Mabomu Gongo la Mboto: Mwinyi asema hajiuzulu

Nguruvi3

Platinum Member
Jun 21, 2010
15,387
31,322
Nimemsikia waziri wa Ulinzi Mh Hussein Mwinyi akihojiwa na VoA swahili. Pamoja na maswali mengine ameulizwa kuhusu kuwajibika kwa kujiuzulu.
Mwinyi: Kujiuzulu kunatoka na makosa yaliyofanywa na mamlaka iliyoko chini ya mtu kama itadhihirika. Tusubiri tume itakayoundwa na tupate matokeo yake kwanza.

My Take:
1. Hili ni tatizo la pili kutokea. Tume ni ya nini ikiwa ile ya kwanza hatukujua nini kilifanyaka?
2. Tunajua kuwa njia rahisi ya kiongozi asiyeweza kupambanua mambo ni tume ili kutengeneza mazingira ya kutengeneza hadithi.
3. Mh Mwinyi anataka kutufanya Watanzania mbumbumbu sana.
Dhana(concept) ya kuwajibika ina maana zaidi ya moja.
a) Kuwajibika kwa makosa ya watendaji kisheria kama alivyosema yeye Mwinyi.
b) Kupisha uchunguzi halali usioingiliwa na wale wanaochunguzwa
c) Kuonyesha machungu au kutoridhika kwa kile kilichotokea, na hapa ni vifo huku
kiongozi husika akiwa na dhamana.(sympath)

Zote (a), (b), (c) zinamgusa Mh Mwinyi moja kwa moja. Wakati leo kuna watu wana misiba mizito majumbani kwao, wengine wapo mahospitalini, watoto hawajui wazazi wapo wapi, mali zimeharibiwa na watu hawajui nini cha kufanya, makazi hakuna watu wapo kwa majirani, hivi kweli hata kama kifungu (a) na (b) hapo juu hakimhusu kiongozi, je kifungu (c) cha kuonyesha huruma na machungu nacho pia kiongozi hawezi kukifanya!!! Yaani hata huruma ya madhara yatokanayo hakuna!!, eti kwasababu tu mtu abaki kuwa waziri.

sad!!!
 
UYU waziri wa ulinzi ni ovyo kabisa anasubiri tume itoe majibu mbona tume ya mbagala hamjatuambia ilichogundua, shame on u!!!
 
Ooo tume ije ili Mwinyi ageuze ukweli kuwa uongo. Thats how "Truth Flip in Tanzania" huyo Mwinyi mwenyewe ndiye atakuwa na input on all these"
Ukweli, wamemuandaa Mwinyi kuwa raisi na hataki kuchafuliwa jina ili awadanganye tena. Kwani Lowasa si alijiuzuru na leo si anaongoza kamati ya usalama na mambo ya nje?

images
 
Naanza kujihoji kama huyu jamaa ni mtoto wa mzee A. H. Mwinyi. kama ndivyo ina maana hakurithi hata kidogo ka-busara kutoka kwa baba yake. Mbona baba yake alijiuzulu na baadae akaja kuwa rais?
 
Hii nchi bwana acha tu maskini tunazidi nyanyasikia

Hadi mtakapojua kuwa nyie ndiyo wenye mamlaka ya kumweka mtu madarakani au kumtoa. Kwa vile bado nyie masikini mmegeuka watumwa wa watala, hakuna lolote mnaloweza kulifanya!

Very sad!
 
Naanza kujihoji kama huyu jamaa ni mtoto wa mzee A. H. Mwinyi. kama ndivyo ina maana hakurithi hata kidogo ka-busara kutoka kwa baba yake. Mbona baba yake alijiuzulu na baadae akaja kuwa rais?

Kujiuzulu au la kunategemea na boss. Kwa dizaini ya boss tuliyenaye ambaye hajui A, B wala C ya nini anatakiwa kufanya, suala kama hilo la kujiuzulu ni ndoto za alinacha. Labda wenye mamlaka waamue kufanya kweli kama alivyofanya yule machinga wa Tunisia!
 
Nimemsikia waziri wa Ulinzi Mh Hussein Mwinyi akihojiwa na VoA swahili. Pamoja na maswali mengine ameulizwa kuhusu kuwajibika kwa kujiuzulu.
Mwinyi: Kujiuzulu kunatoka na makosa yaliyofanywa na mamla iliyoko chini ya mtu kama itadhihirika. Tusubiri tume itakayoundwa na tupate matokeo yake kwanza.

My Take:
1. Hili ni tatizo la pili kutokea. Tume ni ya nini ikiwa ile ya kwanza hatukujua nini kilifanyaka?
2. Tunajua kuwa njia rahisi ya kiongozi asiyeweza kupambanua mambo ni tume ili kutengeneza mazingira ya kutengeneza hadithi.
3. Mh Mwinyi anataka kutufanya Watanzania mbumbumbu sana.
Dhana(concept) ya kuwajibika ina maana zaidi ya moja.
a) Kuwajibika kwa makosa ya watendaji kisheria kama alivyosema yeye Mwinyi.
b) Kupisha uchunguzi halali usioingiliwa na wale wanaochunguzwa
c) Kuonyesha machungu au kutoridhika kwa kile kilichotokea, na hapa ni vifo huku
kiongozi husika akiwa na dhamana.(sympath)

Zote (a), (b), (c) zinamgusa Mh Mwinyi moja kwa moja. Wakati leo kuna watu wanamisiba mizito majumbani kwao, wengine wapo mahospitalini, watoto hawajui wazazi wapo wapi, mali zimeharibiwa na watu hawajui nini cha kufanya, makazi hakuna watu wapo kwa majirani, hivi kweli hata kama kifungu (a) na (b) hapo juu hakimhusu kiongozi, je kifungu (c) cha kuonyesha huruma na machungu nacho pia kiongozi hawezi kukifanya!!! Yaani hata huruma ya madhara yatokanyo hakuna!!, eti kwasababu tu mtu abaki kuwa waziri.

sad!!!


mkuu wa nchi alishaambiwa kuwa yanunuliwe mengine hayo ya mwaka 1972 yaondolewe jibu mnalijuwa!
 
