Madai ya Prof Lipumba kuwa alikuwa UN akishauri Uchumi ni changa la macho?

wadau mimi nimejaribu ku-google madai kuwa prof alikuwa akishauri mambo ya uchumi kwa kutumwa na UN sioni kitu
nimepata haya
Prof.Ibrahim Lipumba/UN - Google Search

hivi siyo danganya toto na kutafuta umaarufu kwa kisiasa.

ebu wenye japo link,inayoonesha hivyo atuwekee ili tuamini,maana wengine ni THOMASO

nitashukuru

Safari yake nchini Marekani
Akizungumzia safari yake ya Washington nchini Marekani, ambayo alikaa huko kwa takriban miezi mitano, alikokwenda kwa ajili ya kufanya utafiti kuhusu demokrasia na maendeleo, utafiti ambao ulilenga kuleta demokrasia itakayoleta maendeleo na ajira katika nchi za Afrika, alisema katika utafiti alipata nafasi ya kutoa mjadala kuhusu miaka 50 ya Uhuru Tanzania na hatua ya maendeleo ambayo nchi imeifikia.
Kwa mujibu wa profesa huyo, miaka 200 ndiyo miaka ya maendeleo ya kisiasa, lakini cha kushangaza sasa hivi nchi iko katika robo ya miaka hiyo 200 ya maendeleo lakini asilimia 70 ya wananchi wake wanatumia chini ya dola moja huku mkazi wa Dar es Salaam ambaye anahesabiwa ndiye tajiri ana uwezo wa kupata sh 650 kwa siku.
Alisema suala la kuendelea uchumi na demokrasia linaenda pamoja hii ikiwa ni pamoja na wananchi kupata fursa ya kuikosoa serikali, kuchagua viongozi wanaowataka na kuwawajibisha.
Mapendekezo yaliyofikiwa katika utafiti huo wa uchumi duniani, Profesa Lipumba alisema aliona kuna haja ya kuwa na asasi muhimu zitakazowezesha uhuru wa wananchi kujieleza na kuikosoa serikali.
Pia mapendekezo mengine ni kuwepo kwa Tume Huru ya Uchaguzi na asasi huru ya kupambana na rushwa kwa kuwa Takukuru haina uwezo ikizingatiwa kwamba haiwezi kumpeleka mtuhumiwa wa rushwa mahakamani mpaka Mkurugenzi wa Mashtaka ya Jinai atie saini jambo linalorudisha nyuma juhudi za kupambana na rushwa.
Vilevile utafiti huo ulitaka kuwepo kwa asasi huru ya kukusanya fedha itakayofanya kazi kwa uwezo na uwazi zaidi na kuwa na matumizi mazuri ya fedha zitakazopatikana katika makusanyo hayo.
“Katika hili wananchi wa Tanzania wanaweza kufunguliwa kila mmoja akaunti yake bila kujali ni mtoto au mkubwa ambapo rasilimali zote kama gesi, mafuta na madini kiasi cha mapato yake kinagawiwa kwa kuweka katika kila akaunti ya mwananchi na makato ya kodi yanatolewa humohumo hali itakayofanya kila Mtanzania kufaidika na rasilimali zilizopo badala ya sasa hivi rasilimali hizo kufaidiwa na wachache.
 
Jamani, sijui ni uvivu ama kukosa kumbukumbu lakini ngojeni niwasaidie, naona kuna kuchanganya mambo na bila tahadhari mtatoana macho bure!
Mwaka 2007, Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa chama cha CUF aliwahi kuteuliwa na Umoja wa Mataifa kujiunga na jopo la wataalamu kuandaa mikakati ambayo ingeziwezesha nchi masikini duniani kufikia malengo ya milenia ifikapo mwaka 2015. Jopo hilo la wataalamu lilifanya shughuli hiyo katika nchi ya Uswisi na Switzerland kwa miezi minne kuanzia mwezi wa Septemba hadi December mwaka 2007. Prof. Lipumba aliondoka kuelekea nchi hizo September 3, 2007 na alirejea nchini Decemba 31, 2007.
Safari ya Prof. Lipumba juzi Marekani haihusiani na taasisi yoyote ya UN wala uchumi ila alikaribishwa na NED (National Endowment for Democracy) kwenda kutoa mada kuhusu mambo ya siasa na hakuwa mwenyekiti wa kundi lolote lile. Hayo mapokezi aliyopewa ni mkakati wa CUF kutafuta dawa ya kujiongezea uhai baada ya kuchungulia kaburi kwa kumtumia huyo msomi, period!
Thanks man,
You have cleared the air around here!
 
