Maandamano makubwa Songea!

skendo

JF-Expert Member
Apr 9, 2011
212
101
Wakuu nimepigiwa simu na rafiki'angu toka Songea anasema kumekuwa na mauwaji ya kutisha kwa mda wa wiki sasa na inasemekana watu zaidi ya kumi wamesha uwawa ingawa RPC amedai wananchi wasihofu.

Pia nasikia wananchi waliandamana mpaka kwa mkuu wa Wilaya ila bado uvumbuzi haujapatikana na inasemekana wananchi waliwachoma moto watu wawili kutokana na tuhuma za kuhusika na mauwaji hayo na ndipo wauwaji wakasema sasa wataendeleza mashamulizi.

Mwenye ndugu pande hizo anaweza mpigia simu ili tuweze pata taarifa zaidi ila kuna jamaa yangu mwingine ni polisi nae ameniakikishia kuwa hali si nzuri kwa sasa.
Kwa mliosikiliza radio na kuangalia ITV mmejulishwa kinachojiri songea asubuhi hii ni mapambano ya askari na raia

CHANZO CHA MAPAMBANO
Kuna raia wanauawa tangu juzi na matukio yanaripotiwa ila askari hawachukui hatua yeyote ile zaidi wanasema ushahidi hawajauona,usiku wa kuamkia leo limekua tukia la 5 raia kuuliwa na askari kama kawaida yao hawatoi ulinzi kwa raia wao.

Asubuhi raia (Watoto, vijana, wazee) wakaamua kuwatolea uvivu askari na kuandamana hadi kituo cha polisi kudai haki ya kulindwa na kuishi raia walikua wengi kuliko uwezo wa askari wa kile kituo hivyo waliona hapa wakiwa wakali kituo kitachomwa moto maaana walikuja na jazba raia wakawaambia taarifa ziko kwa mkuu wa wilaya raia bila simile wakaanza maandamano hadi kwa mkuu wa wilaya kufika huko naye akanawa mikono kama pilato akasema mkuu wa mkoa ndo liko mikononi mwake.

Raia hawakuishia hapo wakalianzisha hadi kwa mkuu wa mkoa huku wakiimba "TUMECHOKA KUUWAWA" hadi kwa mkuu wa mkoa, hapo ndo movie ilpoanzia kumbe raia wakati wanaenda kwa mkuu wa mkoa inaaminika simu zilipigwa kwa mkuu wa mkoa na askari wanaolinda (FFU) wakafunga geti hapo ndo ikawa vuta nikuvute raia wakaweka kambi nje huku wanaimba nyimbo "MKUU WA MKOA UNAWAOGOPA RAIA WAKO JIUZURU", muda si mrefu gari ya FFU likawasiri likiwa na askari wa kutosha kwa vile raia hawakua na silaha wala ugomvi wakaamua kubaki huku wanaimba.

Askari kama kawaida yao wakawa wanazidi kusogelea huku wakitoa ishara wananchi watawanyike huku wananchi wakigoma hawatoki hadi mkuu wa mkoa naye atoke nje hapo ndo askari wakaanza kufyatua risasi za moto na raia wawili wakafa.habari zikafika mjini raia wameuliwa na askari hapo ndo mji ukazizima raia wakaingia mitaani askari waliokua mitaani walianza kupata upinzani mkali hd askari wawili wamekufa hadi hivi sasa, imebidi jeshi liingilie kati na mji wote kufungwa hivi ss mjini ni makundi ya wanajeshi na askari ndo yametawala hakuna maduka wala mabenki yanayofanya kazi

VIFO
Nimeshuhudia raia wawili na askari mmoja tu kwa macho yangu kwa sehem niliyokuwepo,kiujumla inasadikiwa raia zaidi ya wa4 na askari 2 ndo wamekufa,mji umepoa kabisa na mm ndo niko nyumbani ila ntarudi later mjini kuchukua news zaidi ili niwajulishe


Nawakilisha


Kwa mujibu wa Wananchi wa mji wa Songea walishatoa taarifa kwa RPC, kuhusu mauaji yanayo fanyika songea kila siku, RPC akasema hakuna kitu kama hicho (kama kawaida dharau), sasa leo asubuhi kuna raia mwingine tena mmoja amefariki kwa kupigwa risasi, wananchi baada ya kuona hali hiyo wakaanza kuandamana kuelekea ofisi ya mkuu wa wilaya, Ndipo wale jamaa wasio kuwa na kazi ya kufanya (FFU) walipopigiwa simu na kuja kutoa kichapo kwa raia ambao wanakufa kama wanyama.
PICT0021-1.jpg
PICT0024-2.jpg
PICT0020.jpg
PICT0024-1.jpg
 
Wakuu nasikia kuna mtu mwingine ameuwawa leo hii na wananchi wako kwenye harakati za kuandamana.mwenye ndugu pande izo ajaribu ulizia tujuwe ukweli wakuu
 
Uletaji wa taarifa wa namna hii na unataka watu wajadili sidhani kama unakubalika kwenye jukwaa makini kama hili.Wewe ndio mleta taarifa sasa unataka nani mwingine atoe taarifa? Sisi hatujui wewe ndio unajua sana unauliza kwetu ili iweje?
 
Uletaji wa taarifa wa namna hii na unataka watu wajadili sidhani kama unakubalika kwenye jukwaa makini kama hili.Wewe ndio mleta taarifa sasa unataka nani mwingine atoe taarifa? Sisi hatujui wewe ndio unajua sana unauliza kwetu ili iweje?

Kaka mbona wewe unaonekana mzoefu hapa JF ..........wewe kama hunandugu Songea tulia..........acha wenye jamaa songea wapige kisha tutajua kinachoendelea.
 
Taarifa nilizopata mda huu nikwamba polisi wanawatawanya raia kwa mabomu ya machozi.

Pia watu wanashangaa kwanini vyombo vya habari vinafumbia macho hili jambo.

Ila habari za kule saiti zinadai ni watu toka msumbiji,wengine wanadai kuna vigogo wanahusishwa ni kwa mambo ya kishirikina ila ukweli kamili bado sijaufahamu nini hasa chanzo.
 
Maandamano makubwa songea kulaani polisi kwa kutochukua hatua kudhibiti mauaji ya raia yanayofanywa karibu kila siku katika mji wa songea.Mabomu ya machozi na risasi zinarindima kuwatawanya waandamanaji.
 
Tayari hadi sasa Raia mmoja ameshafariki kwa kupigwa risasi na polisi hali ni mbaya kupindukia.FFU wamejaa mji mzima wa songea wakitoa kichapo kwa Raia wema,wasio kuwa na hatia.
 
SACGOT inakuja huko ombeni mungu sana, mtanyan'ganywa mashamba yenu yote na kupigwa risasi za mchanganyiko wa moto na baridi, sisi wameogopa kuja huku kwenye vihamba vyetu
 
Kwa mujibu wa Wananchi wa mji wa Songea walishatoa taarifa kwa RPC, kuhusu mauaji yanayo fanyika songea kila siku, RPC akasema hakuna kitu kama hicho (kama kawaida dharau), sasa leo asubuhi kuna raia mwingine tena mmoja amefariki kwa kupigwa risasi, wananchi baada ya kuona hali hiyo wakaanza kuandamana kuelekea ofisi ya mkuu wa wilaya, Ndipo wale jamaa wasio kuwa na kazi ya kufanya (FFU) walipopigiwa simu na kuja kutoa kichapo kwa raia ambao wanakufa kama wanyama.
 
Hali inadhidi kuwa tete,wanafunzi wanalia,wengine wanakimbia,wametoka madarasani,mji mzima umejaa polisi,hali ni mbaya sana sana,hakuna maelewano kwa sasa,kijana alipigwa risasi kwa sasa amekimbizwa hospitali ya mkoa anatokea sehemu moja naitwa matarawe.
 
Jamani nimepata habari kuwa songea hali sio nzuri, kuna vita kubwa katika ya FFU na Bodaboda chanjo kuuwawa kwa dereva mmoja wa bodaboda. Aliekaribu atujuze jaman.

Nawakilisha.
 
Back
Top Bottom