Mabango ya CCM... Milions of US$

hahahahaaa! nilikuwa sijakupata mkuu....baby sitter indeed!

Halafu wakachukua na portrait yake ya zamani wakai-photoshop na kutundika barabarani....:confused2:
Nimefeli kuelewa kabisa....
 
Yale mabango yanakera sana ila ni dalili za uoga kama unajiamini hauwezi kuweka mabango mengi kiasi hicho
 
Yale mabango yanakera sana ila ni dalili za uoga kama hakuna kujiamini hauwezi kuweka mabango mengi kiasi hicho kama unajiamini na sera zako
 
Halafu wakachukua na portrait yake ya zamani wakai-photoshop na kutundika barabarani....:confused2:
Nimefeli kuelewa kabisa....

Ile bwana nikiangalia nabakia kucheka naona huyu jamaa sasa ameamua kufanya show off
 
Afadhali hata wangeonyesha "barabara,shule,zahanati" wanazojisifu nazo eti wamejenga...
Utadhani angombea u-maarafu kila mahala sura yake...

CCM wote akili zimevia....sura ya JK si ishu kwenye uchaguzi wa sasa, Watz wameshasahau habari za utananshati kwenye siasa, ni kazi tu...after all, mwanaume hasifiwi sura, kazi tu,...
 
CHADEMA kukosa picha za kutosha na hata mabango ni suala lao,bajeti yao hairuhusu.
CCM kama chama kina miradi yake,ruzuku kubwa kuliko CHADEMA,UDP au APPT-Maendeleo.
Hivyo kuwa na mabango mengi maana yake bajeti inaruhusu na Chadema kutokuwa na mabango mengi maana yake bajeti yao finyu,inawatosha kununulia tu combat!.
 
CHADEMA kukosa picha za kutosha na hata mabango ni suala lao,bajeti yao hairuhusu.
CCM kama chama kina miradi yake,ruzuku kubwa kuliko CHADEMA,UDP au APPT-Maendeleo.
Hivyo kuwa na mabango mengi maana yake bajeti inaruhusu na Chadema kutokuwa na mabango mengi maana yake bajeti yao finyu,inawatosha kununulia tu combat!.

Wingi wa mabango mi kwagu sio ishu....tatizo langu ni contents za mabango yenyewe....sura, babysitting etc....
 
Wingi wa mabango mi kwagu sio ishu....tatizo langu ni contents za mabango yenyewe....sura, babysitting etc....
yeah... na walivyofanya mwaka huu, yaani JK amekua kama sigara mpya au vodafasta

balaah
 
mamanyere.jpg
hahahahaaa! nilikuwa sijakupata mkuu....baby sitter indeed!
 
Aya za Ayah

Kwa Waziri wa Mikiki na Makeke,
Uzitoni Street,
Bongo.

Mpenzi Frank,

Pole sana mpenzi! Nimesikitika sana kusikia mdogo wako alivyosumbuliwa na mwalimu hadi alilazimika kuacha shule. Yaani hawa wanaume sijui wakoje. Wanatunyanyasa, wanatutongoza weeeeeeeeeee, wanatulazimisha mapenzi, kisha mwisho wa siku tunapopata mimba au UKIMWI, wanasema ni kiherehere chetu.

Nani ana kiherehere? Au kwa sababu wasichana hao ni wadogo na hawana kura, hawana sauti, wakati wazee wazima wenye wazimu bado wana kura muhimu. Inakera, mpenzi inakera. Kwa hiyo mpe mdogo wako pole kubwa sana kutoka kwangu, na umpige yule mwalimu mateke matatu yenye jina la Hidaya ukimwona.

Mzima lakini sweetee wangu? Mnaendeleaje huko? Mmeshaahidiwa pipi ngapi mkimchagua huyu au yule? Ni barabara zile ambazo ziliahidiwa safari iliyopita? Uwanja wa ndege? Chuo Kikuu? Shamba la pesa (maana siku hizi nasikia wamevumbua mti unaotoa manoti badala ya matunda)? Godi la almasi kila kaya? Teh teh teh!

Mwaka huu ni senema ya bure kwelikweli. Bila shaka utakuwa tajiri kutokana na ahadi zote hizo na tutaweza kuoana hatimaye. Labda waahidi wapenzi wote watapewa mchango wa harusi.

Mimi mzima na bahati nzuri bosi hajataka niende huko kwenye jimbo lake kwa sasa, sijui amekingwa vya kutosha na mganga wake maana hirizi nilizomkuta nazo siku moja akibugia supu yake ya asubuhi zilitisha, potelea mbali nazi zote zilizovunjwa mlangoni. Nadhani wachuuzi wa nazi mwaka huu wana soko zuri kweli.

