Mabwege uishi miaka mingi 1

Jacaranda

Member
Oct 23, 2011
45
20
Jua lililokuwa limetawala lilimezwa ghafla na mawingu yaliyokuwa yametanda.kiupepo kilianza kuvuma na kubeba takataka nyepesi na kuzirusha juu na kulifanya angaa litawaliwe na rangi nyeusi ya mifuko ya plastiki.Viatu vyangu nilivyo vaa vilipigwa na vumbi na kuvifanya vionekane kama vimeopolewa toka kwenye kifusi cha udongo wa mererani.Ghafla manyunyu yakaanza kudondoka,nikaongeza mwendo huku nikiwa nimeificha bahasha ya kaki iliyokuwa na vyeti vyangu kwapani,taratibu kimvua kikazidi na hivyo kunifanya nianze kukimbia huku mkono wangu wa kulia nikiwa nimeuweka kwenye mfuko wangu wa suruali kuzuia shilingi mia tatu niliyobakiza isidondoke.

Nilipofika kituo cha mwenge nilikua nimebakiza shilingi mia tatu kwa hiyo nikakata shauri ya kutembea kwa mguu mpaka ubungo kisha nipande daladala kumalizia safari yangu mpaka mbezi kibanda cha mkaa.Nilipofika maeneo ya Mlimani city Mvua ikazidi kuongezeka kiasi cha kunifanya nisiweze kuona mbele vizuri.Nilipoangalia kushoto nikaona watu wengi wakikimbilia ndani ya maduka ya mlimani city nikajiunga nao.Nilipofika ndani ya jengo la mlimani city nikaifungua bahasha yangu na kuvitazama vyeti vyangu baada ya kuridhika kuwa havijaloana nikatabasamu huku nikijifuta uso wangu kwa handkcheif ambayo ilikuwa ikitoa harufu ya jasho,niilipomaliza nikaikunja nakuiweka kwenye mfuko wa shati nililokuwa nimelivaa,Ambalo kwa sasa lilikuwa limeloana na hivyo kuufanya uchafu uliokuwa umejificha kuonekana vizuri zaidi.Niliponyanyua macho yangu nikagonganisha macho yangu na kikundi cha watu waliokuwa wakinitazama utafikiri nzi aliyedondokea kwenye chakula chao cha gharama.Nikajitazama aikunichukua muda kujua kwa nini walikuwa wakinishangaa.Kwa jinsi nilivyokuwa mchafu sikuwa na tofauti na mchimbaji wa tanzanite aliyeshinda handakini kwa wiki nzima bila kubadirisha nguo,ghafla nikajihisi kama mkimbizi ndani ya nchi nisiyotakiwa."Go to hell" nikasonya kwa sauti ya chini huku nikingia kwenye duka la vitabu liitwalo scholastica

Nikaelekea moja kwa moja kwenye shelfu lenye novel,nikachomoa kitabu kimoja nikageuza nyuma,nikaanza kusoma muhtasari wake taratibu.wakati nikiendelea kusoma nikasikia sauti nyororo ya msichana ikiimba kwa sauti ya chini nikageuka kumtazama.Nilipigwa na butwaa,nikajihisi kama mtu aliyepigwa na radi,midomo yangu ikabaki wazi,kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nikajiona nimekuwa zuzu.Macho yangu hayakuamini nilichokiona nikayaficha kisha nikakodoa zaidi na kugundua kuwa siko ndotoni.Msichana aliyekuwa amesimama mbele yangu alikuwa ni mzuri sijapata kuona.Alikuwa na uso mzuri uliopambwa na macho yaliyomfanya haonekane kama amelemewa na usingizi,midomo yake ilikuwa imekaa vyema kama ungeilinganisha na ya Angelina Jolly ni wazi Angelina angeonekana kikaragosi.Alikuwa na nywele nyingi zilizoanguka mabegani na baadhi alikuwa amezirushia usoni na hivyo kumfanya aonekane mzuri zaidi.Alikuwa amevalia kitop cha rangi ya pinki kilichoyafanya maziwa yake yaliojazia vyema yajitokeze vizuri na kuonekana kama vichuguu viwili vilivyotenganishwa na kinjia chembamba,nikayatuliza macho yangu kwenye kifua chake huku nikihisi kama nitayaondoa macho yangu wenda pumzi yangu itakata,nikajikuta nikiwaza kama mimi ningekuwa msichana na ninakifua kama hicho basi tayari ningekuwa nishakua milionea,kitopu chake kilikomea juu ya kitovu na hivyo kulifanya tumbo lake lisilo na kitambi kuonekana.Chini alikuwa amevalia kaptura ya rangi nyeusi ambayo ilikuwa imefikaa mpaka magotini na hivyo kuzisitiri hips zake ambazo kwa ukubwa zilizokuwa nao zilikuwa zikipigana na nyuzi za kaptura hiyo kutakaa kuzitatua.Alikuwa ni mrefu wa wastani huku kiuno chake cha nyingu kikimfanya hazidi kuonekana kama malaika aliyedondoka kwa bahati mbaya toka mbiguni.Nilipogonganisha macho yangu na yake, nikaugeza uso wangu kwa aibu utafikiri mtu aliyekamatwa akipiga chabo.Nikayarudisha macho yangu kwenye novel iliyokuwa mkononi mwangu.

