Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Askofu Ruwaichi alilia na haki
Kwa upande wake, Ruwaichi ambaye ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, alisisitiza umuhimu wa Serikali na dola kutoa haki kwa umma akisema: Siyo lazima kelele ya wengi inaporindima ndiyo haki inatendeka.
Akihubiri kwenye ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Epifania, Parokia ya Bugando, Askofu Ruwaichi alisema kila mmoja anawajibika kusimamia ukweli ili kuungana na Kristo katika kutenda haki.
Alisema watendaji wa Serikali wanapaswa kujihoji ni kwa kiasi gani wanatimiza mapenzi ya Mungu katika kuwatendea wenzao haki.
Rwaichi alihoji ni mara ngapi watu waliopo katika dola wamenawa mikono yao ili kutoa haki dhidi ya wanyonge. Aliwataka kumrudia Kristo kujutia dhambi zao ili watakasike.
Alikemea tabia ya baadhi ya watu kufanya mambo kisha kuwatwisha mzigo wengine ili kuokoa roho zao na kwamba tabia hiyo ni kinyume na Kristo ambaye hakuwa kigeugeu katika uamuzi wake.
Ulimwengu wa leo umebadilika tunapofanya makosa tunatafuta njia za kuwatupia watu wengine mizigo ili kunusuru roho zetu huo siyo mfano ambao tulionyeshwa na Kristo, alisema Ruwaichi.
Mapema katika mahojiano na gazeti hili, Askofu Ruwa'ichi, alisema Watanzania wana wajibu wa kudumisha amani na kukwepa kila aina ya dalili zitakazoweza kuivuruga.
Source: Mwananchi
Kwa upande wake, Ruwaichi ambaye ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, alisisitiza umuhimu wa Serikali na dola kutoa haki kwa umma akisema: Siyo lazima kelele ya wengi inaporindima ndiyo haki inatendeka.
Akihubiri kwenye ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Epifania, Parokia ya Bugando, Askofu Ruwaichi alisema kila mmoja anawajibika kusimamia ukweli ili kuungana na Kristo katika kutenda haki.
Alisema watendaji wa Serikali wanapaswa kujihoji ni kwa kiasi gani wanatimiza mapenzi ya Mungu katika kuwatendea wenzao haki.
Rwaichi alihoji ni mara ngapi watu waliopo katika dola wamenawa mikono yao ili kutoa haki dhidi ya wanyonge. Aliwataka kumrudia Kristo kujutia dhambi zao ili watakasike.
Alikemea tabia ya baadhi ya watu kufanya mambo kisha kuwatwisha mzigo wengine ili kuokoa roho zao na kwamba tabia hiyo ni kinyume na Kristo ambaye hakuwa kigeugeu katika uamuzi wake.
Ulimwengu wa leo umebadilika tunapofanya makosa tunatafuta njia za kuwatupia watu wengine mizigo ili kunusuru roho zetu huo siyo mfano ambao tulionyeshwa na Kristo, alisema Ruwaichi.
Mapema katika mahojiano na gazeti hili, Askofu Ruwa'ichi, alisema Watanzania wana wajibu wa kudumisha amani na kukwepa kila aina ya dalili zitakazoweza kuivuruga.
Source: Mwananchi