Na kwa kuwa Mama Bosi naye yuko na mzee kwenye kampeni, mimi Hidaya napata nafasi ya kuangalia luninga na kusikiliza mijadala na midahalo ya watu. Laiti ningeweza kusikiliza pande zote lakini ndiyo hivyo tena. Naona chama kilekile ni kama mwalimu wetu mkuu ambaye hakutaka kushiriki baraza la shule eti sisi ni watoto na hawezi kubishana na watoto. Watamwambia nini? Matokeo yake alisababisha mgomo maana hakuwa tayari kueleza kwa nini anafanya hiki au kile.

Lakini wiki hii nimemkumbuka sana yule fyatu wako Makengeza, na kulinganisha na hali ya mdogo wako. Unakumbuka wakati anaandika kuhusu masuala ya UKIMWI na vijana aliwahi kusema kwamba watu wanapoteza pesa kwelikweli.

Haya mabango makuuuuuuuuubwa nani anayasoma? Tena mabango yenye amri, bila taarifa, bila maelezo, mabango ya kutuambia tuwe na tabia hii au ile. Wangapi wanabadili tabia kwa njia hiyo? Basi Makengeza kasema kwa gharama ya yale mabango matano tu au kumi wangeweza kujenga kituo cha vijana, kisha wakitaka kuandika upuuzi wao wote kwenye kuta za kituo cha vijana, poa, lakini angalau vijana wangekuwa na mahali pao pa kukutana, kufundishana, kujipanga, kupata burdani na kuanzisha miradi yao. Kwa njia hiyo wangeweza kubadili maisha yao kwa sababu fursa ipo ya kuweza kufanya hivyo.

Sasa Makengeza kasema vile wakati mabango yale ya UKIMWI hayakuwa mengi sana. Je hali ya sasa na siasa ambapo mabango yameota kuliko uyoga. Kila unapogeuka bango. Na kama yale ya UKIMWI hayatuelezi chochote. Ni sura si sera. Sura, sura ,sura, sura, sura, sura! Sasa kwa nini nipende sura hiyo na si ile?

Kuna vigezo gani zaidi ya kutuaminisha kwamba huyu ni muungwana zaidi. Kwani nchi inaendeshwa na uungwana tu?

Hapo kwa kweli nilicheka kumsikia jamaa akiongelea bango moja linaloonyesha mama akisaidiwa na ndoo yake ya maji kichwani. Jamaa akasema hii peke yake inatosha kutomchagua yule. Suala si uungwana wake wa kumsaidia mama, suala ni kwa nini huyu mama bado analazimishwa kubeba ndoo baada ya miaka yote hii.

Na kweli mpenzi. Tunaona wachache wanazidi kuneemeka, tunasikia wakubwa wanavyojipatia marupurupu yasiyoisha wakati sisi tunabaki na marapurapu yetu. Sasa kumsaidia mama mmoja na ndoo yake kutasaidia nini? Tunachohitaji ni marupurupu vijijini, au hata kule kwako mjini ambapo ajira ya vijana ni kusaka maji tu. Na shule zetu vilevile n.k. Kama hela zote za anasa za wachache zipo, kwa nini bado tu maskini hivyo?

Na hapo bado narudi kwenye viherehere vyetu sisi wasichana. Wacha mambo ya kusumbuliwa na wanaume kila mahali, shuleni, sokoni, barabarani, hata nyumbani (na jirani) na hospitalini (tangu lini mtu ashikwe matiti kupima kama ana malaria?).

Katika mazingira ya sasa, msichana ana matumaini gani ya maisha, au ana mambo gani ya kumpa uwezo wa kujiendeleza? Wagombea wanamjali na hali yake au wanamdhihaki bila haki? Kwa kweli hii ndiyo kigezo changu nimchague nani au nimkatae nani.

Nashangaa kwa nini wanasiasa wanapenda kusema bila kusoma. Juzi niliwasikia wakielezea jaribio walilolifanya huko Kenya. Sehemu moja waliendesha mafunzo kuhusu UKIMWI na mimba za utotoni kwa nguvu kabisa. Walimu wakafundisha hadi wakawa weusi tiiii! Lakini mwisho wa siku, hakuna badiliko lolote lililotokea. Ngono iliendelea vilevile na mimba zikaendelea vilevile pia.

Lakini sehemu nyingine waliwapa wasichana sare ya shule. Sare ya shule tu, si kalamu, si daftari, si dawati, sare ya shule tu. Idadi ya wasichana walioacha shule ikapungua kweli, na mimba zikapungua pia. Mimba zilipungua na yule jamaa alikuwa anasema kwamba ni kwa sababu matumaini na kujiamini kwa wasichana kuliongezeka ndiyo maana hata tabia yao, viherehere vyao, vilibadilika. Hebu fikiria wangeongeza mambo mengine pia.

