Mabango ya CCM... Milions of US$

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilipoanzishwa mwaka 1977 kilikuwa chama cha wakulima na wafanyakazi (chama cha watu wa vijijini na mjini). Na wengi wetu tulifanikiwa kupata elimu na huduma zingine za jamii bila ubaguzi kutokana na sera zake zilizolenga Watanzania wote. Hapa nasemea CCM iliyokuwa chini ya uongozi wa Mwalimu Julius Nyerere.

Baada ya Mwalimu, kimekuwa chama cha matajiri tu huku kikiendelea kuwatumia wakulima na watu maskini kupata kura za kukifanya kiendelee kuongoza serikali. Nasema hivi kwa kuangalia jinsi CCM kinavyotumia fedha kwa mambo ambayo hayaleti maendeleo kwa jamii. Mfano, nikiangalia mabango ya kukitangaza chama hiki hapa Dar es Salaam, hela yake ingeweza kuleta mabadiliko katika maisha ya Watnzania walio wengi. Yaani chama kinajitangaza utafikiri kimeanza leo kwa kuweka mabango kila sehemu na yenye thamani ya mamilioni ya hela? Na hii ni Dar es Salaam tu sijui mikoa mingine hali ikoje. Nimekuwa nikijiuliza: je, ni kweli CCM hakijulikani kiasi cha kuweza kuweka mabango ambayo naamini ni mamilioni ya hela karibu kila sehemu ya mji wa Dar es Salaam au ni kutaka kuonesha kuwa ni chama cha watu wenye uwezo kifedha na hivyo wanaweza kutumia fedha wanazopata jinsi wanavyopenda? Nadhani hata waangalizi wa uchaguzi kutoka nje watashangaa kwa nini tuendelee kuomba misaada kama tunatumia fedha hovyohovyo kiasi hicho! Wasiposhangaa nitawashagaa mimi.

Utawezaje kugharimia mabango yote hayo halafu baadaye uende tena kuomba fedha za maendeleo kwa wafadhili? Na matumizi mabaya ye fedha za umma ndiyo sababu inayoifanya CCM iamini huduma za afya na elimu bure au kuondoa kodi kwenye vifaa vya ujenzi haviwezekani. Lakini vyama shindani vinavyosema huduma hizo zitatolewa bure zinatumia takwimu na vyanzo vya kuingiza fedha kama serikali ya CCM inavyofanya.

Yaani, kwa bajeti ya serikali ya CCM yenye matumizi makubwa yanayotafunwa zaidi na vigogo, huduma za afya na elimu bure haziwezekani! Lakini chama chenye sera za kusimamia vizuri vyanzo vya mapato na matumizi ya serikali, huduma muhimu za jamii kutolewa bure inawezekana. Kenya, kwa mfano, wameonesha mfano huo upande wa elimu licha ya kwamba hawana raslimali (vyanzo vya mapato) nyingi kama ilivyo Tanzania.

Ni suala la utashi wa kisiasa na siyo kutowezekana. Kwa hiyo, mabango ambayo CCM imeweza kuweka karibu kila kona ya jiji la Dar es Salaam, inaonesha wazi, CCM hawawezi kutumia raslimali vizuri ili kuleta maendeleo bali kufuja mali kwa matumizi mabaya. Haya matumizi mabaya ya fedha yamewapofusha kiasi cha kuona kwamba haiwezekani kupunguza hayo matumizi ili kuleta maendeleo zaidi. Vyama shindani vimekuwa vikitoa bajeti mbadala bungeni kuonesha jnsi gani inawezekana kuleta maendeleo zaidi ya watu na vitu.

Hata walioibua ufisadi ni vyama shindani na siyo chama kinachoongoza serikali kwa sasa licha ya kwamba walipingwa vikali kuwa ni habari za uongo! Isingekuwa vyama shindani sasa hivi zingekuwa zimetafunwa fedha nyingi sana bila kujulikana. Jamani Watanzania wenzangu tulete mabadiliko na tusikubali kuendelea kudanganywa kuwa viongozi wa CCM wana uzoefu kuliko wa vyama vingine na wanachokisema ni kweli kabisa na kile kinachosemwa na viongozi wa vyama shindani si kweli.
 
Hiyo ni bonge ya observation mkuu. Nawashangaa wanajitundika nchi nzima. Kama ningekuwa mshauri wa maswala ya kampeni kwa hicho chama, ningewashauri hiyo bajeti yao ya mabango, wheel covers, kofia na mashati waielekeze kwenye huduma muhimu.

Yaani wanatundika mabango moja likiwa na thamani zaidi ya Milioni wakati wanafunzi wanakaa chini?? Hospitali hazina hata maji? Jamani!!! hiviii.... mnatumia akili au matope? Mnadhihirisha upumbavu wenu kwa wananchi hata walio masikini sasa. Badala ya kuwasaidia nyie mnaendekeza show off.

Mwaka huu mnalo!
 
kampeni za mwaka huu zina mambo ....mabango mji mzima ........yaani nasikia yameagizwa canada kwa mamilion ya dola........kazi kwelikweli......hakuna hata moja la wapinzani...hapa kuna fair play kweli??

kila mwezi ccm inachota ruzuku milioni 2000, cuf milioni 160 na chadem milioni 61 tu. Bado zipo taarifa kuwa picha zimetengenezwa kwa fedha za serikali kama ambavyo invoice kutka canda ilitumwa ikulu kwa salbva rwetemamu badala yusuph makamba; na hadi leo hii abrahamna kinana hajajitokeza kujibu tuhuma hizi kama ambavyo alifanya wakati wa tuhuma za m=ndege ya mama salama kikwete.
 
