Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
WanaJF:
Hii imekaaje? Polisi kuchunguzana kuhusu tuhuma zinazoelekezwa kwao wenyewe? Daima jamaa hawa hulkindana, hivi kweli haki itatendeka? Soma habari hii:
IGP Mwema: Tunachunguza Polisi waliotajwa na Mengi
Aunda timu ya polisi
Imekwisha kuanza kazi
Takukuru nao wachunguza
Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema
Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema, ameunda timu ya maofisa waandamizi wa polisi kuchunguza njama za maofisa watatu wa Jeshi hilo za kutaka kumbambika dawa za kulevya mtoto wa Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Abdiel Mengi.
Habari za njama hizo chafu zilifichuliwa na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi, juzi alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Mengi aliwataja maofisa hao watatu kuwa ni Mkuu wa Kitengo cha Kudhibiti Dawa za Kulevya, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Godfrey Nzowa, Mkuu wa Upelelezi wa Kanda
Maalum ya Dar es Salaam, Charles Mkumbo na askari mwingine wa kitengo cha Polisi wa Kimataifa (Interpol), aliyemtaja kwa jina moja la Hendry. Wote waliahidiwa kulipwa kiasi kukubwa cha fedha kuanzia Sh. milioni 15 hadi dola za Marekani 40,000.
IGP Mwema alisema timu hiyo ambayo iliundwa juzi usiku mara baada ya taarifa za madai hayo kutoka kwenye vyombo vya habari, ilianza kazi rasmi jana asubuhi na itaongozwa na Mkuu wa Upelelezi wa Jinai, (DCI), Robert Manumba.
Katika madai hayo, Mengi aliviambia vyombo vya habari kuwa, maofisa hao waandamizi wa jeshi hilo, walitaka kumbambika dawa za kulevya Abdiel katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Septemba 26, mwaka huu.
IGP Mwema alieleza kuwa alipokea taarifa za tukio hilo juzi usiku kwa njia ya simu ndipo alipoamua kuunda timu hiyo mara moja kwa ajili ya uchunguzi wa madai hayo.
"Kwa kawaida Jeshi la Polisi tuna kitengo cha kupokea malalamiko ya polisi wenyewe na wananchi, hili la Mengi tumelipokea kwa unyenyekevu kupitia vyombo vya habari, na kwa sasa tayari utekelezaji umeanza kuna timu nimeiunda," alisema.
Mwema alisema ameunda timu hiyo ili haki itendeke na ukweli ujulikane.
Alitaja baadhi ya watu waliopo kwenye timu hiyo kuwa ni Naibu DCI, Kamishna Msaidizi wa Jeshi hilo, Peter Kivuyo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Samson Kasala, pamoja na wadau wengine wa usalama.
"Siku zote penye ukweli uongo hujitenga, tumeunda timu hii ili tuweze kujua ukweli ni upi, lakini ili iwe ya uwazi zaidi, litakalojitokeza tutawaarifu na hatua zitachukuliwa kwa wale wote watakaobainika walitenda kosa," alisema.
Hata hivyo, Mwema alipoulizwa timu hiyo ameipa muda gani kukamilisha uchunguzi, alisema kutokana na taarifa alizipokea juzi usiku kwa njia ya simu (bila kumtaja aliyempigia), aliamua kuchukua hatua haraka kwa kuunda timu hiyo.
"Swali lako mwandishi nitalifanyia kazi nitakapokutana na timu husika, nitakaa nao ili tupange ichukue muda gani wa uchunguzi huo, lakini hadi sasa tayari wameshaanza kumhoji mhusika aliyetoa taarifa hizo (Mengi)," alisema. Katika hatua nyingine, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) nayo kwa upande wake imesema kuwa inaendeleza uchunguzi wa tukio hilo ulioanzishwa na vyombo vingine vya upelelezi chini ya ofisi ya DCI.
