sita wanaihujumu ccm ipi?
Kwamba inafahamika wazi kuwa hata mmiliki wa dowans ni ghost, yaani mtu asiyejulikana , na kuwa mtu huyu asiyejulikana amefungua mashtaka dhidi ya tanesco, na hao hao tanesco wanataka kununua mitambo hiyo ya mmiliki asiyejulikana , je wanaopinga hili wanaihujumu ccm ipi?
Ni wazi kuwa ccm anayozungumzia serukamba si hii tunaoifahamu, yaani kile chama kilichoanzishwa kwa kuunganisa vyama vya ASP, NA TANU vyama vilivyokikomboa nchi hii. Hivyo ccm chama kilichojijengea umaarufu kwa kuongozwa na watu kama akina marehemu sokoine na nyerere ambao walifanya kazi usiku na mchana kumkomboa mwananchi bila hila wala ufisadi, ningetaka serukamba anipe jibu, je ni ccm hii anayosema inahujumiwa au ni ingine?
Hivi serukamba angetaka mwakyembe na sita, pamoja na sisi wengine tunyamaze wakati kundi la watu wachache kama yeye na wengine wasiozidi ishirini wakiendelea kuikomba asali ya taifa? Yaani tunyamaze wakati wao kupitia kagoda, wakiendelea kukomba hazina ya nchi pale benki kuu,hadi imalizike. ? tunyamaze wakati vijana wetu wakishindwa kuendelea na elimu ya chuo kikuu licha ya kufaulu kwa kukosa ada, wakati serukamba akiwashangilia na kuwalinda mafisadi?
Ni wazi na nakutaka serukamba unielewe kuwa wewe ni kibaraka wa kikundi cha watu wachache wanaoijiita ccm ambao ni majambazi wa rasilimali za taifa letu, wewe serukamba unaonekana kufaidi kwa ujangili huo wa mali zataifa letu. Kwa kuwa wewe ndiwe msemaji wa washenzi hawa. Au kwa namna au lugha sahihi wewe ni kibaraka namba wani wa wezi wa Richmond, deep green, epa, dowans, nk.
Kwa hiyo mheshiwa serukamba, ni kweli kuwa sita na mwakyembe na wengine tunaolipenda taifa letu, tunaihujumu ccm ile unaoijua wewe yaani chama chama mafisadi na Wala siyo ile ccm ilyoasisisiwa na mwalimu nyerere.
Huu ni wakati muafaka kwako na vibaraka wenzako muamue kumtambua mama yenu ambaye ni taifa la Tanzania, na kusahau kushujudia majangili na wezi wa rasilimali za taifa. Kama bado hujatambua hili umechelewa sana, na huna nafasi tena kwa kuwa mapambano yameanza na kamwe hatutshindwa damu ikiwa bado inazunguka katika mishipa yetu ya damu
ALUTA CONTINUA
MWIKIMBI M. MWITORI