Mawazo yangu hayakuwa tena kwenye kitabu,moyo wangu ulijihisi kumpenda ghafla huyo msichana,lakini nilijua kamwe siwezi kumpata na jambo jingine lilikuwa wazi baada ya kumuona huyo msichana sitaweza tena kumpenda msichana mwingine mpaka siku sura yake itakapotoweka katika fikra zangu.Ufunuo huu ulinifanya niwe mnyonge moyoni mwangu huku sehem nyingine ya moyo wangu ikihisi furaha fulani ya ajabu ya japo kumuona,"Hicho ni kitabu cha Mario Puzo Godfather?" sikutegemea kuongeleshwa na yule msichana,nikajikuta nimenyanyua uso na kumkodolea macho kisha nikakigeuza kitabu nilichokuwa nimekishika na kukiangalia nikakutana na maandishi makubwa yalioandikwa Godfather Mario Puzo.Ghafla tumbo langu likatoa miungurumo ambayo ilisikika na kunifanya nione aibu nikakumbuka kuwa mchana wa siku hiyo nilikuwa sijala kisa kutokuwa na hela."Ndi ndi............" nikajikuta nimekabwa na kigugumizi akanikatisha na kuniambia "you should buy it.it is a very nice novel" sauti yake nyororo ikaamusha hisia fulani akilini na mwilini mwangu,nikahisi kama viungo vyangu vya kiume vinasimama taratibu.nikakishusha kitabu mpaka katikati ya mapaja yangu ili kujisitiri.nilipomuangalia nikamuone bado anakiangalia kitabu ambacho kwa sasa kilikuwa kimeshafika mapajani mwangu.
AISEEE NIMECHOKA TUTAENDELEA
 
Nimeipenda story yako. Nzuri sana.

Si kwa ubaya ..
Ila umetumia neno "NIKA"karibu kila sentence na sehemu nyingine umetumia neno hiilo zaidi ya mara tatu kwenye sentence moja. Kama una plan kuwa muandishi WA vitabu just be careful with that word . Otherwise great job.
 
Jua lililokuwa limetawala lilimezwa ghafla na mawingu yaliyokuwa yametanda.kiupepo kilianza kuvuma na kubeba takataka nyepesi na kuzirusha juu na kulifanya angaa litawaliwe na rangi nyeusi ya mifuko ya plastiki.Viatu vyangu nilivyo vaa vilipigwa na vumbi na kuvifanya vionekane kama vimeopolewa toka kwenye kifusi cha udongo wa mererani.Ghafla manyunyu yakaanza kudondoka,nikaongeza mwendo huku nikiwa nimeificha bahasha ya kaki iliyokuwa na vyeti vyangu kwapani,taratibu kimvua kikazidi na hivyo kunifanya nianze kukimbia huku mkono wangu wa kulia nikiwa nimeuweka kwenye mfuko wangu wa suruali kuzuia shilingi mia tatu niliyobakiza isidondoke.

Nilipofika kituo cha mwenge nilikua nimebakiza shilingi mia tatu kwa hiyo nikakata shauri ya kutembea kwa mguu mpaka ubungo kisha nipande daladala kumalizia safari yangu mpaka mbezi kibanda cha mkaa.Nilipofika maeneo ya Mlimani city Mvua ikazidi kuongezeka kiasi cha kunifanya nisiweze kuona mbele vizuri.Nilipoangalia kushoto nikaona watu wengi wakikimbilia ndani ya maduka ya mlimani city nikajiunga nao.Nilipofika ndani ya jengo la mlimani city nikaifungua bahasha yangu na kuvitazama vyeti vyangu baada ya kuridhika kuwa havijaloana nikatabasamu huku nikijifuta uso wangu kwa handkcheif ambayo ilikuwa ikitoa harufu ya jasho,niilipomaliza nikaikunja nakuiweka kwenye mfuko wa shati nililokuwa nimelivaa,Ambalo kwa sasa lilikuwa limeloana na hivyo kuufanya uchafu uliokuwa umejificha kuonekana vizuri zaidi.Niliponyanyua macho yangu nikagonganisha macho yangu na kikundi cha watu waliokuwa wakinitazama utafikiri nzi aliyedondokea kwenye chakula chao cha gharama.Nikajitazama aikunichukua muda kujua kwa nini walikuwa wakinishangaa.Kwa jinsi nilivyokuwa mchafu sikuwa na tofauti na mchimbaji wa tanzanite aliyeshinda handakini kwa wiki nzima bila kubadirisha nguo,ghafla nikajihisi kama mkimbizi ndani ya nchi nisiyotakiwa."Go to hell" nikasonya kwa sauti ya chini huku nikingia kwenye duka la vitabu liitwalo scholastica

