ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,906
- 6,909
Guyz,
Naombeni mnielewe, msione kama mimi napinga kila kitu. Na mimi nilisoma kwenye chuo hicho hicho na migomo ilikuwepo. Ukijaribu kufanya analyis ya migomo ya miaka hii, yote ni yakitoto, kwanza hawapo organized. Wanajigomea tu, hawana common objective!Wanaogoma ni kikundi tu cha wanafunzi. Migomo imekuwa inafanywa kila siku kudai vitu ambavyo hata havina msingi. Haipose threat yoyote kwa serikali. Miaka yetu ilikuwa ukisikia chuo kikuu wamegoma(miaka hiyo kilikuwa kimoja tu) kila mtu alikuwa anatetemeka. Siku hizi imeshakuwa routine! Tumeshaona ni kitu cha kawaida, ndio maana mwaka jana UD waligoma 3 dayz mfulululizo lakini chuo hakikufungwa wakati kisheria ingetakiwa kifungwe!
Kipindi kile mlikuwa na common objectives kwa kuwa majority mlikuwa ni watoto toka vijijini, uchumi wenu ulifanana na hali ya kiuchumi ya taifa ilikuwa inawafanya hata matajiri waonekane maskini hivyo mlipmbana kama wamoja.
Rejao wewe siku hizi ni matawi ya juu, uchumi wako uko juu, tayari ulisha mwandaa mwanao kufikiria kibepari kwani pesa unazo, na mwanao kwa ujinga uliomlisha na kuona yeye ana hela za kutosha, huwezi kumwondoa kwenye thinking hiyo.
Kinachofanyika, ni kwa wale majority ambao hali zetu bado ziko chini kuwalazimisha hata mwanao akubaliane na matakwa ya maskini, na akigoma, lazima kiboko achapwe kumlazi9misha kufikiria waliowengi maskini kazi ambayo wewe uliitelekeza kwa kumlea mwanao atambue pesa/nafasi uliyonayo imetokana na uwezo wako wakati ukweli siyo