Maandamano ya wanaharakati wazalendo hayana taarifa za kiintelijensia?

Shansila

Senior Member
Jan 28, 2012
189
36
Kikundi cha watanzania wanaojiita wanaharakati wazalendo leo kimeitisha mkutano na waandishi wa habari na kutangaza azimio la kufanya maandamano siku ya Jumapili kwa lengo la kulaani mgomo wa madaktari unaoendelea nchini!

Awali maandamano hayo yalipangwa kufanyika kesho Jumamosi,lkn yakaahirishwa ili kupisha mazungumzo kati ya Rais Kikwete na viongozi wa chama cha madaktari.Sina hakika na tafsiri ya neno 'wanaharakati wazalendo',iwapo maana yake ni kuwa kuna wanaharakati mamluki au la,lkn hili si lengo langu.

Kilichonisukuma kuandika hii thread ni kwanza jinsi walivyowashambulia madaktari waliogoma.Niliudhika na kauli yao kuwa madaktari wasijifanye ni watu muhimu sana kuliko wengine na kadhalika.Sasa nikajiuliza,kama madaktari si muhimu,kuna umuhimu gani wa kuweweseka kuwataka warudi kazini?Kwa nn tusiwaache tu waendelee na mgomo?

Pili,ni namna kibali cha maandamano yao kilivyotolewa chapchap na polisi,tofauti na maandamano mengine ya watu wengine ambapo hudaiwa kuna taarifa za kiintelijensia kuwa kutakuwa na uvunjifu wa amani!

Hapa utagundua kuwa kumbe ili upate kibali cha kuandamana,inabidi lengo la maandamano yako liwe ni kuunga mkono upande wa chama tawala au serikali na si kwa kigezo cha maandamano ya amani.

Ni dhahiri kuwa kikundi kingine kikioma kibali cha kuandamana kwa lengo la,mfano,kuunga mkono mgomo wa madaktari hakutakuwa na kibali kitakachotolewa na hata kama kitatolewa na maandamano hayo yakafanyika sambamba na haya ya 'wanaharakati wazalendo' polisi watatembeza bakora upande mmoja.

Kwa hiyo hii intelijensia ya hawa jamaa huwa ni janja ya kisiasa tu.
 
Kikundi cha watanzania wanaojiita wanaharakati wazalendo leo kimeitisha mkutano na waandishi wa habari na kutangaza azimio la kufanya maandamano siku ya Jumapili kwa lengo la kulaani mgomo wa madaktari unaoendelea nchini!
Pili,ni namna kibali cha maandamano yao kilivyotolewa chapchap na polisi,tofauti na maandamano mengine ya watu wengine ambapo hudaiwa kuna taarifa za kiintelijensia kuwa kutakuwa na uvunjifu wa amani!

Ni dhahiri kuwa kikundi kingine kikioma kibali cha kuandamana kwa lengo la,mfano,kuunga mkono mgomo wa madaktari hakutakuwa na kibali kitakachotolewa na hata kama kitatolewa na maandamano hayo yakafanyika sambamba na haya ya 'wanaharakati wazalendo' polisi watatembeza bakora upande mmoja.

Kwa hiyo hii intelijensia ya hawa jamaa huwa ni janja ya kisiasa tu.


Yaani hawa ni kikundi cha Watu ambao wamewekwa kama mamluki wa Serikali, ili kuwafunga macho Madakitari na wote wenye nia ya kutetea haki zao tuone kuwa huu mgomo Wananchi tunaupinga.

Mimi binafsi jana niliwasikiliza wale jamaa katika television ya ITV, jinsi walivyokuwa wanaongea kwa jazba lisilo kuwa na point kabisa. Walikuwa wanatakiwa watoe sababu ya kutushawishi sisi wananchi tuwaunge mkono katika maandamano hayo, lakini eti badala yake wao wanalazimisha kuwa Madakitari warudi kazini na wasipo rudi Serikali iwafukuze wote na hata wakiendanda nchi zingine basi serikali iwasiliane na hizo nchi ili wafukuzwe.

HIVI WANA AKILI TIMAMU KWELI WALE. NILIMSIKILIZA MWISHO NIKATEMA MATE JINSI WALIVYONIKERA. PTYUUUUUUUUUUUUUUU!!!!!

Wanaongea kama wapo katika vijiwevya kunywa kahawa. Hawana na point ya kuonyesha kuwa ni wasomi wenye uelewa na wanachokiongea. Ni watu wenye njaa wameokotwa na kupandikizwa kuturubuni.

Yaani serikali iwafukuze madakitari wote waliogoma, AKILI ZAO ZIMEGANDA KWELI WALE, AU KUNA NATI IMEOTA KUTU KICHWANI MWAO; ETI NI WANAHARAKATI HIVI WANAUA MAANA YAKE AU WANAVAMIA FANI ZA WATU KUJIITA MWANAHARAKATI.

MTU MWENYE AKILI TIMAMU HAWEZI KUONGEA KAMA WALIVYOKUWA WANAONGEA WALE VIDAMPA JANA!!!!


Nilitegemea watalazimisha kuwe na maongezi kati ya Madakitari na Serikali ili suala hili liishe mapema na kwa amani. Lakini badala yake wakaongea pumba heri hata mtoto mdogo wa Nursery school ana akili kulikoni wale watu wazima ovyo.



ANGALIZO:

(1) Jeshi la Polisi kama limewapatia kibali wale waandamane Jumapili, basi wawe tayari hata watu wengine wakitaka kibali pia wapewe bila masharti. Mfano Kikundi kingine kikitaka kibali kuandamana kuunga mkono mgomo wa madakitari pia wapewe.

(2) Hawa Waandamanaji popote watakapopita Wananchi wenye mapenzi mema na nchi hii tuwazomee hadi wajione kama wamajinyea.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Intelegensia ya Tanzania huona mambo ya kufikirika yasiyokuwepo na haioni mambo yanayoonekana. elimu na hekima yao ni jambo linalotia mashaka makubwa.
 
Back
Top Bottom