Maandamano ya chadema yapigwa stop

Averos

JF-Expert Member
Aug 6, 2010
993
695
Wakati huo huo, Jeshi la Polisi wilayani Songea, mkoani Ruvuma limezuia kufanyika kwa maandamano ya amani yaliyoitishwa na Chadema wilayani humo jana yenye lengo la kupinga uamuzi wa mkuu wa wilaya hiyo, Thomas Oley Sabaya, wa kuwanyima vocha za pembejeo za kilimo wakulima wa kata tisa kati ya kata 21 za Halmashauri ya Manispaa ya Songea zikiwemo kata 5 zinazoongozwa na Madiwani wa Chadema.
Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye ofisi za Chama hicho zilizopo Mfaranyaki mjini hapa, Mwenyekiti Chadema mkoa wa Ruvuma, Joseph Fuime, alisema kuwa Chadema wilaya ya Songea walipanga kufanya maandamano ambayo yalikuwa na madhumuni ya kupinga uchakachuaji wa vocha za pembejeo za wakulima uliofanywa na mkuu wa Wilya Sabaya
Fuime ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mjini kupitia Chadema, alisema kuwa taarifa ya kufanya maandamano hayo ilitolewa tangu Januari 7, mwaka huu kwa mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Songea, lakini ameshangaa kuona mkuu huyo wa polisi amethibitisha kufanya maandamano hayo kwa madai kuwa tatizo la wakulima kunyimwa vocha linashughulikiwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dk. Christine Ishengoma.
Ameeleza zaidi kuwa pamoja na Polisi kuzuia maandamano hayo kupitia barua yao iliyowafikia jana na kusainiwa na OCD Peter Kubezya yenye kumb,Na,SO/A.3/6/54, Chadema iliruhusiwa kufanya mkutano wa hadhara ambao ulifanyika kwenye soko la Samaki la zamani karibu na Shule ya Msingi Mfaranyaki
Alieleza zaidi kuwa sababu zilizotolewa na OCD Peter Kubezya ni dhaifu na zilizozeeka na kwamba Dk. Ishengoma alipaswa kuchukua hatua za haraka kuwakomboa wakulima toka pale tatizo lilipojitokeza Desemba 15, mwaka jana lililofanywa kwa makusudi na DC Sabaya ambapo maamuzi ya ajabu ya kukiukwa kikao cha wadau wa kilimo kilichofanyika Novemba 12, mwaka jana ambacho kiliazimia kuwa wakulima wa kata za Manispaa ya Songea wakachukulie vocha za mbolea ya ruzuku kwenye maeneo yao wanayoishi ambapo kuna kamati za pembejeo za kata ambazo zinawafahamu wakulima husika
Fuime alisema kuwa Polisi wanapaswa kulinda raia na mali zao na kwamba hawapaswi kutumia uwepo wao kuwadhulumu wananchi haki zao, ikiwemo ya kupewa mbolea katika kata zinazoongozwa na madiwani wa Chadema za Mjini, Lizaboni, Majengo, Bombambili na Misufini na kata nyingine nne za Matarawe, Mjimwema, Ruvuma na Seedfarm.
Idadi kubwa ya skari polisi walikuwa wamemwagwa kwenye eneo la mkutano na wengine wakiwa wanazunguka kwenye magari yao wakiwa na silaha mbalimbali toka saa 5:00 asubuhi kabla ya mkutano uliopangwa kuanza saa 10: alasiri.
Hata hivyo, jitihada za kumpata OCD Kubezya hazikuweza kufanikiwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamuhanda, alipohojiwa kwa njia ya simu alikana jeshi lake kuzuia maandamano hayo, lakini katika barua yake aliyoiandikia Chadema ambayo gazeti hili limefanikiwa kupata nakala yake, OCD Kubezya amempelekea nakala Kamuhanda, DC Sabaya na Afisa Usalama wa wilaya.
NIPASHE
 