wadau mimi nimejaribu ku-google madai kuwa prof alikuwa akishauri mambo ya uchumi kwa kutumwa na UN sioni kitu
nimepata haya
Prof.Ibrahim Lipumba/UN - Google Search

hivi siyo danganya toto na kutafuta umaarufu kwa kisiasa.

ebu wenye japo link,inayoonesha hivyo atuwekee ili tuamini,maana wengine ni THOMASO

nitashukuru

Safari yake nchini Marekani
Akizungumzia safari yake ya Washington nchini Marekani, ambayo alikaa huko kwa takriban miezi mitano, alikokwenda kwa ajili ya kufanya utafiti kuhusu demokrasia na maendeleo, utafiti ambao ulilenga kuleta demokrasia itakayoleta maendeleo na ajira katika nchi za Afrika, alisema katika utafiti alipata nafasi ya kutoa mjadala kuhusu miaka 50 ya Uhuru Tanzania na hatua ya maendeleo ambayo nchi imeifikia.
Kwa mujibu wa profesa huyo, miaka 200 ndiyo miaka ya maendeleo ya kisiasa, lakini cha kushangaza sasa hivi nchi iko katika robo ya miaka hiyo 200 ya maendeleo lakini asilimia 70 ya wananchi wake wanatumia chini ya dola moja huku mkazi wa Dar es Salaam ambaye anahesabiwa ndiye tajiri ana uwezo wa kupata sh 650 kwa siku.
Alisema suala la kuendelea uchumi na demokrasia linaenda pamoja hii ikiwa ni pamoja na wananchi kupata fursa ya kuikosoa serikali, kuchagua viongozi wanaowataka na kuwawajibisha.
Mapendekezo yaliyofikiwa katika utafiti huo wa uchumi duniani, Profesa Lipumba alisema aliona kuna haja ya kuwa na asasi muhimu zitakazowezesha uhuru wa wananchi kujieleza na kuikosoa serikali.
Pia mapendekezo mengine ni kuwepo kwa Tume Huru ya Uchaguzi na asasi huru ya kupambana na rushwa kwa kuwa Takukuru haina uwezo ikizingatiwa kwamba haiwezi kumpeleka mtuhumiwa wa rushwa mahakamani mpaka Mkurugenzi wa Mashtaka ya Jinai atie saini jambo linalorudisha nyuma juhudi za kupambana na rushwa.
Vilevile utafiti huo ulitaka kuwepo kwa asasi huru ya kukusanya fedha itakayofanya kazi kwa uwezo na uwazi zaidi na kuwa na matumizi mazuri ya fedha zitakazopatikana katika makusanyo hayo.
“Katika hili wananchi wa Tanzania wanaweza kufunguliwa kila mmoja akaunti yake bila kujali ni mtoto au mkubwa ambapo rasilimali zote kama gesi, mafuta na madini kiasi cha mapato yake kinagawiwa kwa kuweka katika kila akaunti ya mwananchi na makato ya kodi yanatolewa humohumo hali itakayofanya kila Mtanzania kufaidika na rasilimali zilizopo badala ya sasa hivi rasilimali hizo kufaidiwa na wachache.
 
Ndugu zangu hebu angalieni kwenye mtandao, Lipimba alikua kwenye 5 months za Reagan-Fascell Democracy Fellowship program ya National Endowment for Democracy, a very prestigious program inayopeleka watu serious, kila mwaka watu wana apply on merit, program hii haina uhusiano wowote na uchumi, na ndiko kunakoandikwa journal maarufu ya political science ya journal of democracy. Huko recipient wanapata muda wa ku research na kuandika juu ya topic wanayochagua, Prof, sio mtanzania wa kwanza kuwa awarded hiyo fellowship, fellows wengine kama sikosei ni pamoja na Dr Bernadeta Kilian, dean wa IJMC ambaye anaonekana kwenye mtandao kuwa aliandika juu ya the political situation ya Zanzibar, na Rosemary Mwakitwange anayeonekana kuandika juu ya Business of Journalism. Nachofahamu ni kwamba akiwa huko prof, alichaguliwa ama kuteuliwa kwenye kazi fulani ya UN linalohusu uchumi, sikumbuki exactly, lakini pamoja na ukweli kuwa ni kichwa cha kujivunia, lakini waandishi hapa wanachanganya facts. Naomba mwenye cha ziada aweke hapa, nakubaliana pia na wengi humu ndani kuwa prof ni hazina kwetu, tusimchafue wala kumlinganisha, mungu anatoa talanta kwa kila mmoja kwa namna yake

