Mabasi ya 'Dar Express' yanahujumiwa?

massai

JF-Expert Member
May 2, 2011
653
137
Inaskitisha sana kuona hujuma za waziwazi zinazofanywa na mafisadi kuhujumu juhudi binafsi za wazawa katika shughuli nzima za kimaendeleo kama kinachoendelea kwenye mabasi ya Dar Express.

Angalizo kwa hujuma anyofanyiwa mmiliki wa hayo magari ni kuwa watu wanaelewa kuwa ni mchezo mbaya anafanyiwa huyo bwana na anaefanya hayo yatajulikana tu kwani kaskazini watu huku wanachukia majungu kuliko kitu chochote kile,hayo magari yenu mmnayoleta mtapanda wenyewe na familia zenu.
 
Siasa za chuki hizi, wakina Nape wanataka wote tuwe CCM. Bado naikumbuka kauli ya Sumaye alipowaambia wafanyabiashara wakitaka mambo yao yaende "vizuri" wawe CCM... Lakini yana mwisho haya!!!
 
Tujuze hizo hujuma kwa sababu wengine kama mimi nimeachwa nja panda
wewe kama ni mfuatiliaji habari kwenye vyombo vya habari kama mitandao,tv,radio na vyanzo vingine vya habari kuna mpango unasukwa wa kuleta magari ya kusafirisha abiria ya mafisadi flani,sasa ushindani mkubwa wa kibiashara kwa usafiri wa arusha to dar huyu jamaa wa dar express huduma zake zimevutia watu wengi wanaofanya safari kwenye njia hiyo.lini umesikia hayo magari yamesababisha ajali kubwa kama hyo mengine ambayo kilakukicha huachikusikia yamesababisha ajali,japo kua hakuna anaeweza kutabiri ajali au kupenda litokee,au kutokupata ajali ni ujanja,simaanishi hivyo ila tahadhari inatakiwa ichukuliwe mapema,kivipi.....mfano kuwa na magari yenye standard inayokubalika kimataifa,angalia mabasi ya dar express sio ya kuunga unga kama hayo mengi yaliopo barabarani,angalia madereva wake kuanzia mavazi mpaka muonekano wa mtu,wewe kama ni mlevi na mla mirungi na ulevi wowote pale kazi hupati ndugu yangu,angalia madereva wa magari mengine unawakuta wapo rufly na uhuni usio na mpango barabarani.ustaarabu kwa ujumla pale dar express ni standard yaani unaokidhi haja.
 
spika amewekeza mabasi 8 ktk kampuni ya supafeo,nahisi anajenga mazingira ya kuingia njia ya DAR ARUSHA. vigogo wengine wamewekeza katika usafiri wa mabasi,
ukweli ni kwamba DAr express ni professional bus service.hawawezi kuwashinda on level playing field wanatumia njia za kihuni.kitu kizuri watu wa njia ya Arusha ni werefu na makini ,wanawajua magamba na mbinu zao,hivyo basi hawawezi kutubadilisha tusitumie bus la DAR EXpress.
wabadili mbinu
 
Nimepishana na basi la Dar Express maeneo ya korogwe leo likiwa na abiria linaonekana linatokea maeneo ya uko kaskazini. Je yamefunguliwa au limeibia? Au mnaoendelea kuandika taarifa hii hamjui kinachoendelea?
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Watashanga hizo chache zilizobaki zitavyopiga mzigo kipindi hii ya sikukuu..
Wataona aibu wenyewe.
Kwa Bwana Yesu Kila Goti Litapigwa
 
Watashanga hizo chache zilizobaki zitavyopiga mzigo kipindi hii ya sikukuu..
Wataona aibu wenyewe.
Kwa Bwana Yesu Kila Goti Litapigwa
kati ya kampuni zenye uzoefu wa muda mrefu,usalama na uhakika ni Dar Express sasa kutuhamisha mawazo labda hayo mabasi yao watuchaji nauli ya 500/= dar-arusha
 
Nashanga Dar Xpress bado wako barabarani kama kawaida pamoja na kufungiwa, kulikoni?
 
Nashanga Dar Xpress bado wako barabarani kama kawaida pamoja na kufungiwa, kulikoni?