Wakati huo huo, Jeshi la Polisi wilayani Songea, mkoani Ruvuma limezuia kufanyika kwa maandamano ya amani yaliyoitishwa na Chadema wilayani humo jana yenye lengo la kupinga uamuzi wa mkuu wa wilaya hiyo, Thomas Oley Sabaya, wa kuwanyima vocha za pembejeo za kilimo wakulima wa kata tisa kati ya kata 21 za Halmashauri ya Manispaa ya Songea zikiwemo kata 5 zinazoongozwa na Madiwani wa Chadema.
Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye ofisi za Chama hicho zilizopo Mfaranyaki mjini hapa, Mwenyekiti Chadema mkoa wa Ruvuma, Joseph Fuime, alisema kuwa Chadema wilaya ya Songea walipanga kufanya maandamano ambayo yalikuwa na madhumuni ya kupinga uchakachuaji wa vocha za pembejeo za wakulima uliofanywa na mkuu wa Wilya Sabaya
Fuime ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mjini kupitia Chadema, alisema kuwa taarifa ya kufanya maandamano hayo ilitolewa tangu Januari 7, mwaka huu kwa mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Songea, lakini ameshangaa kuona mkuu huyo wa polisi amethibitisha kufanya maandamano hayo kwa madai kuwa tatizo la wakulima kunyimwa vocha linashughulikiwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dk. Christine Ishengoma.
Ameeleza zaidi kuwa pamoja na Polisi kuzuia maandamano hayo kupitia barua yao iliyowafikia jana na kusainiwa na OCD Peter Kubezya yenye kumb,Na,SO/A.3/6/54, Chadema iliruhusiwa kufanya mkutano wa hadhara ambao ulifanyika kwenye soko la Samaki la zamani karibu na Shule ya Msingi Mfaranyaki
Alieleza zaidi kuwa sababu zilizotolewa na OCD Peter Kubezya ni dhaifu na zilizozeeka na kwamba Dk. Ishengoma alipaswa kuchukua hatua za haraka kuwakomboa wakulima toka pale tatizo lilipojitokeza Desemba 15, mwaka jana lililofanywa kwa makusudi na DC Sabaya ambapo maamuzi ya ajabu ya kukiukwa kikao cha wadau wa kilimo kilichofanyika Novemba 12, mwaka jana ambacho kiliazimia kuwa wakulima wa kata za Manispaa ya Songea wakachukulie vocha za mbolea ya ruzuku kwenye maeneo yao wanayoishi ambapo kuna kamati za pembejeo za kata ambazo zinawafahamu wakulima husika
Fuime alisema kuwa Polisi wanapaswa kulinda raia na mali zao na kwamba hawapaswi kutumia uwepo wao kuwadhulumu wananchi haki zao, ikiwemo ya kupewa mbolea katika kata zinazoongozwa na madiwani wa Chadema za Mjini, Lizaboni, Majengo, Bombambili na Misufini na kata nyingine nne za Matarawe, Mjimwema, Ruvuma na Seedfarm.
Idadi kubwa ya skari polisi walikuwa wamemwagwa kwenye eneo la mkutano na wengine wakiwa wanazunguka kwenye magari yao wakiwa na silaha mbalimbali toka saa 5:00 asubuhi kabla ya mkutano uliopangwa kuanza saa 10: alasiri.
Hata hivyo, jitihada za kumpata OCD Kubezya hazikuweza kufanikiwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamuhanda, alipohojiwa kwa njia ya simu alikana jeshi lake kuzuia maandamano hayo, lakini katika barua yake aliyoiandikia Chadema ambayo gazeti hili limefanikiwa kupata nakala yake, OCD Kubezya amempelekea nakala Kamuhanda, DC Sabaya na Afisa Usalama wa wilaya.
NIPASHE

Aibu tupu, aibu tupu. Aibu Tanzania
 
hivi kwa nini maandamano yanaogopwa lakini mkutano ruksa? Kuna nini katika maandamano lakini hakipo ktk mkutano?
 
