Maazimio ya kamati ya jumuiya ya madaktari kuhusu tamko la serikali juu ya mgomo wa madaktari

Na nyie msituchoshe! Kama vipi jifukuzisheni kazi kabisa ili tujue hatuna madaktari. Sitaki nataka kibaooooooooo!
Kwani vipi Mwita25 nani hakujui, hii wewe na serikali yako imewabana sawa sawa kuivua hii ni kazi pole!!!!!!!!! Msijifarague tekelezeni matakwa ya madaktari meupushe vifo vya watu wanyonge!!!!!!!
 
Mimi bado nasubiri tamko la serikali la kuwafukuza madaktari waliogoma, kama alivyopayuka bwana pinda akili. Au masaa 48 bado jamani?
 
Kama kuna jambo kubwa linaloweza kujitokeza ni huu mgomo kusambaa hadi kwenye sectors nyingine...Tatizo ni hawa watu kama Mgaya wa TUCTA ambao wanakomba michango ya wanachama wao wakiwemo madkaria halafu eti wanajidai kuwakana hadharani.

These have to be dealt with after this step!
kazi ya tucta ni kuratibu sherehe za mei mosi.ni kweli after this MAT watajitoa tughe.
 
Ni aibu sana kwa professional kama yeye kubadilika ghafla baada ya kuukwaa uwaziri!...Hivi alipokuwa IHI kweli alikuwa ameridhika hivi?

Mponda sio medical Dr , alikuwa anafanya kazi za "matangazo" IHI

Acha kuhadaa umma wewe. Mponda ni doctor by profession. Amefanya kazi IHRI na utendaji wake hauna mfano. Fuatilia tafiti zake uone naongelea nini.

Ebu tupe hizo tafiti au kila kitu mnawaza kuchakachua ?
 
Nimemsikiliza kwa makini sana Dk. Ulimboka kupitia Star Tv asubuhi, jamaa anafaa kuwakomboa Ma-daktari. Bwana Mponda ***** tu.
 
Madaktari nawapa tu angalizo,msikubali kabisa kuzungumza na kamati ya bunge ya huduma za jamii,maana hao ni mabingwa wa porojo tu,na jambo hili lingekuwa limeshakwisha kama tungekuwa na bunge lenye nguvu lisiloegemea itikadi ya CCM,na ndio maana walifanya njama za kukataa kuijadili taarifa ya serikali kuhusu mgomo wa madaktari,na ndio maana wabunge hao hao wameipokea taarifa iliyojaa upotoshaji,huku wakidai huduma zimerejea wakati ukweli si hivyo hali mbaya tena mbaya sana,kwa anaesoma post hii ajaribu kutembelea MNH au KCMC na maeneo kuliko na hospitali za rufaa.
wakikubali tu watakuwa wameongopewa vikali maana wao ndio wamefanya utaratibu ili kuinusuru serikali ya CCM.na kwa hal ilipofikia ni kwanini hata Rais asingekuwa ameingilia kati?na kingine mbona hawajawa na umoja kuwatetea madaktari waongezewe mshahara na madai yao mengine badala yake wanajirundikia wao.

Binafsi siamini katika kukutana na kamati ya kudumu ya bunge tena yenye wabunge wengi wa CCM kama kutaleta muafaka ulio wa kweli.
 
Juhudi zooote za rais kujiweka karibu na watu kwa kupitia matukio mbalimbali zinayeyuka kabisa na huu mgomo wa madaktari. Kama rais anapata muda wa kutembelea wagonjwa hospitalini, majumbani mwao, kufariji wafiwa na hata kuhudhuria mazishi kwa nini asijitoze wakati huu watu wanakufa Muhimbili? Washauri wake waangalie hili kwa makini. Inawezakana serikali inasoma vibaya hali hii lakini mtaani watu wengi wanaonekana kuwaunga madaktari mgomo. Itakuwa vigumu sana kuondoka kwenye hili tope kama serikali haitajishusha na kutambua kuwa jukumu la kutoa huduma za afya la serikali pekee.