Hili neno!
Inashangaza watu wanashabikia kama mpira wa simba na yanga - dini inatawala kama kawaida.
Wanalumbana sijui ni juu ya nini!
 
Inaonekana wewe IT yako ndogo sana, acha kabisa kujiita C programming...Nenda kasome kasome jinsi search engine inavyofanya kazi utapata jibu lako.chochote kilichowekwa kwenye website lazima google ikupe majibu labda kama hujui kusearch

Wewe ndio IT yako ndogo. Chochote kinachopatikana kwenye website kwa kutumia AJAX search engine haiwezi kukipata.
 
Kwani wale wanaoshabikia na "kushangaa" Prof kwenda kutoa ushauri wao wameelewa nini?
Hizo assignments ni vitu vya kawaida kwa mtu mwenye "profession na experiences". Hebu tusijifanye "washamba" sana
kushangazwa na Prof kwenda kutoa ujuzi wake popote alipoenda.Hata wewe waweza kama unazo sifa na pia kama unajibidisha kuonyesha unachoweza kufanya.


BTW -Watanzania tutachekwa sana jinsi tulivyopokea kitendo cha Prof kurudi na mapokezi makubwa utadhani katoka vitani kumbe ni kitu cha kawaida na wako wengi wanaoenda na kufanya kilichowapeleka na kurudi kimya kimya.Hayo maandamano makubwa na shamrashamra yalikuwa na nini?

chuki na roho mbaya imekutawala hata baba yako kama niyuhai akienda ulaya nakukaa muda utakwenda kumpokea kwakua lipumba ni maarufu na anaheshimika na kupendwa watanzania wamejitokeza kumpokea kaliaga na roho mbaya
 
KIMSINGI HUTAKI KUULIZA,DUNIA YOTE INAJUA KUWA ALIKUWA MAREKANI AKIWA KAMA MWENYEKITI WA MAPROFESA DUNIANI AKIJADILI DEPRESSION YA DUNIA.HOWEVER SISI TUMEKUWA NA DHANA POTOFU YA USHABIKI WA KINAZI HATA KWA MAMBO YA MSINGI.MI NADHANI PENYE UKWELI TUWE WEPESI KUKUBALI.KWA USHAURI WA BURE JARIBU KUTAFUTA KWENYE GOOGLE ANDIKA PROFESSOR IBRAHIM HAROUN LIPUMBA.:bump2::bump2:

ujinga umekutawala sana nauvivu google imekutepetesha. Pasingekuwapo google.?
 
Huwezi kuona harakati zake. Degree hazipatikani MADRASA ndugu yangu. Ukiwa na umri zaidi ya miaka 16 na umesoma angalau ukafika std 7 huwezi kusema huoni mchango wa Dr.Slaa katika maendeleo ya demokrasia ya nchi na vita dhidi ya ufisadi.

Huu udini kauletaje? Labda ungenisaidia kujua namna alivyoleta udini.

Ukiwa dhaifu siku zote utawaona watu wa upande wa pili kama threat kwako hata kama ni resource. Shida yako ni kuwahofia wakristo kwa kujua kwako huna maarifa dhidi yao. Stop being pathetic dear boy, bado unaweza kujibidiisha katika yaliyo ya maana kuisaidia jamii yako badala ya kuandaa manung'uniko kila kukicha.