Wakati huo huo, Jeshi la Polisi wilayani Songea, mkoani Ruvuma limezuia kufanyika kwa maandamano ya amani yaliyoitishwa na Chadema wilayani humo jana yenye lengo la kupinga uamuzi wa mkuu wa wilaya hiyo, Thomas Oley Sabaya, wa kuwanyima vocha za pembejeo za kilimo wakulima wa kata tisa kati ya kata 21 za Halmashauri ya Manispaa ya Songea zikiwemo kata 5 zinazoongozwa na Madiwani wa Chadema.
Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye ofisi za Chama hicho zilizopo Mfaranyaki mjini hapa, Mwenyekiti Chadema mkoa wa Ruvuma, Joseph Fuime, alisema kuwa Chadema wilaya ya Songea walipanga kufanya maandamano ambayo yalikuwa na madhumuni ya kupinga uchakachuaji wa vocha za pembejeo za wakulima uliofanywa na mkuu wa Wilya Sabaya
Fuime ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mjini kupitia Chadema, alisema kuwa taarifa ya kufanya maandamano hayo ilitolewa tangu Januari 7, mwaka huu kwa mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Songea, lakini ameshangaa kuona mkuu huyo wa polisi amethibitisha kufanya maandamano hayo kwa madai kuwa tatizo la wakulima kunyimwa vocha linashughulikiwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dk. Christine Ishengoma.
Ameeleza zaidi kuwa pamoja na Polisi kuzuia maandamano hayo kupitia barua yao iliyowafikia jana na kusainiwa na OCD Peter Kubezya yenye kumb,Na,SO/A.3/6/54, Chadema iliruhusiwa kufanya mkutano wa hadhara ambao ulifanyika kwenye soko la Samaki la zamani karibu na Shule ya Msingi Mfaranyaki
Alieleza zaidi kuwa sababu zilizotolewa na OCD Peter Kubezya ni dhaifu na zilizozeeka na kwamba Dk. Ishengoma alipaswa kuchukua hatua za haraka kuwakomboa wakulima toka pale tatizo lilipojitokeza Desemba 15, mwaka jana lililofanywa kwa makusudi na DC Sabaya ambapo maamuzi ya ajabu ya kukiukwa kikao cha wadau wa kilimo kilichofanyika Novemba 12, mwaka jana ambacho kiliazimia kuwa wakulima wa kata za Manispaa ya Songea wakachukulie vocha za mbolea ya ruzuku kwenye maeneo yao wanayoishi ambapo kuna kamati za pembejeo za kata ambazo zinawafahamu wakulima husika
Fuime alisema kuwa Polisi wanapaswa kulinda raia na mali zao na kwamba hawapaswi kutumia uwepo wao kuwadhulumu wananchi haki zao, ikiwemo ya kupewa mbolea katika kata zinazoongozwa na madiwani wa Chadema za Mjini, Lizaboni, Majengo, Bombambili na Misufini na kata nyingine nne za Matarawe, Mjimwema, Ruvuma na Seedfarm.
Idadi kubwa ya skari polisi walikuwa wamemwagwa kwenye eneo la mkutano na wengine wakiwa wanazunguka kwenye magari yao wakiwa na silaha mbalimbali toka saa 5:00 asubuhi kabla ya mkutano uliopangwa kuanza saa 10: alasiri.
Hata hivyo, jitihada za kumpata OCD Kubezya hazikuweza kufanikiwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamuhanda, alipohojiwa kwa njia ya simu alikana jeshi lake kuzuia maandamano hayo, lakini katika barua yake aliyoiandikia Chadema ambayo gazeti hili limefanikiwa kupata nakala yake, OCD Kubezya amempelekea nakala Kamuhanda, DC Sabaya na Afisa Usalama wa wilaya.
NIPASHE

Pamoja na kiwewe cha serikali ya ccm kufuatia kuporomoka kwa kura zao katika uchaguzi mkuu uliopita na hofu yao juu ya kupanda chati kwa chadema lakini pia jeshi la polisi nalo lina udhaifu mkubwa sana, sijui ni kwa sababu wengi wa waajiriwa wa jeshi hilo ni failures? manake wengi wanaingia polisi kwa elimu za kuunga unga tu ndio maana hawajiamini katika maamuzi yao wala hawajui kutafsiri na kusimamia sheria.