Niliposikia maelezo hayo na kufananisha na shule yetu ya kata kule kijijini nilijisikia kulia kabisa. Shule haina madawati, haina walimu, haina vitabu, kwa nini msichana asishikwe na kiherehere, hasa hawa mbwa dume wote wakimwandama na viherehere vyao. Yule msichana anayesema hadanganyiki ana bahati kweli maana akishatamka ‘sidanganyiki’ ni kama hirizi, wanaume wanarudi nyuma badala ya kumshawishi zaidi, au kumtukana au kufanya mpango wa kumbaka.

Hii ndiyo hali halisi jamani siyo viherehere vyetu. Kama msichana nasikitika kweli kueleweka vibaya namna hiyo maana kama shida ni viherehere tu, basi hakuna haja ya kuleta mabadiliko katika jamii. Lakini kama hali ya wasichana huathirika na hali ya jamii yake, shule mbovu, walimu watongozaji, na wanaume wengine wote, ukosefu wa ulinzi wa wasichana katika jamii, ukosefu wa njia zingine za kujikimu, wazazi kutegemea vijisenti vya msichana na ‘kiherehere’ chake na kadhalika, lazima tuwe na mabadiliko, tuwe na mapinduzi inayowajali vijana hasa sisi vijana wa kike. Lakini nani anatutetea?

Ndipo hapo narudi kwenye mabango yote hayo. Najiuliza haya mabango yote yametumia hela kiasi gani? Na hizi hela kweli zingetumika kujenga vituo vya vijana kila mahali, mbona vijana wangeweza kufanya mengi.

Lakini naona wanasiasa wanaona bora kutuhonga na vijisenti tuandamane kwa niaba yao, kutuhubiria na mabango tumchague nani na kisha kutuacha katika lindi lilelile ya ufukara. Kisha watafurahi kutulaumu tena na viherehere vyetu. Aaaaa!

Akupendaye daima dumu dume langu lisilodumazwa na mfumo dume.

Hidaya

Raia Mwema - Muungwana ni Vitendo
 
mabango ya Sura kwani we hujui kuwa ni handsome? Sura yake Inauzika bwana hatuna haja yakuandika tutakayoyafanya ila kutoa sura ya handsome wetu!
 
mabango ya Sura kwani we hujui kuwa ni handsome? Sura yake Inauzika bwana hatuna haja yakuandika tutakayoyafanya ila kutoa sura ya handsome wetu!

Mbona hayo mabango yenu yasiyokuwa na sura na yenye sera hatuyaoni? :tonguez:
 
Mabango inawezekana hayakughalimu chochote. So hata yakiwekwa kila kitanda na mawe barabarani si tatizo.
 
mabango ya sisiem ni kama vile wanamtafutia mke mwingine kikwete...! na sio urais..!

sisi tunataka tuone mabango ya kionyesha miradi mikubwa aliofanya katika kipindi cha kwanza badala ya SURA YAKE...! kwani nani haijui sura ya kikwete...????

kampeini maneja wa SISIEM HOVYOOOOOOOO....!

hiyo sura imeleta matatizo tu katika nchi hii..! mfumuko wa bei juuuuuuuuuuu,

exchange rate wala usiseme..! 1520 kwa dola..!! agiza gari uone moto wake..!

sura inafaa kwa kazi za USHENGA,,...! period!
 
But Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. JK ni handsome, ndiyo maana Dr, Yahya alisema ni mwanamke. Na yeye mwenyewe (Jk) anakubaliana kwa sababu hakuwahi kukanusha!!!!!!
:llama:
 
Kumbe hata mimi nikiphotoshop picha kibao nikiwa na wanyama mbalimbali naweza kuitwa "mtu wa wanyama"..teh teh
 
Ingelikuwa mabango yanaashiria uwingi kura basi kikwete amesha washinda wapinzani wake.
Mabango na picha za Kikwete yamekuwa mengi barabarani na mitaani hadi yamekifu. Ajabu hata alipogombea kwa mara ya kwanza 2005 mabango yake hayakuwa mengi kihivyo! hii ni dalili ya nini? uwoga? mabango yote haya ya nini? Utendaji mzuri wa mtu ndiyo mabango yake siyo haya yaliyoagizwa Canada na Salva. matendo ya mtu na utendaji uliotukuka ndiyo mabango bora na tena yanaongea yana sauti.

Mbona utendaji kazi wa John Pombe magufuli unazungumza mpaka leo pamoja na kuwekwa kwenye wizara isiyosikikamara kwa mara kama aliyokuwepo kwanza. Dr Slaa mabango yake ni utendaji wake wa kazi.
 
Back
Top Bottom