Mkuu, Mabasi yaliyofungiwa ni 14 tu. Dar Express wana mabasi zaidi ya 20. Watu wengine wameshkilia mtazamo wa hujuma dhidi ya Dar express bila kufanya hata kautafiti kadogo tu. Sio siri, kama wewe ni mtumiaji wa mara kwa mara wa mabasi ya Dar Express, utakuwa umegundua kuwa ubora wa huduma ya baadhi ya mabasi hayo imeshuka sana katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Mimi ni mteja mzuri tu wa kampuni hii. Huwa ninapanda Dar Express walau mara mbili kila mwezi( Dar- Arusha, Arusha -Dar). Katika safari zangu mbili zilizopita, safari yetu iliishia njiani - kisa ubovu wa gari. Tumetoka Dar, kufika chalinze gari ikaanza kuvuja oil sana. Jamaa wakapambana nayo ikatulia. Tulipofika mombo( Mkumbara?), bodi ikakatika na kulalia tairi za nyuma. Hapo ikawa mwisho wa safari yetu. Sikukata tamaa, nikaunga unga safari hadi Arusha. Niliopomaliza shughuli zangu nikaamua kurudi Dar kwa kutumia tena Dar Express. Njiani pancha mara tatu. Tukafika mahali, gari ikienda spidi zaidi ya 80, inayumba sana. haya mambo hayakuwepo siku za nyuma! Isitoshe, kuna baadhi ya madereva wao ni wakorofi mno. mmoja alikuwa akienda kwa kasi sana. Abiria tukapiga kelele. Akapunguza mwendo, akawa anatembea spidi ya kilomota 40 kwa saa- kutoka Segera hadi chalinze!

Ushauri kwangu kwa mzee Mremi: Ajitahidi kudumisha viwango vya ubora alivyoanza navyo; Awalipe madereva wake vizuri na aweke mfumo mzuri wa kufuatilia maoni kutoka kwa wateja wake.
 
Mkuu, Mabasi yaliyofungiwa ni 14 tu. Dar Express wana mabasi zaidi ya 20. Watu wengine wameshkilia mtazamo wa hujuma dhidi ya Dar express bila kufanya hata kautafiti kadogo tu. Sio siri, kama wewe ni mtumiaji wa mara kwa mara wa mabasi ya Dar Express, utakuwa umegundua kuwa ubora wa huduma ya baadhi ya mabasi hayo imeshuka sana katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Mimi ni mteja mzuri tu wa kampuni hii. Huwa ninapanda Dar Express walau mara mbili kila mwezi( Dar- Arusha, Arusha -Dar). Katika safari zangu mbili zilizopita, safari yetu iliishia njiani - kisa ubovu wa gari. Tumetoka Dar, kufika chalinze gari ikaanza kuvuja oil sana. Jamaa wakapambana nayo ikatulia. Tulipofika mombo( Mkumbara?), bodi ikakatika na kulalia tairi za nyuma. Hapo ikawa mwisho wa safari yetu. Sikukata tamaa, nikaunga unga safari hadi Arusha. Niliopomaliza shughuli zangu nikaamua kurudi Dar kwa kutumia tena Dar Express. Njiani pancha mara tatu. Tukafika mahali, gari ikienda spidi zaidi ya 80, inayumba sana. haya mambo hayakuwepo siku za nyuma! Isitoshe, kuna baadhi ya madereva wao ni wakorofi mno. mmoja alikuwa akienda kwa kasi sana. Abiria tukapiga kelele. Akapunguza mwendo, akawa anatembea spidi ya kilomota 40 kwa saa- kutoka Segera hadi chalinze!

Ushauri kwangu kwa mzee Mremi: Ajitahidi kudumisha viwango vya ubora alivyoanza navyo; Awalipe madereva wake vizuri na aweke mfumo mzuri wa kufuatilia maoni kutoka kwa wateja wake.
Upo sahihi sana mkuu, yapata miaka miwili iliyopita niliwahi kusafiri na Dar Express lakini waliniudhi kiasi ambacho niliapa sitarudia tena kupanda basi hilo. Kuanzia hapo nimekuwa nikipanda Kilimanjaro Express mpaka leo na katika safari zangu mara nyingi nimeshuhudia magari mengi ya Dar Express yamekufa njiani.
 
Back
Top Bottom