mangikule
JF-Expert Member
- Jun 11, 2012
- 6,054
- 5,432
Are you serious! or A BIG JOKE?!!Ni pendekezo tu wakuu....nimekaa nikatafakari mazuri aliofanya raisi wetu KIkwete kweli nimeona ni bora aongezewe kipindi kingine amalizie juhudi zake....
Sasa naangalia barabara lami nzuri maji yanatoka majumbani 24 hrs umeme wa uhakika japo na majungu yenu lakini wananchi tunafaidika bora kidogo kuliko kukosa.....
Angalia shule nyingi sio kama zamani.....watoto wanapata elimu bora ya uhakika angalia wahitimu wa shahada hapa nchini wako very clean and smart shukrani Raisi kikwete kwa chuo kikuu dodoma.....
Huduma za afya ni bora tena hapa anafaa kupongezwa jamani.....zamani enzi ya nyerere hakukuwa hivi....zahanati moja kilomita 50 ndio unaikuta..leo hi hospitali nyingi za kumwaga dawa zipo za kutosha kwa kweli anafaa kuongezewa kiindi kingine.....
Amani kwa kweli tanzania ya kikwete imejaa telee sio kama enzi ya mwalimu...si mnakumbuka tulienda vitani enzi ya mwalimu....mkapa akaua wenzetu mwembechai....sasa jamani tutake nini juu ya huyu baba yetu KIkwete? zaidi ya kumuongezea kipindi kingine amalizie mazuri tunayoyaonaa......
Wote mmeshuhudia barabara za lami alizofungua...angalia nchi yetu tajiri raisi wetu kwa sasa juu ya mafuta nma gesi kaweka mkakati murua kufanikisha tunafaidika na rasilimali zetu.....
Kupitia kwenye mikono yake bora ya utawala wake na uongozi mzuri raisi wetu ametuletea vijana wachapa kazi kama Nape na wasomi vijana kama Adam malima.....angalia safu yake ya uwaziri ilivyosheheni watu makini....wizara ya fedha yupo mtu makini Dkt. William Mgimwa Ph.D msomi,muadirifu mwenye kuchapa kazi....wizarani sasa kunakwenda vizuri....Wizara ya elimu wapo watu makini Mr Mulugo acheni majungu yenu ila ni mtu makini na ataifikisha elimu yetu pazuri.....sidhani kama manjungu na wivu wenu vitatufikisha pazuri....tumpe ushirikiano raisi wetu kwa kweli kama ikwekzekana aongezewe kipindi kingine atuongoze.....
Mungu mbariki raisi wetu Dr Kikwete
Mungu ibariki Tanzania