Kuna bango Moja la Mwalimu J. K. Nyerere (Tumuenzi Mwalimu Nyerere ) lipo pale Boma karibu na Mwalimu house limedondoka chini kwa uchakavu wameshindwa kulirudishia, ila ya Mkuu wa kaya mpaka miti inakatwa ili yaonekane.

Wana JF, tuanzishe harambee kukusanya hela za kukarabati bango la kipenzi chetu Mwalimu Nyerere!! Mwasemaje?
 
CHADEMA kukosa picha za kutosha na hata mabango ni suala lao,bajeti yao hairuhusu.
CCM kama chama kina miradi yake,ruzuku kubwa kuliko CHADEMA,UDP au APPT-Maendeleo.
Hivyo kuwa na mabango mengi maana yake bajeti inaruhusu na Chadema kutokuwa na mabango mengi maana yake bajeti yao finyu,inawatosha kununulia tu combat!.
Kweli nyie mnapesa nyingi saaana mpaka nchi inaendelea kwa kasi ya ajabu, kwanini hamtumii akili hiyo katika uzalishaji na kuiendeleza nchi!
aaaaaah! ondoa upuuzi wako hapa naishia kuwa na hasira tuu!
 
Hivi mtu unaweza kupiga kura kwa kuangalia bango? Hata mashindano ya Ma miss yameishaacha upuuzi kuangalia wa sura za watu. Its the credibility which matters!
 
Hivi mtu unaweza kupiga kura kwa kuangalia bango? Hata mashindano ya Ma miss yameishaacha upuuzi kuangalia wa sura za watu. Its the credibility which matters!

Bullet, uchaguzi ni credibility sawa, lakini unawafikia vipi watu ndio tatizo, CCM imefanikiwa sana katika njia za kuwafikia watu katika chaguzi zote zilizopita, tukiacha ubishi usiokuwa na maana nadhani chama kitakacho wafikia watu kama CCM kinaweza kufurukuta( kama unakumbuka NCCR- Mageuzi walisaidiwa sana na Mrema kuwafikia hasa publicity aliyoipata na coverage). Ningekuwa strategist wa CHADEMA this time ningepata ujiko sana maana CCM imetumia njia ambazo hata CHADEMA inaweza kuzi afford na ku invent nyingine za gharama nafuu.
 
Kampeni za mwaka huu zina mambo ....mabango mji mzima ........yaani nasikia yameagizwa canada kwa mamilion ya dola........kazi kwelikweli......hakuna hata moja la wapinzani...hapa kuna fair play kweli??

kuna lingine nimeliona hapa mitaa ya palm beach mkuu kakaa na mama m1 pembeni halafu limeandikwa UPENDO WA MAMA kwa chini limeandikwa chagua kikwete yaani sijalielewa kabisaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
JK ana sifa za kipekee sana....chache kati ya hizo ni kwamba, anajulikana, si Tanzania na Afrika tu, bali ni dunia nzima! Alikua rais wa kwanza wa Afrika kumtembelea Barack Obama, amekua mgombea wa CCM mwenye mvuto na aliyepata kura nyingi zaidi ktk kipindi hiki cha vyama vingi...amekua ni mtu wa watu, akikumbukwa enzi za uwaziri kwa kuhudhuria matamasha, mashindano ya walimbwende n.k bila kujibagua na watu wa kawaida...amemleta Maximo, Tz ikajulikana zaidi kwenye soka...amewapatanisha Raila na Kibaki nuru ikachanua Kenya..amepeleka jeshi Commoro amani ikapatikana...amefanya ziara wizara zooote alipopata urais, kitu mabacho hakijawahi kutokea kabla...ametuma mawaziri mikoani kusifia bajeti yake ya mwaka jana...amemteua Makamba, katibu mkuu wa aina yake ambaye utendaji wake katika chama ni wa kipekee kabisa..nikiendelea kuandika sifa zake hapa,hakika kurasa haitatosha.............SASA SWALI NI JE?????

>>KUNA HAJA YA KUWA NA MABANGO YOTE HAYA YA KAMPENI?????

Ni upuuzi tu, wangeweza kufanya mambo mengine kwa gharama hizo za mabango, lakini kama kawaida yao, ni KUFISADI tu kwa kwenda mbele 10% everywhere!!
 
Hebu tusubiri tuone jinsi watakavyo account fedha za matumizi ya mabango hayo yaliyozagaa nchi nzima. NEC itafungwa kamba wasipokuwa makini.
 
Ni upuuzi tu, wangeweza kufanya mambo mengine kwa gharama hizo za mabango, lakini kama kawaida yao, ni KUFISADI tu kwa kwenda mbele 10% everywhere!!

tutajua punde upuuzi upi, kulalamika au kufanya.
 
Kampeni za mwaka huu zina mambo ....mabango mji mzima ........yaani nasikia yameagizwa canada kwa mamilion ya dola........kazi kwelikweli......hakuna hata moja la wapinzani...hapa kuna fair play kweli??
What do you think about escrow saga?
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom