Maaskofu mmevuna mlichopanda

Walipaswa sana kuacha ushabiki wa kisiasa tangu mwanzo wa regime hii, walipaswa wawe marefa kwa uongozi uloingia madarakani na wananchi kwa kushirikiana na wazee wenzao ndani ya chama kinachotawala(hapa wangelimsaidia mzee mwinyi na kawawa kuirejesha ccm ktk mstari baada ya minyukano ya ndani ya ccm kumpata kikwete, walilisahau hili wote kama maaskofu, wasisi wa chama na kuwaacha mtandao wakiendelea huku walioshindwa na mtandao wakiugulia pasipokujua wapi wakililie au kupata faraja... Haya tuyaonayo ni matokeo ya uzembe wa maaskofu wetu, na wazee aliowaachia kambarage jahazi la ccm kukubali kuegemea na kuacha utamaduni wa kukosoana na kuridhiana ndani ya chama na kuiweka nchi mbele....), maaskofu kama mngeifanya hii kazi vizuri sidhani kama mkuu angelithubutu kuwakoga hadharani....., sasa anapaswa na yeye aseme maana anahisi kuwa aliachiwa mzigo wa kujiponya peke yake ndani ya chama....au anawaona ni chanzo cha matatizo yake..., tafakarini ili muijenge nchi na siyo mtu. Kidumu chama cha mapinduzi

Mimi nimeipenda sana sinema aliyoicheza JK huko Mbinga mbele ya wahasham Maaskofu wakuu, Maaskofu, mapadre, Masista, balaza la walei na waumini kwa ujumla.Haya mambo yamekuwa yakitukera sana sisi waumini, kwani viongozi wetu wameendelea kujishusha na kupunguza hadhi yao mbele ya serikali. Cha kushangaza leo ni kwamba; CCT, na TEC ya leo si ile ya enzi ya utawala wa nyerere na Mwinyi, enzi hizo walikuwa na authority kweli, lakini wamejikuta wakiingizwa mkenge kwa kuwa karibu na watawala kisiasa japo wamekuwa wakifanya kimaficho lakini sisi waumini tunajua na tunaona.Hili ni fundisho kuwa viongozi wa dini wabaki kambini ili siku wanapotoka na hoja mara moja jamii ielewe na kuheshimu.Lakini aliyosema JK jamii inaweza leo kushawishika kukubali hata kama itakuwa uongo kwani wamejenga mazoea ya kuchanganya mambo.
 
Inawezekana watajwa wakawa kweli wanajihusisha na mambo hayo,lkn aliyesema hayo ndio amri jeshi mkuu wa nchi hii alishindwa nini kuwatia mbaroni au kuwataja?
Hii ni sinema kama ya CCM ya kuwataka mliowaandikia barua kuwaita na muongee nao?
Muongee nini sasa wakati majibu ya kuwapa mnayo!
Guys let's be strict on to the fact!
 
Pamoja na madawa ya kulevya tujihadhari na tabia hatarishi za viongozi wa dini kama vile ulevi, ubaguzi, ubakaji, uwizi wa mali za waumini, na hata kutembea na wake watu...tuwaangaze kwa jicho pana na jema..kwa faida yao (mbele ya Muumba) na kwa faida ya waliowaamini

Mifano ya ubakaji angalia report za maaskofu wa kikatoliki huko Ulaya ...POPE anaomba msamaha kila anakoenda..tahadharini na watoto wenu.please..kumbuka watu hawa wahajaoa...
 
Back
Top Bottom