Machozi

X-PASTER

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
11,610
1,810
Machozi

Kila kitaka yafuta, mengine yanasogea
Chozi churuta churuta, Nguoni yanaingia
Walokufa hawajafata, nasaba nilozaliwa

Wamekufa zinjibari, pahala tulozaliwa
imewabana bahari, hawana pakukimbia
wengi wakitafakari, mauti yanawajia

Mauti ni machungu, hakuna anokataa
huzidi yakiwa chungu, kwa sababu soyofaa
tamaa ya ulimwengu, ndio watu yahadaa

Msiba huu jamani, ukubwa sijaujua
Umeathiri wandani, mpaka nje ya dunia
Roho zetu mefundani, Mola tatuhukumia

Hukumu itapitishwa, wasiwasi tusitia
Mtoto wa miaka sita, baharini aelea
jaketi yeye kavishwa, mama mtu kajifia

nduguye kamkamata, miwili hajatimia
waelea usiku kutwa, macho wazi wakodoa
Nugwi bahari waikata, malaika wawapepea

hapa ndio tunaona, uwezo wa subuhana
watoto hawa wapona, bahari ya maulana
Rabi wape yalomema, duniani na kiyama

Tupoe wazanzibari, msiba ulotufikia
haya si yetu khiyari, tungeweza yazuwia
alipangalo jalali, katu kulipangua

Rabi warehemu, waja walotangulia
Uwatie peponi, moya baada ya moya
huko wende kaonani, na zao familia

©Intisar Al'Abri
 
Back
Top Bottom