Pili, kamati ya bunge kwa nini hawakuingilia kati tangu awali? Kwa nini wasubiri hadi wakiwa Dodoma ndio warudi Dar kuongea na madaktari wakati watu wanaendelea kupata shida? Pamoja na kwamba spika amekuwa aking'ang'ania kuwa bunge linaendeshwa na kanuni lakini naamini busara nayo inatakiwa. Hivi kama nchi hii ikivamiwa wakati ambao si wa bunge spika atakaa kimya mpaka muda wa bunge uwadie aende Dodoma na kutoa maelekezo? Wabunge wakiwa nje ya Dodoma akili zinawatoka? Au hawaoni hali ya Muhimbili kama dharura! Ni kanuni ipi inayokataza kamati ya bunge kumuita waziri wa afya wakati wagonjwa wanapoteza maisha?

Serikali nayo itakaa kimya hadi iende Dodoma kutoa statement kwamba tumevamiwa? Watu wanakufa Muhimbili kwa nini usubiri week nzima upande shangingi lako kwenda Dodoma kuongelea huko?
 
Nchi yetu haitawaliki tena kutokana na Uongozi mbovu. Ukisoma kwa makini madai ya madaktari utajua makosa yako ktk muundo mzima wa AFYA nchini lakini nina hakika wananchi hawako tayari kukubali ukweli kama wanavyomshabikia Lowassa arudi madarakani. Bunge linaloshindwa kuwaita viongozi wahusika wa mgomo huu bungeni kujibu ama kutafuta suluhu kwa sababu ya kanuni ambazo hazikutegemea dharura kama hii ni mfano mzuri sana kuonyesha kwamba Katiba nzima ya Tanzania inatakiwa kutazamwa Upya...

Pengine nikubali kwamba huu mgomo wa madaktari unaweza kuwa mwanzo wa anguko la CCM lakini kama kweli wamekubali kukutana na kamati ya Bunge ili wapate kuongezewa posho, bima na kadhalika wakati wananchi na watumishi wengi nchini hawana posho wala bima hizi ni mwanzo wa kuivuruga nchi kwenda bila dira, sera na ilani...

Nitarudia kusema kama daktari haridhiki na kazi au mazingira ya kazi alo ajiriwa anatakiwa kuandika barua ya kuacha kazi na atafute sehemu nyingine..Lakini hili haliwezekani kutokana na kwamba vitengo vyote vya Afya nchini vinalindwa na mfumo mmoja ambao ndio tatizo kubwa. Isipokuwa kama lilivyo swala la waziri mkuu mstaafu Lowassa, wananchi wameamua kulifumbia macho na kama kawaida yetu kutafuta mchawi mwingine hali mchawi tunaye na tunakula naye meza moja.

Mkandara sielewi kwanini kila jambo unalochangia unaltaja jina la Lowassa...Hivi nini kilimzuia huyu bwana Lowassa kujitetea bungeni na kuamua kuzira uwaziri mkuu; madaktari hawata"zira" na kuacha kazi, wana madai ya msingi na njia sahihi ni kuyadai mpaka kuhakikisha yanapatikana. dawa ya matatizo sio kuyakimbia. Mpaka hapa walipofika serikali wamefanikiwa jambo mmoja kubwa sana; kuwaonyesha watanzania kuwa serikali yao "mdebwedo". Uongozi wowote makini huupimwi kwa kutokufanya makosa; bali hupimwa ni jinsi gani inavyoshughulikia makosa yakitokea.
 