Taarifa iliyotolewa jana na Takukuru kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Ofisa Uhusiano, Doreen Kapwani, ilisema kuwa watafanya hivyo kutokana na malalamiko hayo kudaiwa kuhusishwa na vitendo vya rushwa.
Aidha, Takukuru imewataka wale wote wenye ushahidi kuhusiana na tuhuma hizo kutoa ushirikiano ili waweze kufanikisha uchunguzi wao.
Mpango huo kwa Mujibu wa Mengi, ungetekelezwa siku Abdiel alipokuwa asafiri kikazi kwenda India na wenzake wanne Septemba 26, mwaka huu.
Aidha, Mengi alisema bahati nzuri mtoto wake aliahirisha safari hiyo ndipo mchezo huo uliposhindwa kufanikiwa, lakini watuhumiwa hao walikuwa wamekwisha kupokea nusu ya malipo ya kazi hiyo.
Alisema Kamishna Nzowa, Kamanda Mkumbo Henry, waliahidiwa donge la Dola za Kimarekani 40,000 wakati vijana wawili ambao ni wafanyakazi wa uwanja wa ndege waliahidiwa Sh. milioni 15 kila mmoja.
Mengi alisema baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema, alilazimika kufuatilia tukio hilo kwa kina na kubaini kuwa maofisa hao walipokea nusu ya malipo ambayo ni Dola za Marekani 20,000 kila mmoja wakati vijana wa uwanja wa ndege walipewa Sh. milioni saba kila mmoja.
Pia, alisema kuwa mchezo huo ulimhusisha kijana mmoja anayefanya kazi kwenye kampuni za simu nchini ambaye hakumtaja jina lake.
Alisema kijana huyo aliahidiwa Sh. milioni 15 na kwamba alipewa Sh. milioni saba kama malipo ya awali.
Mengi alisema kashfa hiyo iliasisiwa na mfanyabishara mmoja nchini ambaye ni miongoni mwa wale aliowataja kuwa mafisadi papa mwaka jana, na kwamba alitenga Sh. bilioni tatu kutekeleza uovu huo.
CHANZO: NIPASHE
Hii imekaaje? Polisi kuchunguzana kuhusu tuhuma zinazoelekezwa kwao wenyewe? Daima jamaa hawa hulkindana, hivi kweli haki itatendeka? Soma habari hii:
IGP Mwema: Tunachunguza Polisi waliotajwa na Mengi
Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema
Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema, ameunda timu ya maofisa waandamizi wa polisi kuchunguza njama za maofisa watatu wa Jeshi hilo za kutaka kumbambika dawa za kulevya mtoto wa Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Abdiel Mengi.
Habari za njama hizo chafu zilifichuliwa na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi, juzi alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Mengi aliwataja maofisa hao watatu kuwa ni Mkuu wa Kitengo cha Kudhibiti Dawa za Kulevya, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Godfrey Nzowa, Mkuu wa Upelelezi wa Kanda
Maalum ya Dar es Salaam, Charles Mkumbo na askari mwingine wa kitengo cha Polisi wa Kimataifa (Interpol), aliyemtaja kwa jina moja la Hendry. Wote waliahidiwa kulipwa kiasi kukubwa cha fedha kuanzia Sh. milioni 15 hadi dola za Marekani 40,000.
IGP Mwema alisema timu hiyo ambayo iliundwa juzi usiku mara baada ya taarifa za madai hayo kutoka kwenye vyombo vya habari, ilianza kazi rasmi jana asubuhi na itaongozwa na Mkuu wa Upelelezi wa Jinai, (DCI), Robert Manumba.
Katika madai hayo, Mengi aliviambia vyombo vya habari kuwa, maofisa hao waandamizi wa jeshi hilo, walitaka kumbambika dawa za kulevya Abdiel katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Septemba 26, mwaka huu.
IGP Mwema alieleza kuwa alipokea taarifa za tukio hilo juzi usiku kwa njia ya simu ndipo alipoamua kuunda timu hiyo mara moja kwa ajili ya uchunguzi wa madai hayo.
