ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Wakati Serikali ikijua kuwa mwaka huu ilijipanga kusherehekea miaka 50 ya uhuru kwa kishindo, maandalizi hayo hayakuwekwa kwenye bajeti inayoishia mwezi juni 2011. Cha kusikitisha, wakati Bunge liliidhinisha bajeti iliyoombwa na serikali kutumika kwa shughuli za maendeleo, Serikali imwitisha toka ktk bajeti za Wizara na taasisi nyingine za umma fedha nyingi ili ziweze kutumika katika maandalizi ya sherehe za uhuru. Maaumuzi haya yanafanyika ktk hali ambayo aijulikani iwapo kibali cha Bunge kimetolewa ili fedha hizo zitumike nje ya malengo yaliyoidhinishwa awali. Pengine ktk mazingira haya ya nchi kukosa huduma muhimu za jamii kma maji, barabara, shule, zahanati, waalimu, vitendea kazi,na ktk hali ambayo wafanyakazi wanalalamikia mishahara duni nk, kuna haja gani kufanya sherehe za mbwembwe kuazimisha matatizo? Kwa nini fedha hizo zisitumike kusaidia sehemu ya maendeleo!?