Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Taarifa za kitafiti ambazo zimeripotiwa kwenye jarida la Evolution and Human Behavior, zinaonesha kwamba, mtoto wa kike ambaye ana uelewano wa karibu sana na baba yake utotoni, akija kuwa mkubwa, bila kujua atakuja kuvutwa na mtu ambaye anafanana sura na huyo baba yake.
Baadhi ya watafiti wanasema, labda hapo ndipo mahali ambapo panachimbuka ile imani kwamba, mtu na mkewe wakiishi kwa muda mrefu huja kufanana.
Pengine siyo suala la muda mrefu, bali zaidi ni kwamba, mwanamke ambaye anafanana na mumewe ni mwanamke ambaye alipokuwa mdogo alipendwa au kuelewana sana na baba yake.
Watafiti wengi waliofanyia kazi suala hili wanasema wamegundua kwamba, mtoto wa kike ambaye hakuwa na uelewano mzuri na baba yake, kwa kawaida havutwi kabisa na wanaume ambao wana sura kama ya baba yake.
Labda hii inaweza pia kuelezea ni kwa nini baadhi ya wanawake wazuri sana huolewa na wanaume ambao ni wabaya wa sura (kama jamii inavyowahukumu). Ni kwamba, inawezekana baba yake msichana alikuwa na sura nzuri na hawakuwa na uhusiano mzuri. Ni wazi, mwanamume mwenye sura ya aina ya baba yake hatamvuta. Lakini, hapa inategemea uzuri huo ulikuwaje, kwa sababu anachofuata msichana siyo uzuri au ubaya wa sura, bali sura inayofanana na ya baba yake au isiyofanana na ya baba yake.
Lakini, kama mtoto wa kike alielewana sana na baba yake ambaye ana sura mbaya kwa mujibu wa vipimo vya jamii, atajikuta akivutwa na wanaume wenye sura kama ya baba yake (mbaya) ambapo itakuwa rahisi kwake kuolewa na mmoja kati yao na siyo na wale wenye sura nzuri.
Hebu fikiria kuhusu mtoto wa kike ambaye anafanana na baba yake, halafu anaelewana sana na huyo baba.
Ina maana kwamba, atakuja kuolewa na mwanamume ambaye siyo tu kwamba, anafanana na baba yake, lakini pia ambaye anafanana naye (mwanamke). Kwa kuwa kuna idadi kubwa ya watoto wa kike wanaofanana sura na kuelewana na baba zao, ina maana ndoa za wanaofanana nazo ni nyingi. Lakini, je utafiti huu unataka kuwafundisha wale akina baba ambao jamii inawahukumu kwamba, wana sura mbaya, kutokuwa karibu na watoto wao wa kike ili kuwaepusha kuja kuolewa na wanaume wenye sura kama zao? Bila shaka hilo si lengo la utafiti huu.
Inaelezwa kwamba, suala ni yupi mzuri kwenye ubongo wa binadamu, halipangwi na wale tunaowaona, bali zaidi hupangwa na wale ambao tulikuwa na uhusiano nao wa dhati na mzuri sana tulipokuwa wadogo. Hapa, baba kwa mtoto wa kike ndivyo ilivyo.
Baadhi ya watafiti wanasema, labda hapo ndipo mahali ambapo panachimbuka ile imani kwamba, mtu na mkewe wakiishi kwa muda mrefu huja kufanana.
Pengine siyo suala la muda mrefu, bali zaidi ni kwamba, mwanamke ambaye anafanana na mumewe ni mwanamke ambaye alipokuwa mdogo alipendwa au kuelewana sana na baba yake.
Watafiti wengi waliofanyia kazi suala hili wanasema wamegundua kwamba, mtoto wa kike ambaye hakuwa na uelewano mzuri na baba yake, kwa kawaida havutwi kabisa na wanaume ambao wana sura kama ya baba yake.
Labda hii inaweza pia kuelezea ni kwa nini baadhi ya wanawake wazuri sana huolewa na wanaume ambao ni wabaya wa sura (kama jamii inavyowahukumu). Ni kwamba, inawezekana baba yake msichana alikuwa na sura nzuri na hawakuwa na uhusiano mzuri. Ni wazi, mwanamume mwenye sura ya aina ya baba yake hatamvuta. Lakini, hapa inategemea uzuri huo ulikuwaje, kwa sababu anachofuata msichana siyo uzuri au ubaya wa sura, bali sura inayofanana na ya baba yake au isiyofanana na ya baba yake.
Lakini, kama mtoto wa kike alielewana sana na baba yake ambaye ana sura mbaya kwa mujibu wa vipimo vya jamii, atajikuta akivutwa na wanaume wenye sura kama ya baba yake (mbaya) ambapo itakuwa rahisi kwake kuolewa na mmoja kati yao na siyo na wale wenye sura nzuri.
Hebu fikiria kuhusu mtoto wa kike ambaye anafanana na baba yake, halafu anaelewana sana na huyo baba.
Ina maana kwamba, atakuja kuolewa na mwanamume ambaye siyo tu kwamba, anafanana na baba yake, lakini pia ambaye anafanana naye (mwanamke). Kwa kuwa kuna idadi kubwa ya watoto wa kike wanaofanana sura na kuelewana na baba zao, ina maana ndoa za wanaofanana nazo ni nyingi. Lakini, je utafiti huu unataka kuwafundisha wale akina baba ambao jamii inawahukumu kwamba, wana sura mbaya, kutokuwa karibu na watoto wao wa kike ili kuwaepusha kuja kuolewa na wanaume wenye sura kama zao? Bila shaka hilo si lengo la utafiti huu.
Inaelezwa kwamba, suala ni yupi mzuri kwenye ubongo wa binadamu, halipangwi na wale tunaowaona, bali zaidi hupangwa na wale ambao tulikuwa na uhusiano nao wa dhati na mzuri sana tulipokuwa wadogo. Hapa, baba kwa mtoto wa kike ndivyo ilivyo.