"Kwa kawaida Jeshi la Polisi tuna kitengo cha kupokea malalamiko ya polisi wenyewe na wananchi, hili la Mengi tumelipokea kwa unyenyekevu kupitia vyombo vya habari, na kwa sasa tayari utekelezaji umeanza kuna timu nimeiunda," alisema.
Mwema alisema ameunda timu hiyo ili haki itendeke na ukweli ujulikane.
Alitaja baadhi ya watu waliopo kwenye timu hiyo kuwa ni Naibu DCI, Kamishna Msaidizi wa Jeshi hilo, Peter Kivuyo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Samson Kasala, pamoja na wadau wengine wa usalama.
"Siku zote penye ukweli uongo hujitenga, tumeunda timu hii ili tuweze kujua ukweli ni upi, lakini ili iwe ya uwazi zaidi, litakalojitokeza tutawaarifu na hatua zitachukuliwa kwa wale wote watakaobainika walitenda kosa," alisema.
Hata hivyo, Mwema alipoulizwa timu hiyo ameipa muda gani kukamilisha uchunguzi, alisema kutokana na taarifa alizipokea juzi usiku kwa njia ya simu (bila kumtaja aliyempigia), aliamua kuchukua hatua haraka kwa kuunda timu hiyo.
"Swali lako mwandishi nitalifanyia kazi nitakapokutana na timu husika, nitakaa nao ili tupange ichukue muda gani wa uchunguzi huo, lakini hadi sasa tayari wameshaanza kumhoji mhusika aliyetoa taarifa hizo (Mengi)," alisema. Katika hatua nyingine, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) nayo kwa upande wake imesema kuwa inaendeleza uchunguzi wa tukio hilo ulioanzishwa na vyombo vingine vya upelelezi chini ya ofisi ya DCI.
Taarifa iliyotolewa jana na Takukuru kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Ofisa Uhusiano, Doreen Kapwani, ilisema kuwa watafanya hivyo kutokana na malalamiko hayo kudaiwa kuhusishwa na vitendo vya rushwa.
Aidha, Takukuru imewataka wale wote wenye ushahidi kuhusiana na tuhuma hizo kutoa ushirikiano ili waweze kufanikisha uchunguzi wao.
Mpango huo kwa Mujibu wa Mengi, ungetekelezwa siku Abdiel alipokuwa asafiri kikazi kwenda India na wenzake wanne Septemba 26, mwaka huu.
Aidha, Mengi alisema bahati nzuri mtoto wake aliahirisha safari hiyo ndipo mchezo huo uliposhindwa kufanikiwa, lakini watuhumiwa hao walikuwa wamekwisha kupokea nusu ya malipo ya kazi hiyo.
Alisema Kamishna Nzowa, Kamanda Mkumbo Henry, waliahidiwa donge la Dola za Kimarekani 40,000 wakati vijana wawili ambao ni wafanyakazi wa uwanja wa ndege waliahidiwa Sh. milioni 15 kila mmoja.
Mengi alisema baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema, alilazimika kufuatilia tukio hilo kwa kina na kubaini kuwa maofisa hao walipokea nusu ya malipo ambayo ni Dola za Marekani 20,000 kila mmoja wakati vijana wa uwanja wa ndege walipewa Sh. milioni saba kila mmoja.
Pia, alisema kuwa mchezo huo ulimhusisha kijana mmoja anayefanya kazi kwenye kampuni za simu nchini ambaye hakumtaja jina lake.
Alisema kijana huyo aliahidiwa Sh. milioni 15 na kwamba alipewa Sh. milioni saba kama malipo ya awali.
Mengi alisema kashfa hiyo iliasisiwa na mfanyabishara mmoja nchini ambaye ni miongoni mwa wale aliowataja kuwa mafisadi papa mwaka jana, na kwamba alitenga Sh. bilioni tatu kutekeleza uovu huo.
CHANZO: NIPASHE