Macho makavu - aibu tena ya kike hakuna?

Umeanza kwenda nje ya mada. Kazi yako, utaanzishiwa thread...
:focus:
Sometimes wanaume pia hawana aibu, tuseme tu ukweli.
Unakuta mwanaume anatongoza kwa kutumia maneno ambayo hata kwa kuyasoma peke yako chumbani utaona aibu!
Alafu the way anataka akushike shike... unamsalimia kwa mkono anakukuna hivi in the palm, au anataka akuvute, akukiss huku humjui hakujui, ndo kwanza mmekutana! shame...

Mimi nitawalaumu wanaume.Ukiwa mwanamke wa heshima, una staha na aibu, mumeo au bf wako hakawii kukupa shock kwa kuparamia migumegume na mikurumbembe! Wanaume wenyewe wamekosa adabu sana siku hizi, wanashobokea sana malaya. Nyumbani hatoi matumizi, kutwa kwenda kuhonga malaya! Maokeo yake wasichana wadogo wanaochipukia wanafikiria ukiwa na tabia za kimalayamalaya ndio unavutia wanaume.Sasa sijui mnalalamika nini wakati nyie ndio mnaonyesha mnayotaka - nataka sitaki mnachanganya wanawake! Jirekebisheni nyie wenyewe kwanza.
 
Kwani kukosa aibu ni tabia za kimalaya??

Labda nieleweshwe hiyo aibu inayoongelewa ni ipi??

Mimi nitawalaumu wanaume.Ukiwa mwanamke wa heshima, una staha na aibu, mumeo au bf wako hakawii kukupa shock kwa kuparamia migumegume na mikurumbembe! Wanaume wenyewe wamekosa adabu sana siku hizi, wanashobokea sana malaya. Nyumbani hatoi matumizi, kutwa kwenda kuhonga malaya! Maokeo yake wasichana wadogo wanaochipukia wanafikiria ukiwa na tabia za kimalayamalaya ndio unavutia wanaume.Sasa sijui mnalalamika nini wakati nyie ndio mnaonyesha mnayotaka - nataka sitaki mnachanganya wanawake! Jirekebisheni nyie wenyewe kwanza.
 
Umeanza na "watu walikuwa na...staha, heshima..." halafu ghafla ikageuka kuwa "hivyo...dada zetu...wasingeweza kuyazungumza...."

Imetokaje kwenye ''watu'' kutakiwa kuwa na heshima kwenda kwenye ''hivyo dada zetu''? Kwanini ume target na kushambulia ''dada zetu''? Mwanamme yeye hatakiwi kuwa na heshima na staha?

Huu ni mfumo dume wa kizamani, eti mwanamme yeye awe huru kuongea machafu chafu bila heshima wala staha na kutembea kifua wazi barabarani akitaka, halafu mwanammke ndio awe na "aibu... staha... heshima... afunike sketi haraka kama ikipeperushwa..." ili awe "sexy." How preposterous! Male chauvinism of the most ridiculous kind.


Kama umemuelewa MKJJ na bado ukawa na maoni hayo basi una kazi.
We kama ni mwanaume utakua unpenda machangudoa ua maguberi!Kama ni mwanamke basi wewe ni gumegume!
 
Kwa wanaume wa ukweli , mwanamke akiwa muwazi sana , asie na aibu na macho makavu huwa tunamshtukia tu. `kitu` kikifichwa fichwa lakini kikijulikana kipo kina mvuto zaidi kuliko kilicho hadharani.
 
Kama umemuelewa MKJJ na bado ukawa na maoni hayo basi una kazi.
We kama ni mwanaume utakua unpenda machangudoa ua maguberi!Kama ni mwanamke basi wewe ni gumegume!

Hebu tueleweshe kwa nini umefikia conclusion hiyo?

Hudhani kuwa na wanaume nao wanatakiwa kuwa na heshima na staha kama wanawake?
 
Hebu tueleweshe kwa nini umefikia conclusion hiyo?

Hudhani kuwa na wanaume nao wanatakiwa kuwa na heshima na staha kama wanawake?

Mada imeanzishwa kujadili "wasichana/wanawake " na kukosa aibu. Atakuwa ana sababu zake kuanzisha mada.
Kama mnataka kuzungumzia wanaume na kukosa aibu kwanini msianzishe yenu?
 
Mada imeanzishwa kujadili "wasichana/wanawake " na kukosa aibu. Atakuwa ana sababu zake kuanzisha mada.
Kama mnataka kuzungumzia wanaume na kukosa aibu kwanini msianzishe yenu?

Ndio tunamuelewesha kuwa kwanza wanawake kukosa aibu ndivyo inavyotakiwa, kama ukilielewa neno aibu. Pili, kuwataka wanawake tu wawe na heshima na taadhima na kuwaacha wanaume wafanye watakavyo ni mfumo dume
 
nimeipenda hii..na angesema hivi ningemtafuta maana kuna uhakika wa solution lol..
but "could" or 'might' itanipotezea muda

solution inategemea na how much you are looking for....
nisiseme ninazo kumbe hazikutoshi lol
 
We si mchumba wangu tayari babu? lol
Yes, I would marry you :)
Tusichakachue thread ya watu, toa mchango wako kwanza...
Mi sipendi mwanamke mwenye aibu, nampenda mwanamke mwenye haya... Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuona aibu na kuona haya.....

Umenielewa? Kama hujanielewa nitafute PM ukiwa without.
 
Nafanya kitu ambacho ni appropriate kwa muda huo ..
iwe mavazi, maongezi, etc.. as long i'm happy ..
Hapo nadhani hakuna atakaeona kosa. Sio mtu ndio kwanza mmekutana eti unamuuliza ana shilingi ngapi :shock:
 
i like your post aisee maanake dadazetu wamekosa aibu kabisa hadi nashangaa ndo utandawazi inafikia point unakuta mwanamke anatukana matusi mpka unaogopa kabisa kma kweli ni binadamu wa kawaida mfano kuna matusi ya viungo vya miili yao wanapenda sana kuitumia hata mbele ya audience does not care huwa nashangaa. dada zetu rudisheni ili aibu yenu i like it aiseee

Wanaharakati hawachelewi kusema kuwa hawa watukanaji wa kike wamefundishwa na wanaume chini ya mfumo dume.
 
Back
Top Bottom