Mabomu yarindima uchaguzi wa serikali za mitaa,mtaa wa Bondeni kata ya Masekelo mkoani Shinyanga

sammosses

JF-Expert Member
Jan 24, 2011
1,682
1,110
Ni saa tano na robo usiku matokeo ya uchaguzi wa serikali za mtaa yanatangazwa kwa kumtangaza mshindi wa kiti cha mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa bondeni kupitia CCM na kusindikizwa na mabomu yaliyorindima.Sababu za kurindima mabomu hayo mpaka sasa hazijulikani,hali inayopelekea kuchafua jina la chama tawala kwa kutoweza kutangazwa mgombea wake pasi na mabomu.

Wananchi wa kata hiyo wameshangazwa na tukio hilo la mabomu kiasi cha kupelekea kupoteza imani na CCM kwa kutumia vyombo vya dola vibaya kwa maslahi ya binafsi na kusahau kuwa chombo hiki ni mali ya umma na kina wajibu wa kulinda mali na raia wake.
]

Iko wapi demokrasia ya kweli ikiwa hata chaguzi za serikali za mitaa zinagubikwa na ukiukwaji mbaya wa vyombo vya dola.Hali hii imeleta picha mbaya kwa uchaguzi mkuu ujao.Nini tufanye kuinusuru hali hii,kama wananchi watachoka na kuamua kujibu mapigo na kutokukubali kuonewa?
 
Mkuu mbona husemi sababu ya mabomu kupigwa. Ni mabomu ya machozi au mabomu ya kudungua ndege? Uchaguzi ulikuwa wa mtaa lakini wananchi wa kata wameshangaa! Tuambie basi ilikuwaje hadi polisi, kama ni polisi, wafike huko na mabomu manake si rahisi rahisi kuwa na mabomu.
 
Mabomu yaliyopigwa ni mabomu ya machozi.Kwanza muda wa kuhesabu kura ulichukua muda mrefu kiasi uvumilivu uliwashinda wananchi na kuimba,tunataka matokeo.Dalili za polisi kuchafua hali ya hewa zilijionyesha mapema mara baada ya magari yaliyobeba askari polisi kuingia kwa mbwembwe.Kama matokeo tu ya serikali za mitaa yanachukua masaa yote hayo je uchaguzi mkuu utachukua muda gani?

Pia ni kwanini basi kila panapotokea mgombea kupitia CCM ameshinda askari polisi hujiandaa kwa mapambano kabla ya matokeo husika kutangazwa,hali inayopeleka wapiga kura kutokuwa na imani na wasimamizi na serikali.
 
Back
Top Bottom