Bill
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 8,232
- 8,429
Hatimaye Mama wa ufisadi nchini amejipambanua na kujiweka wazi kwa kila mwananchi. Katika vikao vya CC na NEC vya CCM vilivyomalizika Jumatatu 17/08/09 hakika imedhihirika mapambano dhidi ya Rushwa na Ufisadi yanayoendelea hapa nchini si kazi rahisi kwani kuna kundi kubwa lilolojipatia hati miliki ya mali ya nchi likiongozwa na kulindwa na mama yao CCM.
Siyo rahisi kuupiga vita ufisadi bila kwanza kuipiga vita CCM, kwani mama wa hawa mafisadi ni CCM, na hawa watoto ndio wanaomlisha mama yao CCM. Haiwezekani kuwapiga vita akina RA,EL na Mzee wa Vijisenti bila kumgusa mama yao CCM. Kwa upande mwingine hata ikiwa hawa mafisadi wa sasa wataondoka Mama yao yaani CCM atazaa wengine kwa maana hiyo tatizo liko palepale.
Kuukata mzizi huu wa ufisadi ni lazima kuanza na mama yao yaani CCM. CCM ni lazima iondoke sasa, imeshapoteza mwelekeo na mwelekeo wake ni dhahiri - Ufisadi.
Wito kwa Maaskofu na Masheikh
Amri ya Mungu inazuia wizi "Usiibe", CCM leo inatetea wizi. Hakika CCM nao wanashiriki wizi
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WABARIKI WATANZANIA NA VIONGOZI WAO WA KIROHO
Siyo rahisi kuupiga vita ufisadi bila kwanza kuipiga vita CCM, kwani mama wa hawa mafisadi ni CCM, na hawa watoto ndio wanaomlisha mama yao CCM. Haiwezekani kuwapiga vita akina RA,EL na Mzee wa Vijisenti bila kumgusa mama yao CCM. Kwa upande mwingine hata ikiwa hawa mafisadi wa sasa wataondoka Mama yao yaani CCM atazaa wengine kwa maana hiyo tatizo liko palepale.
Kuukata mzizi huu wa ufisadi ni lazima kuanza na mama yao yaani CCM. CCM ni lazima iondoke sasa, imeshapoteza mwelekeo na mwelekeo wake ni dhahiri - Ufisadi.
Wito kwa Maaskofu na Masheikh
- Ikiwa ninyi mnahubiri amani, upendo, uvumilivu na ustawi wa kiroho na kimwili - Haya yote hayawezekani chini ya usimamizi wa Mama wa Mafisadi yaani CCM. Hubirini habari ya ukombozi kutoka katika kundi la hawa wadharimu ili haya yote yawezekane. Hubirini na kuhamisisha waumini wenu bila ya kificho, hubirini wazi wazi waumini wenu wakikikatae Chama cha Mafisadi
- Hamasisheni waumini wenu kutokushabikia vyama bali utaifa. Chama kinaweza kufa lakini taifa letu litaendelea kuwepo hadi utimilifu wa dahari. Kwa hiyo fumbueni macho waumini wenu waache ushabiki wa kijinga kama inavyoenezwa na CCM kuwa maslahi ya chama kwanza. Hubirini maslahi ya nchi kwanza, Hakuna maana yoyote ya kutanguliza maslahi ya chama kwani hii ina maana ya kutanguliza mbele maslahi ya kundi fulani.
- Waambieni waumini wenu kuikataa CCM kwani imeshajipambanua kuwa ni kundi la mafisadi na lisislozingatia katiba ya nchi kwa malengo ya kutimiza malengo yao. Kitendo cha kumkemea spika kinadhihirisha hili na kinajaribu kurudisha nyuma vita hii ya mapambano dhidi ya ufisadi. Hamasisheni waumini waikatae CCM kwani haina agenda ya msingi ya kuwaletea maendeleo.
Amri ya Mungu inazuia wizi "Usiibe", CCM leo inatetea wizi. Hakika CCM nao wanashiriki wizi
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WABARIKI WATANZANIA NA VIONGOZI WAO WA KIROHO