Jambo la pili ni huyo mkuu wa wilaya Ole sabaya, ni miongoni mwa watu wapuuzi sana ambao nimepata kuwashuhudia, nadhani huyu mtu huwa hatumii akili yake vizuri. Tangu akiwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya arumeru alipozua zogo hadi wamasai wakaandamana na kutaka kuanzisha vita na uongozi wa wilaya na mkoa ndipo alilazimishwa kuachia ngazi. Alipoteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya serengeti ndio kabisa akalewa madaraka, akadiriki kuchoma moto nyumba za wananchi kwa kisingizio cha kuingia kwenye pori la akiba la grumeti ilihali alikuwa amapewa mlungula na "mwekezaji" ili kuwaondoa wananchi kwenye ardhi yao wanayoimmiliki na kuitumia tangu enzi za mababu zao kabla ya kuundwa kwa taifa la Tanganyika. Mtakumbuka hapa lile sakata la Wananchi wa Nyamuma ambalo tume ya haki za binadamu chini ya jaji mstaafu Dr. Kisanga ilithibitisha pasipo shaka uhuni na unyama uliofanywa na sabaya dhidi ya wananchi hao, na hadi leo serikali bado haijawalipa.

Huyu ole sabaya ni kirusi ndani ya jamii ya watanzania, hafai hata kuwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa lakini kwa kuwa ni ccm basi huyo ndiye kiongozi bora. Wananchi wa songea msirudi nyuma, bila kupigania haki zenu ole sabaya ataendelea kuwakandamiza.
 
Hivi maandamano ya amani si polisi wanatakiwa kutoa ulinzi ili yawe ya amani kweli?? Kwa nini hawatoi ulinzi na badala yake wanayazuia?
Hivi siku CCM nao wakitaka kufanya maandamano ya amani watazuiwa??
 
Kwa hali ninayoina inabidi tubadilike jamani maana huko tunakoenda siko kabisa forum kama hii inakua ya kichama zaidi badala ya kuwa ya kimapinduzi hasa ya fikra. Mtu unakuta afanya kazi ofisi fulani na ina urasimu mkubwa alafu hapa anauliza hivi nchi hii ina uongozi kweli? uongozi ni mimi na wewe. na JF yapaswa iwe kwa minajiri ya kufanya mageuzi ya kifikra hasa kwa vijana ambao ndio kundi maalumu lenye tatizo ambalo hakuna anayeliaddress ambalo ni ukosefu wa ajira.
 
Pamoja na kiwewe cha serikali ya ccm kufuatia kuporomoka kwa kura zao katika uchaguzi mkuu uliopita na hofu yao juu ya kupanda chati kwa chadema lakini pia jeshi la polisi nalo lina udhaifu mkubwa sana, sijui ni kwa sababu wengi wa waajiriwa wa jeshi hilo ni failures? manake wengi wanaingia polisi kwa elimu za kuunga unga tu ndio maana hawajiamini katika maamuzi yao wala hawajui kutafsiri na kusimamia sheria.

Jambo la pili ni huyo mkuu wa wilaya Ole sabaya, ni miongoni mwa watu wapuuzi sana ambao nimepata kuwashuhudia, nadhani huyu mtu huwa hatumii akili yake vizuri. Tangu akiwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya arumeru alipozua zogo hadi wamasai wakaandamana na kutaka kuanzisha vita na uongozi wa wilaya na mkoa ndipo alilazimishwa kuachia ngazi. Alipoteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya serengeti ndio kabisa akalewa madaraka, akadiriki kuchoma moto nyumba za wananchi kwa kisingizio cha kuingia kwenye pori la akiba la grumeti ilihali alikuwa amapewa mlungula na "mwekezaji" ili kuwaondoa wananchi kwenye ardhi yao wanayoimmiliki na kuitumia tangu enzi za mababu zao kabla ya kuundwa kwa taifa la Tanganyika. Mtakumbuka hapa lile sakata la Wananchi wa Nyamuma ambalo tume ya haki za binadamu chini ya jaji mstaafu Dr. Kisanga ilithibitisha pasipo shaka uhuni na unyama uliofanywa na sabaya dhidi ya wananchi hao, na hadi leo serikali bado haijawalipa.