Jamaa anang'ang'ania nini? Na tume ya nini wakati inaonyesha kabisa kuwa kuna uzembe ulifanyika. Huyu jamaa ana matatizo sana, milipuko yote imetokea chini yake halafu anasema eti tusubiri tume....
 
Kama yeye Mwinyi na Mwamnyange hawataki kujiuzuru, JK anatakiwa awe bold na kuwafukuza kazi leo hii na wala siyo kesho
 
Kaazi kweli! Nchi hii ni rahisi sana kuiongoza maan wananchi wake ni wapole, wakarimu nk. Tunaonyesha kukerwa na uwajibikaji wa viongozi wetu lakini kwa sababu ya upole tunaishia kusema " aaah Mungu anajuwa bwana!" Tunaendelea kuumia tuu.
Hizo tume hazileti chochote maana zinateuliwa na haohao waliowaweka sasa unategemea nini? Tume zooooote za hapa kwetu huwa si huru kabisa, zinajengwa na dhana ya kulindana.
Cha kujiuliza ni kwamba hivi ni tume gani iliyowahi kuundwa na kutoa ukweli? (Ukiondoa tume ya Richmond)
Tutabaki kuumia tuu. Hata wale wanaodhani suluhisho ni 2015 wasahau. Kura zitachakachuliwa na itaundwa tume ya kuchunguza.
Kutokana na uoga na unafiki tuliokuwa nao ya egypt hatuyawezi. Yaani pamoja na matatizo na mapungufu ya serikali yetu kuna mijitu bado inadhani tuko kwenye kampeni! Tutakufa bila kelele. Yaani huwa nakasirika sana!
 
Ooo tume ije ili Mwinyi ageuze ukweli kuwa uongo. Thats how "Truth Flip in Tanzania" huyo Mwinyi mwenyewe ndiye atakuwa na input on all these"
Ukweli, wamemuandaa Mwinyi kuwa raisi na hataki kuchafuliwa jina ili awadanganye tena. Kwani Lowasa si alijiuzuru na leo si anaongoza kamati ya usalama na mambo ya nje?

images
Yaani wanamuandaa yeye kuwa rais!!!! Wala hafai hata kidogo....
 
Nimemsikia waziri wa Ulinzi Mh Hussein Mwinyi akihojiwa na VoA swahili. Pamoja na maswali mengine ameulizwa kuhusu kuwajibika kwa kujiuzulu.
Mwinyi: Kujiuzulu kunatoka na makosa yaliyofanywa na mamla iliyoko chini ya mtu kama itadhihirika. Tusubiri tume itakayoundwa na tupate matokeo yake kwanza.

My Take:
1. Hili ni tatizo la pili kutokea. Tume ni ya nini ikiwa ile ya kwanza hatukujua nini kilifanyaka?
2. Tunajua kuwa njia rahisi ya kiongozi asiyeweza kupambanua mambo ni tume ili kutengeneza mazingira ya kutengeneza hadithi.
3. Mh Mwinyi anataka kutufanya Watanzania mbumbumbu sana.
Dhana(concept) ya kuwajibika ina maana zaidi ya moja.
a) Kuwajibika kwa makosa ya watendaji kisheria kama alivyosema yeye Mwinyi.
b) Kupisha uchunguzi halali usioingiliwa na wale wanaochunguzwa
c) Kuonyesha machungu au kutoridhika kwa kile kilichotokea, na hapa ni vifo huku
kiongozi husika akiwa na dhamana.(sympath)

Zote (a), (b), (c) zinamgusa Mh Mwinyi moja kwa moja. Wakati leo kuna watu wanamisiba mizito majumbani kwao, wengine wapo mahospitalini, watoto hawajui wazazi wapo wapi, mali zimeharibiwa na watu hawajui nini cha kufanya, makazi hakuna watu wapo kwa majirani, hivi kweli hata kama kifungu (a) na (b) hapo juu hakimhusu kiongozi, je kifungu (c) cha kuonyesha huruma na machungu nacho pia kiongozi hawezi kukifanya!!! Yaani hata huruma ya madhara yatokanyo hakuna!!, eti kwasababu tu mtu abaki kuwa waziri.

sad!!!

anajiandaa kuwa rais.

suala la kujiuzulu halipo kwenye list yake.
 
Kama yeye Mwinyi na Mwamnyange hawataki kujiuzuru, JK anatakiwa awe bold na kuwafukuza kazi leo hii na wala siyo kesho

Na Kikwete hawezi kuwafukuza kazi kwa sababu hatuna utaratibu huo, na tumetawaliwa na uswahiba sana....
 
kama watu hatutaamka nchi hii, every day the truth will be twisted to another completely different story...."a fake truth" which is expected all to understand and take it....at the expense of peoples' life, jamani...why? and for how long?
 
Back
Top Bottom