Maandazi yanawamaliza Tembo Tanzania!

Mzizi wa Mbuyu

JF-Expert Member
May 15, 2009
7,312
6,770
Jamani sjui niseme ni ubunifu au uharibifu!?<br />
Imeibuka mbinu mpya inayotumiwa na majangili kuwaua tembo, na hii mbinu inatumika sana katika pori la hifadhi ya selous...<br />
Yanachukuliwa maandazi ya kutosha, kisha yanachomwa sindano ya sumu(kwa usalama naomba nisiitaje aina hiyo ya sumu)<br />
Basi, jangili huenda na maandazi hayo hadi porini na kutegesha njia ambayo anajua kabisa tembo watakuja...<br />
Kwa ugunduzi wao wa kijangili,..tembo wanapenda sana maandazi! Basi tembo wanapofika eneo hilo lenye maandazi hufakamia....na baada ya muda mfupi hufa! Jamaa wanakuja na kung,oa meno na kuondoka zao.<br />
Mbinu hii inawasumbua sana askari wetu wa maliasili kwani walizoea kusikiliza milio ya risasi ili kujua mahahali fulani kuna majangili.<br />
Hii mbinu ni mbaya sana kwani huua hata tembo wadogo wasio na meno.<br />
Tutunze maliasili zetu jamani, ubunifu wa uharibifu si jambo jema.
 
Wenzetu wa kenya huwatupia tembo nusu kaputi, tembo akilala wanakata pembe kwa msumeno baabae tembo anaamka na kuendelea na maisha- elephant with no ivory. Hii ya selou ni chiboko.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom