Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
SHIRIKISHO la vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), limeeleza kuwa watafanya maandamano ya amani Januari 29 mwaka huu kwa lengo la kupinga bei ya umeme na kuunga mkono mabadiliko ya Katiba mpya.
Hayo yalisema jana jijini Dar es Salaam na Kaimu Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholas Mgaya, amabaye alidai uamuzi huo ulifikiwa Alhamisi wiki hii katika kikao cha kamati ya utendaji ya shirikisho hilo.
Alisema maandamano hayo yatafanyika nchi nzima ambapo kamati ya utendaji ya shirikisho hilo imeazimia kupinga hatua ya serikali kupandisha bei ya umeme huku kiwango cha mishahara kwa wafanyakzi kikibaki kile kile.
Maandamano yetu ya amani yatafanyika nchi nzima kupinga serikali kupandisha gharama ya umeme huku mishahara ya watumishi ikibaki bila kuongezwa chochote, hatua ambayo inaonyesha kutaka kumnyonya mfanyakazi ambapo si haki, alisema Mgaya.
Alisema ili nchi yoyote iweze kupata maendeleo ya kasi ni lazima mazingira ya kazi ya wafanyakazi wake yaboreshwe na kuwa na nyongeza ya mishahara.
Mgaya alisema kwa sasa wameunda kamati maalumu itakayokuwa chini yake ili kuweza kurartibu taratibu za kisheria ikiwamo kuandika barua kwa Jeshi la Polisi na kupata baraka za kufanya maandamano hayo ya amani.
Hayo yalisema jana jijini Dar es Salaam na Kaimu Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholas Mgaya, amabaye alidai uamuzi huo ulifikiwa Alhamisi wiki hii katika kikao cha kamati ya utendaji ya shirikisho hilo.
Alisema maandamano hayo yatafanyika nchi nzima ambapo kamati ya utendaji ya shirikisho hilo imeazimia kupinga hatua ya serikali kupandisha bei ya umeme huku kiwango cha mishahara kwa wafanyakzi kikibaki kile kile.
Maandamano yetu ya amani yatafanyika nchi nzima kupinga serikali kupandisha gharama ya umeme huku mishahara ya watumishi ikibaki bila kuongezwa chochote, hatua ambayo inaonyesha kutaka kumnyonya mfanyakazi ambapo si haki, alisema Mgaya.
Alisema ili nchi yoyote iweze kupata maendeleo ya kasi ni lazima mazingira ya kazi ya wafanyakazi wake yaboreshwe na kuwa na nyongeza ya mishahara.
Mgaya alisema kwa sasa wameunda kamati maalumu itakayokuwa chini yake ili kuweza kurartibu taratibu za kisheria ikiwamo kuandika barua kwa Jeshi la Polisi na kupata baraka za kufanya maandamano hayo ya amani.