Huyu ole sabaya ni kirusi ndani ya jamii ya watanzania, hafai hata kuwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa lakini kwa kuwa ni ccm basi huyo ndiye kiongozi bora. Wananchi wa songea msirudi nyuma, bila kupigania haki zenu ole sabaya ataendelea kuwakandamiza.

Mwita hiyo picha hapo kushoto ina hati miliki lazima unilipe kwa kuitumia bila kupata ruhusa yangu..off point!
 
Kwa hali ninayoina inabidi tubadilike jamani maana huko tunakoenda siko kabisa forum kama hii inakua ya kichama zaidi badala ya kuwa ya kimapinduzi hasa ya fikra. Mtu unakuta afanya kazi ofisi fulani na ina urasimu mkubwa alafu hapa anauliza hivi nchi hii ina uongozi kweli? uongozi ni mimi na wewe. na JF yapaswa iwe kwa minajiri ya kufanya mageuzi ya kifikra hasa kwa vijana ambao ndio kundi maalumu lenye tatizo ambalo hakuna anayeliaddress ambalo ni ukosefu wa ajira.

Nani kakudanganya kwamba uongozi ni mimi na wewe? au unazungumzia nadharia ndugu yangu, watu wanazungumza kutokana na uzoefu na ukweli wa mamabo wanaoushuhudia. Kama katiba inampatia haki mwananchi kuandamana na kukusanyika, inakuwaje tena kiongozi huyo huyo ambaye ni wewe na mimi tuzuiwe na polisi ama kupigwa risasi za moto na mabou badala ya kutupatia ulinzi?
Nchi hii hatuna viongozi, tuna watawala na katika hili hatuna sababu yoyote kujifariji kwamba tuna viongozi.
 
Hivi siku CCM nao wakitaka kufanya maandamano ya amani watazuiwa??
Ili kuadaa watanzania ipo siku CCM nao watajifanya wanataka kufanya maandamano ya amani na jeshi la polisi litawakatalia ili ionekane kama ni jambo la kawaida polisi kujuia maandamano!!
 
Kwa tanzania hii inahitaji dictator tu. swala la kuandamana lina misingi na taratibu yake katiba inasema uandamane lakini usivunje sheria utafute haki lakini siyo kwa kukandamiza haki ya mwingine. Kiongozi ni mimi na wewe narudia tena hao mabwana wakubwa wao ni watawala na ndicho tulichorithi toka kwa wakoloni hata iweje watabaki hivyohivyo na tena tuendako watakuwa mabwana nasi watwana kama tusipojitambua. Unajua lema hana sera ana ubabe ni sawa na mbowe. Msikilize Slaa au zito vyema alafu uwasikilize lema, mbowe etc alafu utafakari.
 
Hivi hii nchi inauongozi kweli? Kazi tunayo!

Uongozi tunao, si ndo huo uliopo madarakani?, ila unaweza ukawa sio uongozi makini, au si uongozi kwa waajili wa wananchi, Mwalimu wangu Plato anasema "tunahitaji Philosopher King, ambae atakuwa na uwezo wa kutofautisha kati ya muonekano na kile kinachotoa muonekano", anayeweza kutofautisha kati ya ukweli na maoni na kuwapeleka watu kule wanakohitaji kufika kwa manufaa ya wote"
 
kwahiyo hata maendeleo nayo kwa mgao? limeni hivyo hivyo kwani sauti ya mnyonge husikiwa na mungu. siku zinahesabika.
 
Hii inanikumbusha ule usemi unaosema "things fall apart........no longer at easy". Hiki chama cha mafisadi kijuwe ya kuwa wa-tz wa miaka ya 47 hawapo tena na hawawezi kutuchezea tena......wajue kuwa nchi hii ni yakwetu na wala wao sio wamiliki. we want our country back and we gonna take it come sun come rain. Enough is enough.
 
Back
Top Bottom