Nikaelekea moja kwa moja kwenye shelfu lenye novel,nikachomoa kitabu kimoja nikageuza nyuma,nikaanza kusoma muhtasari wake taratibu.wakati nikiendelea kusoma nikasikia sauti nyororo ya msichana ikiimba kwa sauti ya chini nikageuka kumtazama.Nilipigwa na butwaa,nikajihisi kama mtu aliyepigwa na radi,midomo yangu ikabaki wazi,kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nikajiona nimekuwa zuzu.Macho yangu hayakuamini nilichokiona nikayaficha kisha nikakodoa zaidi na kugundua kuwa siko ndotoni.Msichana aliyekuwa amesimama mbele yangu alikuwa ni mzuri sijapata kuona.Alikuwa na uso mzuri uliopambwa na macho yaliyomfanya haonekane kama amelemewa na usingizi,midomo yake ilikuwa imekaa vyema kama ungeilinganisha na ya Angelina Jolly ni wazi Angelina angeonekana kikaragosi.Alikuwa na nywele nyingi zilizoanguka mabegani na baadhi alikuwa amezirushia usoni na hivyo kumfanya aonekane mzuri zaidi.Alikuwa amevalia kitop cha rangi ya pinki kilichoyafanya maziwa yake yaliojazia vyema yajitokeze vizuri na kuonekana kama vichuguu viwili vilivyotenganishwa na kinjia chembamba,nikayatuliza macho yangu kwenye kifua chake huku nikihisi kama nitayaondoa macho yangu wenda pumzi yangu itakata,nikajikuta nikiwaza kama mimi ningekuwa msichana na ninakifua kama hicho basi tayari ningekuwa nishakua milionea,kitopu chake kilikomea juu ya kitovu na hivyo kulifanya tumbo lake lisilo na kitambi kuonekana.Chini alikuwa amevalia kaptura ya rangi nyeusi ambayo ilikuwa imefikaa mpaka magotini na hivyo kuzisitiri hips zake ambazo kwa ukubwa zilizokuwa nao zilikuwa zikipigana na nyuzi za kaptura hiyo kutakaa kuzitatua.Alikuwa ni mrefu wa wastani huku kiuno chake cha nyingu kikimfanya hazidi kuonekana kama malaika aliyedondoka kwa bahati mbaya toka mbiguni.Nilipogonganisha macho yangu na yake, nikaugeza uso wangu kwa aibu utafikiri mtu aliyekamatwa akipiga chabo.Nikayarudisha macho yangu kwenye novel iliyokuwa mkononi mwangu.

Mawazo yangu hayakuwa tena kwenye kitabu,moyo wangu ulijihisi kumpenda ghafla huyo msichana,lakini nilijua kamwe siwezi kumpata na jambo jingine lilikuwa wazi baada ya kumuona huyo msichana sitaweza tena kumpenda msichana mwingine mpaka siku sura yake itakapotoweka katika fikra zangu.Ufunuo huu ulinifanya niwe mnyonge moyoni mwangu huku sehem nyingine ya moyo wangu ikihisi furaha fulani ya ajabu ya japo kumuona,"Hicho ni kitabu cha Mario Puzo Godfather?" sikutegemea kuongeleshwa na yule msichana,nikajikuta nimenyanyua uso na kumkodolea macho kisha nikakigeuza kitabu nilichokuwa nimekishika na kukiangalia nikakutana na maandishi makubwa yalioandikwa Godfather Mario Puzo.Ghafla tumbo langu likatoa miungurumo ambayo ilisikika na kunifanya nione aibu nikakumbuka kuwa mchana wa siku hiyo nilikuwa sijala kisa kutokuwa na hela."Ndi ndi............" nikajikuta nimekabwa na kigugumizi akanikatisha na kuniambia "you should buy it.it is a very nice novel" sauti yake nyororo ikaamusha hisia fulani akilini na mwilini mwangu,nikahisi kama viungo vyangu vya kiume vinasimama taratibu.nikakishusha kitabu mpaka katikati ya mapaja yangu ili kujisitiri.nilipomuangalia nikamuone bado anakiangalia kitabu ambacho kwa sasa kilikuwa kimeshafika mapajani mwangu.
AISEEE NIMECHOKA TUTAENDELEA
nice story
 
ulipo taja the god father,mh umenikumbusha,the last don na the ometra.hivi vitabu vya mario puzo navipenda sana.
 
Nimeipenda story yako. Nzuri sana.

Si kwa ubaya ..
Ila umetumia neno "NIKA"karibu kila sentence na sehemu nyingine umetumia neno hiilo zaidi ya mara tatu kwenye sentence moja. Kama una plan kuwa muandishi WA vitabu just be careful with that word . Otherwise great job.

Nimekusoma
 
Nimeipenda story yako. Nzuri sana.

Si kwa ubaya ..
Ila umetumia neno "NIKA"karibu kila sentence na sehemu nyingine umetumia neno hiilo zaidi ya mara tatu kwenye sentence moja. Kama una plan kuwa muandishi WA vitabu just be careful with that word . Otherwise great job.

editor wake si wewe?
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom