Maandamano makubwa zanzibar kupinga rasimu ya katiba mpya

Malaria Sugu

JF-Expert Member
Jul 7, 2009
2,653
264
katiba-ya-tanzania-564x272.jpg

Jumuiya ya uamsho na mihadhara ya kiislam, JUMIKI, imeandaa maandamo ya amani ya kupinga rasimu ya muswaada wa katiba ya Muungano.
Maandamano hayo yanayotegemea kufanyika kesho baada ya swalah ya Ijumaa yataanzia msikiti wa Ijumaa malindi na kumalizikia kwenye viwanja vya Lumumba.
Hadi tunafika kutoa taarifa hii kibali bado hakijapatikana, lakini waandalizi wamesema wapo kwenye subira na hawaoni sababu ya Polisi kuwanyima kibali cha kufanyia maandamano hayo ya amani
 
Polisi Zanzibar wameshayapiga stop maandamano hayo. Kwa taarifa nilizo nazo maandamano hayatafanyika kwa sababu polisi wamesema suala la udini linaweza kuleta uvunjifu wa amani.
 
Hao ni Polisi wa CCM hatushangai. Kuingiza sababu za kidini ni woga wa watawala tu kwani sijapata kuona watu woga kama CCM.

Maandamano wanaweza kuyazuia lakini chehe ya mabadiliko haizimiki tena kamwe.

Keep watching this page.
 
yakheeeee naomba mzidi kunifahamisha maana hii mijitu ya sisi embu ni tabuuu kweli kweli...
 
Maandamano ya amani kupinga rasimu ya muswada wa katiba yanageukaje kuwa udini?? Polisi kweli hamnazo. Wazanzibar komaeni, kitaeleweka tu.
 
Polisi Zanzibar wameshayapiga stop maandamano hayo. Kwa taarifa nilizo nazo maandamano hayatafanyika kwa sababu polisi wamesema suala la udini linaweza kuleta uvunjifu wa amani.
Udini uko wapi sasa?
 
Hao ni Polisi wa CCM hatushangai. Kuingiza sababu za kidini ni woga wa watawala tu kwani sijapata kuona watu woga kama CCM.

Maandamano wanaweza kuyazuia lakini chehe ya mabadiliko haizimiki tena kamwe.

Keep watching this page.
uvunjifu wa aman unatumika kama kisingizio na chama cha magamba kukanyaga haki za wa-tz.
 
katiba-ya-tanzania-564x272.jpg

Jumuiya ya uamsho na mihadhara ya kiislam, JUMIKI, imeandaa maandamo ya amani ya kupinga rasimu ya muswaada wa katiba ya Muungano.
Maandamano hayo yanayotegemea kufanyika kesho baada ya swalah ya Ijumaa yataanzia msikiti wa Ijumaa malindi na kumalizikia kwenye viwanja vya Lumumba.
Hadi tunafika kutoa taarifa hii kibali bado hakijapatikana, lakini waandalizi wamesema wapo kwenye subira na hawaoni sababu ya Polisi kuwanyima kibali cha kufanyia maandamano hayo ya amani

Rasimu ya mswada wa Marejeo ya Katiba. Rasimu ya Katiba Mpya bado. Huu ni mswada wa kuunda tume ya kukusanya maoni.
 
Polisi Zanzibar wameshayapiga stop maandamano hayo. Kwa taarifa nilizo nazo maandamano hayatafanyika kwa sababu polisi wamesema suala la udini linaweza kuleta uvunjifu wa amani.

Kivipi wakati waZanziberi karibu wote ni dini moja?!
 
Hata wasipowapa kibali andamaneni kwani usitarajie hata siku moja watawale wawape haki yenu mkiwa mmelala majumbani mwenu.

Haki hutafutwa ikiwezekana kwa nguvu. Hata Outarra kama asingepigania haki yake kwa nguvu Gbagbo asingeondoka.

Hivyo mkomae hata wakiwanyima kibali muandamane kwa nguvu
 
Huku bara mara nyingi lawama huwaendea CDM kwa kila maandamano na huko vipi ?
 
Back
Top Bottom