Madaktari nawapa tu angalizo,msikubali kabisa kuzungumza na kamati ya bunge ya huduma za jamii,maana hao ni mabingwa wa porojo tu,na jambo hili lingekuwa limeshakwisha kama tungekuwa na bunge lenye nguvu lisiloegemea itikadi ya CCM,na ndio maana walifanya njama za kukataa kuijadili taarifa ya serikali kuhusu mgomo wa madaktari,na ndio maana wabunge hao hao wameipokea taarifa iliyojaa upotoshaji,huku wakidai huduma zimerejea wakati ukweli si hivyo hali mbaya tena mbaya sana,kwa anaesoma post hii ajaribu kutembelea MNH au KCMC na maeneo kuliko na hospitali za rufaa.
wakikubali tu watakuwa wameongopewa vikali maana wao ndio wamefanya utaratibu ili kuinusuru serikali ya CCM.na kwa hal ilipofikia ni kwanini hata Rais asingekuwa ameingilia kati?na kingine mbona hawajawa na umoja kuwatetea madaktari waongezewe mshahara na madai yao mengine badala yake wanajirundikia wao.

Binafsi siamini katika kukutana na kamati ya kudumu ya bunge tena yenye wabunge wengi wa CCM kama kutaleta muafaka ulio wa kweli.

naskia kamati ya bunge walihongwa kupitisha ile bajeti ya wizara....
 
he is not a medical doctor..ana phd..kasoma mzumbe university..alaf akafanya phd..usiongee bila facts....tafuta cv kwa wadau...madaktari wanafahamiana sana..
 
hawa madaktari sasa nao wamekuwa wanasiasa.waseme katika madai yao ya msingi yamefanyiwa kazi waache propaganda.
 
Madaktari lazima muwe makini na hii kamati ya bunge! Kimsingi hakuna cha maana mtakacho kipata maana wabunge wote wa ccm wako njia panda kutokana na issue ya posho ya 200k. Hii imethibitika jana pale ndugai alivyoktoa nafasi ya kujadili hili jambo lakini wabunge wakataa wenyewe kuunga mkono.

Issue ya posho imewakalia vibaya sana wananshindwa waikwepe vipi. Maana wakiunga mkono hoja za madaktari, serikali itawanyima hizo posho. Lakini pia wakiunga mkono serikali, basi wananchi watawavaa wao.

Kimsingi bunge halina majibu katika mgogoro huu maana halina meno maana serikali imewatega!

Madaktari nyie endeleeni mbele na simameni imara atakayetatua madai yenu ni hawahawa serikali nasio bunge. Kamati ya bunge itakachokifanya ni kuwabembeleza mrudi kazini mikono mitupu.
Simameni palepale mtashinda!
 
tujadili uwezo wa kikwete wa kuteua viongozi,kuwasimamia na kuwachukulia hatua.hivi kweli anaweza chochote?
mbona ka-issue kadogo tu ka-madaktari kamemshinda!! je ingekua wizara!! hivi kweli huyu bwana aliwahi kua mjeshi? manake najua jeshini hakuna kuuza sura,mambo mbele.vipi yeye anakua mla-iiiini..ana nini na akina mponda wake?
 
Ni aibu sana kwa professional kama yeye kubadilika ghafla baada ya kuukwaa uwaziri!...Hivi alipokuwa IHI kweli alikuwa ameridhika hivi?
Na hiyo kamati ya kudumu ya huduma za jamii ina guts au meno kiasi gani?..Inaweza kum'summon Waziri na kumhoji kwa huo uwongo wa mchana kweupe aliolidanganya taifa kupitia Bunge letu??
Napenda kujua hayo kwanza!
Wabunge nao kenge kweli. Walikuwa wanapiga meza kama wehu wakati wanadanganywa. Magamba ndo walikuwa wanashangilia uongo toka kwa mpondwa..
 
tujadili uwezo wa kikwete wa kuteua viongozi,kuwasimamia na kuwachukulia hatua.hivi kweli anaweza chochote?
mbona ka-issue kadogo tu ka-madaktari kamemshinda!! je ingekua wizara!! hivi kweli huyu bwana aliwahi kua mjeshi? manake najua jeshini hakuna kuuza sura,mambo mbele.vipi yeye anakua mla-iiiini..ana nini na akina mponda wake?


Hivi ndo anayofanya. Baada ya kupokea mabillioni toka kwa wahisani, kwa maana wao ndo wenye nchi
 
Back
Top Bottom