punguani we slaa ana harakati gani zamaana kama ni mtoto ulie zaliwa 1993 ndo unaweza sema. Ufisadi wa epa yote unaiona kama slaa aliibua lipumba kaanza kuisema muda mrefu wakati cuf iko ktk peak 2000-2005. Majukwaani. Hakuna jipya aliloleta slaa. Ni mganga njaa tu huyo anategemea ukatibu kuendesha maisha. Na hayo unayoona sasa nimatunda ya cuf. Kufa kwa watanzania zaidi ya 21 mwaka 2001 damu ilimwagika ulikuwa huwezi fanya shughuli za kisiasa baada ya uchaguzi ndomana mpaka leo cuf ikitakufanya maandamano huwazuii mfano wahayo mapokezi yanakuthibitishia cuf is very power full tunavyoendelea mpaka 2015 utalithibitisha hilo nyota njema huanza kuonekana mapema mapokezi hayajawahi tokea hapa tanzania we acha. Ila wakipokelewa kina zitto, slaa, nape huko mikoani wakitoka tu hapa dsm ni haki yao wala wanaowapokea siwajinga ila wanao mpokea lipumba ni wajinga na mateja. Acheni uhamnazo
 
chuki na roho mbaya imekutawala hata baba yako kama niyuhai akienda ulaya nakukaa muda utakwenda kumpokea kwakua lipumba ni maarufu na anaheshimika na kupendwa watanzania wamejitokeza kumpokea kaliaga na roho mbaya
Hebu nisaidie hapo kwenye RED kutokana na kupendwa huko kwa Lipumba na Watanzania, je walimpa kura ngapi kwenye uchaguzi mkuu uliopita na alishika nafasi ya ngapi?......... naomba twende na hoja za kisomi kama msomi wetu Lipumba!
 
Wafungue tu hospitali zao bila hizo MoU Waswahili wa Kariakoo na Gerezani wakatibiwe tende na majini kwa jero na Masheikh. Kudadeki!
 
"Shura ya maimamu" wafungue hospitali zao bila MoU ili Waswahil wa Pwani nao waweze tibiwa mishipa na urogwaji kwa shilingi 200. Demand ni kubwa. Kwa mtaji huu, hata Waganga wa Kienyeji na Watoa Majini mitaa ya K'ndoni, Mbagala, Buguruni, Kimanzichana bila kusahau Gerezani na Kariakoo watakuwa hawana dili tena.
 
Kwani mleta mada kapata wapi taarifa kwamba Lipumba alikuwa UN? Mbona mi sijasikia habari za UN? Au mwenyewe Lipumba alisema kwamba alikuwa UN?
 
hoja si cuf hapa. ni uhakika kuwa alikuwa usa kwa kazi tajwa. nenda ka-google huwezi kajifunze mambo yako wazi mtandaoni mpaka mahojiano aliyofanya usa
 
Duh! sawa mkuu sisi hatujaona umuhimu wa kusoma ila tunadai tujengewe shule nyinyi wasomi wetu mmeamua kupeleka proposal pesa za umma ziende kanisani through MoU..

Usishangae mkuu sisi wanyonge na maskini hatujali sana tunashukuru kwa Muumba wetu..hii ndio destari yetu/

Vipi tajiri yangu na msomi wangu ...kuna ubaya kushukuru kwa lolote?

huyu nae ni GREAT THINKER? Jf imevamiwa.
 
Ndio mkuu ndio maana nimekubali wanachama wa CUF wametoka maeneo ya buguruni na mwananyamala kwa maskini wale ambao nyinyi mnawaona hawajasoma...

Kama ni umaskini namshukuru Muumba na kama ni tajiri namshukuru Muumba..

Nyie jamii yenu inaakili sana bana kwasababu ni wakristo na siyo maskini..sawa mkuu nimekusikia..

hivi Topical mbona unataka kutuchafulia uislamu wewe? Kuwa binadamu just a lit' bit basi. Nchi yetu haina hayo mambo ya udini ila chama cha CUF kinajitahidi kuyaeneza na hii imedhihilishwa na wanachama waliojitoa, sasa wewe unang'ang'ania kuwa sisi ni wajinga, mara maskini, mara hatuwezi. Tafadhali acha kutumia neno sisi kwani waislamu hawana hizo sifa tajwa hapo na kwa ushahidi kasome kitabu, kwani mwenyezi mungu kamwe havutiwi na mnyonge ila anapendezwa na shupavu. Kama unataka kutetea CUF itetee kwa hoja ila sio mfumo wako wa 'lol' utadhani tupo kwenye mipasho hapa.
 
Back
Top Bottom