Maandiko na mabandiko havitoshi

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,877
2,756
Katika kuleta mabadiliko ya kidola kuna njia tatu, kwanza ya kikatiba, pili kuingia msituni, tatu kupindua uongozi uliopo. Hakuna njia ambayo si halali hapo. Uhalali na si uhalali inategemea na upande unaohusika kwenye harakati. Kwa tz kalam imetumika sana na hakuna badiliko. Katiba imechakalia kwenye kibeti chake. Watawala wamekuwa sugu kwa kwa kauli na maandishi ya watawaliwa. Hawahisi tena, kwa maana hiyo wanahitaji namna ya kuifanya milango yao mitano ya faham kuhisi. Mifano iko mingi Afrika ila njia zao wengine ni za kishenzi. Madagascar ni mfano mzuri. Bermuda ni mfano mzuri. Hatuhitaji njia ya msituni, tunahitaji mapinduzi. Yaweza kuwa ni traditional coup au mapinduzi ya fikra. Yote yanahusika. Adui anapoingia kwenye himaya yako unamkabili kwanza ndipo unaangalia aliwezaje kuingia. Adui si lazima awe mtu. Wadudu, fikra, mazoea, woga, n.k vinahusika. Ni wakati wa mapinduzi ama tuache kuchonga domo zetu. Tunaharibu rasilimali bure; karatasi, wino, fikra, muda, n.k. Nadhani ujumbe huu ni delivered, not only sent.
 
Back
Top Bottom