Mabadiliko ya Katiba: Kikwete aongezewe muda wa miaka mitano

Japo umemtania mh raisi kwa kutoa mlolongo wa sifa, umetumia nafasi kupunguza uchovu kwa watu. Maendeleo ni kitu endelevu, hayafiki mwisho, hivo hakuna mtu wa kuyakamilisha, anachoweza na kutimiza sehemu yake tu mpaka anakufa hajayamaliza, labda aishi bila mipango.
 
Kila mtu ni shahidi jinsi gani nchi yetu ya Jamhuhuri ya Muungano wa Tanzania ilivyopiga hatua kubwa ya maendeleo hasa katika uongozi wa mh.Rais JK.Kwa muda mfupi nchi yetu imefanya vizuri katika nyanja zote,uchumi wetu umeimarika kwa kasi ya ajabu.Sekta za elimu,afya,kilimo,utawala bora,demokrasia na uhusiano wa kimataifa ni mafanikio ya hali ya juu ktk uongozi wa mh.Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania,ndg.Jakaya M.Kikwete.Hivyo basi katiba ijayo inapaswa iwe na kipengele cha kumuongezea muda rais aliyefanya vizuri km mh.JK ili aweze kukamilisha kazi ya kuwatumikia Watanzania.Miaka mingine 5 inatosha ili amalizie kutuletea maendeleo.Wapinzani hasa Chadema hamna chenu,chama chenyewe kinakwenda mramba.Mmeshindwa hata kutuma mwakilishi Sauz kwenye msiba wa mzee Mandela.Napenda kuwasilisha.

inaelekea unapenda sana kutukanwa
 
Iwapo katiba ingeruhusu rais Kikwete kugombea tena awamu hii, je kwa utendaji wake na utekelezaji wa ilani na ahadi zake tangu alipoingia madarakani angeweza kuibuka tena kwa ushindi urais 2015?
 
we hata std 7 sijui kama ulimaliza!! na lazima uko tandahimba,au huko uzaramoni ambapo hakuna zaidi ya ngoma na uchawi tuondokee apa na akili zako zenye kutu usojua hata kuandika

mramba=mrama
 
Iwapo katiba ingeruhusu rais Kikwete kugombea tena awamu hii, je kwa utendaji wake na utekelezaji wa ilani na ahadi zake tangu alipoingia madarakani angeweza kuibuka tena kwa ushindi urais 2015?

kwa upinzani gani uliopo mpaka umfanye asipete?
 
Unatumia nguvu nyingi kupingna na hoja ndogo sana. Dig deep kwenye issues. Nasema hivi, JK amefanya mema mengi kwa Tanzania pamoja na Changamoto za kiutawala anazokutana nazo. Kubali hoja kwa hoja, pinga hoja kwa hoja. Hayo mengine unayoyasema ukayaseme kwa wenzako mnapokuwa mnasukana nywele au mkiteka maji...

Quadratic,

Wewe ni mmoja wa Watanzania machizi walioleweshwa unga(madawa ya kulevya) na CCM.
Hili unalosema hapa haliwezekani si kwa Katiba iliyopo kwa sasa wala inayopendekezwa na Mafisadi wako CCM. Kila Awamu ni miaka 5 kwa vipindi 2 yaani 10 years.

Hata kama ni kuchakachua Katiba ili aongezewe miaka 5, kwa lipi hasa alilowatendea Watanzania? Mipango yote ya mabarabara alikuta imeshaanzishwa na Mkapa.

Kiwete is one of the weakest President ever since independece.Kama unataka aendelee kuwa Rais hamia nyumbani kwake ukawe chini ya himaya ya familia yake.

Pambaf!
 
Yaani Kikwete akiongezewa hata masaa mawili baada ya musa wake hii ncji itakuwa kam chekecheke. Wakati wa Mkapa Mh Magufuli alikuqa akitamba amejwnga barabaea km kadhaa kwa pwsa za ndani. Leo muulize anadaiwa na mataifa ya nje kiaai gani kwa ujenzi wa mita chache za baeabara?? /
 
Hapo kwenye afya.
Kama afya ingekuwa imeboreshwa asingepeleka Tezi dume lake marekani.
 
Hivi JK ameshaelewa sasa kinachoifanya Tanzania kuwa maskini? Mimi naona kuwa JK apunguziwe muda wa kukaa Ikulu, miaka 5 mingi sana! Wakati wa Serikali zilizopita JK alikuwa Waziri wa Nishati na Madini na alisaini mikataba mibovu ya madini! Pia baada ya kujua uovu uliofanywa na Serikali ya Mkapa, aliamua kuyafumbia macho na kuamua kudai kwamba "mzee (Mkapa) aachwe apumzike" kwa ufisadi aliofanya!

Tusidanganyane JK akiendelea kuwa Ikulu Tanzania itakuwa kama Somalia!
Aisee
 
Upo?
Hakuna shaka kuwa wapuuzi ni wale wanaoupinga ukweli. Hata kama una chuki binafsi na JK lakini kusema ukweli mema tunayaona.
Mradi wa mabasi yaendayo kasi umeshaanza, upo hatua ya mwanzoni
Flyovers nazo zipo mbioni...
Mnataka mfanyiwe nini watanzania??
 
Quadratic

Ulichosema ni kweli tupu,Rais JK asiongezewe tu miaka 5 bali Katiba mpya imtangaze kabisa kuwa ni Rais wa milele wa TZ kwani kaifanyia mengi sana nchi yake Tanzania

Mosi;katupa umeme wa uhakika kabisa TZ;chini ya utawala wa maulana JK kwa kweli wa TZ wanafaidi umeme wa bei rahisi tofauti na viongozi wengi waliotangulia.

Pili;hali za huduma za afya TZ ni za juu sana chini ya utawala wa JK hata ikafikia ile kadhia ya kulala chini akina mama wajawazito pale Mwananyamale,Muhimbili na karibia hospital zote za TZ sasa haipo tena

Tatu;Rais wetu JK kadhibiti sana mfumuko wa bei na hivi sasa chini ya utawala wake shupavu shilingi yetu imepanda sana bei kulinganisha na bei ya dola ya kimarekani

Nne;wakulima hivi sasa wana uhakika wa kupata bei nzuri ya mazao yao kwani JK kaimarisha sana soko la ndani na la nje kwa products zitokazo mashambani mwetu hasa alipowapa pembejeo za kisasa wakulima wa TZ

JK kaifanyia mambo mengi sana TZ na mengine nitaendelea kuyataja siku zinazokuja lkn sidhani kama itakuwa vibaya kutoa wazo langu kwenye katiba mpya imtangaze JK kama Rais wa milele wa TZ ili kuenzi mazuri aliyoyafanya kwa miaka 5 tu ya uongozi wake!
Kamwene
 
Back
Top Bottom