Maboresho ya Posho ya Kuchunguza Maiti kwa Madaktari..

samora10

JF-Expert Member
Jul 21, 2010
7,594
4,798
Wakuu ni muda mrefu nimejaribu kufuatilia sakata la mgomo wa madaktari na serikali yetu.. Kiukweli sijafurahishwa na jinsi serikali inavyolishughulikia suala hili, Ni kama vile viongozi wetu wanaendesha nchi kidikteta na hapa sitataka kuanza kuongelea mkasa uliompata ndugu yetu Ulimboka na mengineyo mengi ila kuna mambo sio ya kufumbia macho asilani..

Fikiria ndugu yako anakufa pale muhimbili halafu mtu anasimama pale bungeni na kuuambia uma eti wamepandisha posho ya kuchunguza maiti na eti huduma ziko sawa na wananchi wasiwe na wasiwasi wakati anajua kabisa kwamba hali sivyo anavyoongea.


Turudi kwenye hoja ya msingi.. Tumesikia Serikali ikijisifia kupandisha POSHO YA KUCHUNGUZA MAITI toka 5000/= mpaka 100,000/= wakati posho ya daktari anayeacha familia yake nyumbani na kuhudumia wagonjwa masaa 24 akilipwa elfu 20!

Najiuliza hivi hawa watawala hua wanafikiria nini? Yani walimaanisha nini kuongeza posho ya kuchunguza maiti na kuacha posho ya muhimu kabisa? Ndio kusema kwamba viongozi/wanasiasa wetu wanathamini maiti kuliko huyu anayeokoa maisha ya wagonjwa? Wanataka madaktari waanze kuua ili wapate posho nene za kuchunguza maiti?

Naomba tutafakari hili..
 
samora10 hiyo posho mmoja wa viongozi wa madaktari amewahi izungumzia kwamba kwa hapa nchini madaktari bingwa wa kufanya uchunguzi wa maiti hawazidi 10!
 
pole kamanda, viongozi ndo hatuna,. wanaona ni bora maiti ichunguzwe utadhani watamfufua kuliko kumtibu mgonjwa apone..huku wenyewe wakikwea mapipa kwenda apollo.
 
pole kamanda, viongozi ndo hatuna,. wanaona ni bora maiti ichunguzwe utadhani watamfufua kuliko kumtibu mgonjwa apone..huku wenyewe wakikwea mapipa kwenda apollo.

Asante mkuu ukiiangalia sana hii kitu unaweza fikiria mambo mengi sana.. ila tunaenda kubaya sana, hizi siasa zinazowekwa kwenye mambo ya msingi zitakuja kututokea puani siku moja
 
samora10 hiyo posho mmoja wa viongozi wa madaktari amewahi izungumzia kwamba kwa hapa nchini madaktari bingwa wa kufanya uchunguzi wa maiti hawazidi 10!

Kwa hiyo mkuu timbilimu hizo numbers ziliwekwa hapo makusudi ili wananchi waone kwamba kuna madai yameshughulikiwa.. sasa tunawadanganya wananchi ili iweje? hivi hawawezi kabisa kufanya chochote cha maana?
 
Last edited by a moderator:
Kama posho hiyo imepandishwa ni kwa madaktari ambao idadi yao ni watano nchi nzima, ndio maana ulisikia raia wa Ethiopia waliofariki kwenye roli walisubiri daktari atoke Dar. Kama wapo madaktari hao kwanini hawakuwatumia wa Dodoma? Hizo ni FIX za watawala wenu waonekane wanajali sana maslahi ya Madaktari. Mbona hawapandishi maeneo mengine ambapo kuna madaktari wengi.
 
uwezi amini,utazani nchi inaongozwa na vichaa.Au viongozi wetu wamewekewa micro chip kwenye ubongo na super computer ina control bongo zao.
 
Back
Top Bottom